Ozzie
JF-Expert Member
- Oct 9, 2007
- 3,217
- 1,259
Leo nimepigiwa simu na kaka yangu. Mazungumzo yetu yalikuwa kama hivi:
Bro: Hello Mambo vipi?
Mimi: Poa tu
Bro: Hapo nyumbani hawajambo?
Mimi: Tunamshukuru Mungu sisi wazima
Bro: Mnaendeleaje?
Mimi: Aaah! Huku hakuna issue. Mambo 50/50. Bado tunateseka na mgao wa umeme.
Bro: Sasa Ozzie, kuna shemeji yako anakaa mitaa ya chini kule karibu na mto. Anasema alikuwa anakuona mara nyingi ukipita na gari.
Mimi: Nani huyo shemeji? Mbona mimi simjui? (Ninadakia nikiwa na hofu, isije ikawa kuna sehemu nimeharibu)
Bro: Yupo kule chini, yeye anakufahamu. Anasema huwa mnaonana mara kwa mara.
Mimi: Dah! Labda nitakuwa namfahamu, ila kuna dada huwa anakuwa kama anaonesha dalili za kunifahamu, lakini huwa nakausha. Kwani yeye ni mweupe?
Bro: Hapana! Atakuwa siye. Yeye ni maji ya kunde.
Mimi: OK! Sasa kwa nini anaogopa kunisalimia au kujitambulisha.
Bro: Aaah! Sijui, ila nadhani anashindwa namna ya kukuanza
Mimi: Basi mwambie kama tutaonana tena asisite kunisalimia na kujitambulisha (maana kwa sasa nimepunguza mizunguko ya mitaa ile). Lakini sijaelewa ni shemeji yangu kivipi?
Bro: Nilizaa naye bwana.
Mimi: Mbona mimi sijui kama ulizaa na mtu mwingine zaidi ya mama Phine (Nikadakia).
Bro: Aah basi tu! Kwa sasa mtoto ni mkubwa sana. Anasoma form one shule ya . (Shule Fulani inasifika kwa kufaulisha wanafunzi)
Mimi: Aah, haiwezekani bwana. Kwanini unasema sasa baada ya miaka yote hiyo kupita? Mama anajua? (Baba alifariki kitambo)
Bro: Ndiyo, Mama anajua (Najua kanidanganya, Mama angejua angeniambia, na angemtafuta mtoto huyu)
Mimi: Sasa siku zote hizi nani anamhudumia mtoto? Wewe unapeleka pesa za matumizi na ada ya shule?
Bro: Hapana, sipeleki chochote. Yule dada ni mke wa mwanajeshi
Mimi: Duh, ina maana jamaa ameamua kuchukua mzigo wa kumtunza mtoto asiye wake.
Bro: Yeye hajui kama mtoto sio wake. Nilimpa mimba mkewe wakiwa kwenye ndoa.
Mimi: Duh! ebwanae? Ndiyo kipindi kile unavuta sigara na bangi nini? (kwa sasa ameokoka)
Bro: Aah! Mimi sijui. Sasa mwanamke kachanganyikiwa kichizi. Haachi kunipigia simu. Anasema siku zinapozidi kusonga mbele na ndivyo mtoto anavyozidi kufanana na mimi.
Mimi: Sasa si bora aende kwa mama kumtambulisha mtoto?
Bro: Kwanza anaogopa sana kwenda kwa Mama (naanza kujua Mama hajui), pili hata asipoogopa atamwambia nini yule mtoto. Unadhani anaweza mtambulisha kwamba ana baba mwingine?
Mimi: Yaani hapo balaa. Sasa mimi nitamwonaje huyo mtoto?
Bro: Nitamwambia akutafute mapema, akiwa na mtoto au hata asipokuwa naye
Mimi: Duh! Poa
Naombeni ushauri. Nimtafute huyu mtoto ili nimwone au nichunie tu.
Bro: Hello Mambo vipi?
Mimi: Poa tu
Bro: Hapo nyumbani hawajambo?
Mimi: Tunamshukuru Mungu sisi wazima
Bro: Mnaendeleaje?
Mimi: Aaah! Huku hakuna issue. Mambo 50/50. Bado tunateseka na mgao wa umeme.
Bro: Sasa Ozzie, kuna shemeji yako anakaa mitaa ya chini kule karibu na mto. Anasema alikuwa anakuona mara nyingi ukipita na gari.
Mimi: Nani huyo shemeji? Mbona mimi simjui? (Ninadakia nikiwa na hofu, isije ikawa kuna sehemu nimeharibu)
Bro: Yupo kule chini, yeye anakufahamu. Anasema huwa mnaonana mara kwa mara.
Mimi: Dah! Labda nitakuwa namfahamu, ila kuna dada huwa anakuwa kama anaonesha dalili za kunifahamu, lakini huwa nakausha. Kwani yeye ni mweupe?
Bro: Hapana! Atakuwa siye. Yeye ni maji ya kunde.
Mimi: OK! Sasa kwa nini anaogopa kunisalimia au kujitambulisha.
Bro: Aaah! Sijui, ila nadhani anashindwa namna ya kukuanza
Mimi: Basi mwambie kama tutaonana tena asisite kunisalimia na kujitambulisha (maana kwa sasa nimepunguza mizunguko ya mitaa ile). Lakini sijaelewa ni shemeji yangu kivipi?
Bro: Nilizaa naye bwana.
Mimi: Mbona mimi sijui kama ulizaa na mtu mwingine zaidi ya mama Phine (Nikadakia).
Bro: Aah basi tu! Kwa sasa mtoto ni mkubwa sana. Anasoma form one shule ya . (Shule Fulani inasifika kwa kufaulisha wanafunzi)
Mimi: Aah, haiwezekani bwana. Kwanini unasema sasa baada ya miaka yote hiyo kupita? Mama anajua? (Baba alifariki kitambo)
Bro: Ndiyo, Mama anajua (Najua kanidanganya, Mama angejua angeniambia, na angemtafuta mtoto huyu)
Mimi: Sasa siku zote hizi nani anamhudumia mtoto? Wewe unapeleka pesa za matumizi na ada ya shule?
Bro: Hapana, sipeleki chochote. Yule dada ni mke wa mwanajeshi
Mimi: Duh, ina maana jamaa ameamua kuchukua mzigo wa kumtunza mtoto asiye wake.
Bro: Yeye hajui kama mtoto sio wake. Nilimpa mimba mkewe wakiwa kwenye ndoa.
Mimi: Duh! ebwanae? Ndiyo kipindi kile unavuta sigara na bangi nini? (kwa sasa ameokoka)
Bro: Aah! Mimi sijui. Sasa mwanamke kachanganyikiwa kichizi. Haachi kunipigia simu. Anasema siku zinapozidi kusonga mbele na ndivyo mtoto anavyozidi kufanana na mimi.
Mimi: Sasa si bora aende kwa mama kumtambulisha mtoto?
Bro: Kwanza anaogopa sana kwenda kwa Mama (naanza kujua Mama hajui), pili hata asipoogopa atamwambia nini yule mtoto. Unadhani anaweza mtambulisha kwamba ana baba mwingine?
Mimi: Yaani hapo balaa. Sasa mimi nitamwonaje huyo mtoto?
Bro: Nitamwambia akutafute mapema, akiwa na mtoto au hata asipokuwa naye
Mimi: Duh! Poa
Naombeni ushauri. Nimtafute huyu mtoto ili nimwone au nichunie tu.