domokaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2010
- 3,545
- 1,719
Watanzania ni wepesi sana kupotoshwa. Kwanza tuangalie alichosema Msemakweli, na tuangalie nyaraka alizowasilisha na anayekuja na hoja mpya, awasilishe nyaraka. Naamini mwandishi wa makala hii (Kubenea) anazo nyaraka kuonyesha CCM walitumia fedha za EPA na si yeye tu wako wengi wenye maelezo kama hayo.
Ni vyema kuyaanika lakini si kusema Msemakweli kakosea. yeye kasema ushahidi alionao ndio huo. Mwingine aje sema na mimi ushahidi ni huu, ili wahusika wawafuate kina Maranda gerezani na si kuendelea kutuchezea akili.
Pia tuangalie Msemakweli ameleta matokeo gani tangu aaanike hayo masuala hadharani. Je kuna wakati wowote Serikali iliamka na kulishukia njuga suala hili? Je kuna wakati wowote Bunge liliamua kufany kitu chochote kama taasisi kabla ya hapo? Je kuna muda wowote Yusuph Manji alitoa taarifa yoyote kuhusu hili na kushutumu KAGODA yenyewe kutoa siri kabla ya hapo?
Yusuph Manji amedai kurejesha fedha alizopewa na KAGODA lakini hamtaji kAGODA ni nani. Yusuph Manji anadai KAGODA mwenyewe ndioe anayetoa siri. Waziri Meghji alituambia KAGODA ni usalama wa Taifa Je kuna ukweli wowote kuwa KAGODA ni usalama wa Taifa? Iweje Usalama wa Taifa ummpe hela Yusuph Manji kupeleka CCM halafu tena usalama wa Taifa utoe siri na nyaraka na kumpa Msemakweli.
Je, KAGODA ni usalama wa Taifa kweli? Au KAGODA ni muasi kutoka ndani ya CCM au KAGODA ni mmoja wa mafisadi ambaye aidha anataka au ametolewa kafara kuwaacha wengine wanusurike lakini yeye hataki kufa peke yake. Nani huyo KAGODA?
Yusuph Manji anamjua, Rais anamjua na CCM inamjua na wanajua nguvu zake na pengine hata inamuhofia.
Nadharia yangu ni kuwa KAGODA alitengeneza gamba na kulitumia kuwaficha wengine ndani ya gamba hilo. Akaonekana yeye peke yake. Sasa ametakiwa ajivue gamba ili abaki uchi.
Yeye alitengeneza gamba kuwaficha wengine kwa matarajio ya kufichwa na yeye kwani na wengine pia akiwafikisha walipo watakuwa na magamba ya kumficha. Wamemgeuka na kumtaka ajivue gamba abaki uchi. Kwa kuwa staha yake inaharibika wakati aliowasitiri wakiendelea kuheshimiwa nae ameamua nao kuwavua magamba. Sasa anataka kutuambia kuwa tulichokiamini ni uongo alioutengeneza wakati ukweli wenyewe ndio huu.
Mwache Msemakweli aseme kwani waliotengeneza uongo kuwa ukweli na bado wanataka watu waendelee kuamini kwa maslahi yao watabishana na wale walioutengeneza uongo kuwa ukweli na sasa wanataka wananchi waufahamu ukweli halisi ili anagalau kuhifadhi kaheshima kao kadogo kalikobaki. Mavuno yetu watanzania tutafahamu kuwa hawa wote ni majambazi sasa wanagombana baada ya kutoafikiana namna ya kugawana kile walichopora.
Bila kugombana wenyewewe kwa wenyewe sisi hatutopata kitu, mwacheni Msemakweli aseme.