Kaimu Katibu Mkuu Nishati na Madini atangazwa

Mbona watulisha kiporo cha jana, tena jioni yote hii.
This is stale news.
 
Hii nchi kama ya akina Chupaku. Likizo ya siku kumi unateua Naibu au ndio mambo ya kuachwa kustaafu kwa heshima aliyokuwa anayatetea JK?
 
Hivi kwa nini kwenye barua HEADER english . Anuani Elglish . Ujumbe kiswahili.


Aisee nyie watu wa mawasilianowa Ikulu na idara nyingine za serikali mnatakiwa kuwa na standard. mkiamua kutumia kingereza kila kitu kitu kwe kingereza. Mkiamua kutumia kiswahili kila kitu kiwe kiswahili.

Umechukua Header header ya kingereza unaadika press release ya kiswahili. Ukichukua header ya Kiswahili ...........
 
Imetolewa na Premi Kibanga
Mwandishi wa habari wa Raisi Msaidizi
Ikulu Dar-es-salaam
22/07/2011

Bwana MASWI, kwa sasa ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
Kwa hiyo atakuwa anashikilia vyeo viwili kwa sasa, hiki cha "kuanzia leo tarehe 22 Julai, 2011," na hiki cha "kwa sasa ni Naibu Katiku Mkuu, ofisi ya waziri Mkuu..." Au?
 
Hivi Ikulu haina Letter head za Kiswahili jamani?

Yaani hii nchi hata wasomi wetu wanatuangusha sana! Inakuwaje unatumia Letter head ya Kiingereza unaandika Kiswahili? Kwa nini asingetafuta ya Kiswahili ili kwenda sawa na hiyo taarifa? Huyu naye ni zumbukuku!!

Imenikera sana kuona imetumika ya Kiingereza halafu unakuta Kiswahili! Ingependeza kama hii taarifa angeitoa kwa kutumia letter head ya Kiswahili bwana! Hawajafundishwa mambo ya kiofisi nini hawa waandishi makanjanja hawa?
 
HIvi jamani hii nchi ikoje Ina maana jairo mpaka sasa hajitwa hata kuhojiwa na Polisi au Taukuru.

Au na makatibu wakuu wana kinga kama wabuge wawapo bungeni kuhojiwa mpaka kibali cha ikulu?.



Maswi Maswi Maswi. mhhh huyu jamaa kuna mtu anamjua kanipa dondooo kuwa kapita foregn affairs, Kapita Wizara fedha na kafanya kazi morogoro kama mkuu wa hazina ndogo .Ana taaluma na mambo ya kihasibu.

Jamaa anasema ni mchapa kazi na anaweza kudeliver zaidi kama nchi isingekuwa chini ya Magamba. katika kizazi cha maktibu wakuu vijana wenye mawazo chanya nadhani anaweza kuhesabiwa. Jamaa anasema hajui sasa kama hajambukizwa gonjwa sugu la CCM ambalo ni UFISADI mana ni siku nyingi sana
Uko sahihi. Jamaa ni mchapakazi , na utendaji wake si wa kubahatisha
 
Kweli magamba nouma. Hapo wanatafuta jinsi ya kumtoa kafara jairo, ishue hii lazima inabaraka zote za top management (waziri na naibu wake).
 
Namfahamu vizuri ndugu Maswi ni mchapakazi mzuri sana kwa kipindi kifupi alichokaa pale TAMISEMI amerudisha nidhamu kidogo kwa Wahasibu wa Serikali za mitaa. Japo Ma DT wengi watafanya sherehe kwa kuhama kwake. Alikuwa Kamishna wa bajeti pale Hazina kipindi cha miaka minne au mitano hv iliyopita.
Binafsi ninamwani.
 
Tumpe pole,pale anatakiwa mtuawe engineer ndio anapaweza

Acha uongo wewe. basic Ladership na management priciple ni zile zile. Uwe engineer ,uwe, lwayer uwe philopher uwe uwe mhasibu au mchumi au Mwanatakwimu huwezi shindwa kuongoza. Ukfuata maadili.
 
hii nchi kama viongozi wote ni walevi au kama sio walevi basi wakati wanatungiwa mimba wazazi wao walikuwa wamelewa. mbona mambo mengi hayaendi kvizuri kila siku ni mchanganyiko tu. haiingii akili mtu uliye mteua amefanya kosa unampa likizo ya malipo it is shem
 
Kweli magamba nouma. Hapo wanatafuta jinsi ya kumtoa kafara jairo, ishue hii lazima inabaraka zote za top management (waziri na naibu wake).
Inawezekana mlikuwa bado hamjainyaka hii,kuwa huyo top wa hiyo wizara, ni daladala ambayo kila siku ilikuwa inapeleka hesabu.lakini nashukuru huyo mpelekewa hesabu baada ya kushitukiwa keshatangulia kujivua gamba kabla mambo hayaja haribika sana. Na hivi sasa yupo ng'ambo anasikilizia.
 
Jamaa tunafahamiana alikuwa mpiganaji!! Sijui kwa sasa, alikuwa makamu raisi wa Daruso enzi hizo tupo hapo! 90's alikuwa kifaaa! cjui sasa manaake watu hubadirika!
 
Maswi si magwanda ila likuwa NCCR mageuzi na ndiyekundi la Mrema walikuja kwenye vyama na kazi maalumu .Yeye ni mtu wa system hawezi kusema sana .Jairo yuko kwenye system hapo madini aliletwa tu imekua soo hawana la kumfanya .Kama huamini ngojeeni mtaona .So Maswi ndiyo huyo ama Msc ya nini muulizeni .Namjua mno mno hana maamuzi na kujipndekeza sana .Ni kijana mdogo tu ila tu ndiyo mambo yake hayo ni opportunist .
 
Back
Top Bottom