Kagera War: Improper Post War Retreat; Turmoil and Unrest in Tarime, Mara region and other areas

Kulya

JF-Expert Member
Sep 24, 2011
368
150
Habari za Asubuhi wanaJF!

Kumekuwepo na umilikaji wa silaha za kivita, ambazo ni hatari na raia yoyote hapaswi kumiliki. Silaha hizo hutumika kwa ujambazi, katika mapori kadhaa yaliyo maeneo ya kanda ya ziwa na mikoa ya jirani. Silaha hizo zinatumika pia kwa ujangili na wizi wa mifugo katika maeneo ya hifadhi za taifa na kwa wafugagi. Aidha, silaha hizo pia zimethibitika kutumika katika vita vya wenyewe kwa wenyewe katika nchi za Rwanda, Burundi na Congo.

Baba yangu ni mmoja ya watanzania waliopigana vita vya Kagera. Jana nilipata wasaa mzuri wa kuzungumza naye kuhusiana na vita vya Kagera. Pamoja na mambo mengine yahusuyo vita hivyo, naomba kuwasilisha hiki kipengele kidogo, "Improper Retreat of our Armies After the War"

Baada ya vita vya Kagera kuisha, kulikuwa na matukio mengi sana ya uporaji yaliyofanywa na wanajeshi wetu, matukio haya yalienda sambamba na kuuwana kwaajili ya kugombea vitu vilivyoachwa na waganda, kama redio, TV, pikipiki, magari na vitu vingine walivyoona ni vya thamani.

Pamoja na sababu nyingine, kama furaha ya ushindi, Vitendo hivi vilipelekea amirijeshi mkuu, Mwl. J.K Nyerere kuamuru majeshi yarudishwe nyumbani haraka sana.

Retreat haikufanywa kwa utaratibu unaotakiwa, kwa kawaida ingewalazimu kukaa huko Uganda hata angalau kwa kipindi cha miaka miwili.

Kutokana na kutofanywa vizuri kwa retreat, hapo ndipo wenzetu wakurya walipopata mwanya wa kujitwalia silaha kali na za kivita kwa idadi waliyoweza kuchukua. Katika kuhakikisha hili linafanikiwa, walitumia mbinu kama kuchonga majeneza na kukata vitako vya bunduki ili ziweze kuingia nyingi ndani ya jeneza na kuonekana kama wamebeba maiti, na kwasababu walikuwa wanatoka vitani, hawakuruhusu wakaguzi waangalie majeneza hayo.

Mbinu nyingine iliyotumika ni kuvaa vyeo vya ngazi ya juu, kama Kanari, meja, Captain na kupitisha mizigo bila kukaguliwa kwa kigezo cha cheo.

Pia jina la Msuguli, mkuu wa majeshi wakati huo na aliyeongoza vita hivyo, lilitumiwa vizuri kupitisha silaha hizo.

Hali ilivyo sasa. Kwa uchache tu, wilaya ya tarime eneo la Nyamongo ulipo mgodi wa ABG. Katika eneo hilo karibu kila mwanaume wa kikurya anamiliki silaha, kuna mahandaki ya kutosha tu yaliyojaa silaha kali za kivita kama sub-machine gun, machine gun na nyinginezo nyingi. Silaha hizi zimetumika sana na majambazi ambao ni matajiri sana wa kanda hii, wanaomiliki viwanda na makampuni makubwa ya usafirishaji abiria na mizigo.

Silaha hizo zinapelekea maeneo hayo yashindwe kutawalika kwa utawala wa sheria. Hivi karibuni kumeibuka vita, sijui kama watanzania wenzangu mmesikia hiyo!? Ni vita kali sana kati ya wananchi na vyombo vya dola, ulinzi na usalama, issue ni mgodi wa north mara.

Yote haya, pamoja na sababu nyingine, ni matokeo ya "POST WAR IMPROPER RETREAT"

Selikari, tafadhali ufanyike msako wa hali ya juu maeneo hayo, silaha zote zichukuliwe toka mikononi mwa hawa jamaa, hali ni tete sana! Ujambazi ni mkubwa sana na mauaji ni mengi sana ila watanzania hawapati habari hizi.

Naomba kuwasilisha.
 
Asantye kwa Taarifa ila sijui kama wamesikia waungwana
.
Nimesoma na nataka niongeze kidogo. Ni vigumu sana kuishi kwa amani ikiwa kama majirani zako wapo kwenye vita. hii inamaanishaya kwamba ni vigumu kwa nchi kama tanzania kuishi kwa amani ikiwa eneo lamaziwa makuu si shwari, ni rahisi sana, na ndivyo ilivyo, silaha kutoka DRC, Rwanda na Burundi kutumika katika matukio ya kihalifu hapa Tanzania.
Mwaka 2008 nilikuwa iliyokuwa wilaya ya Mpanda, mkoani Rukwa kwa shughuli za kiserekali. Nilipata kuongea na wakazi, ikiumbukwe zaidi ya 75% ya wakazi ni wakimbizi kutoka Rwanda na Burundi, na kujua ya kwamba takribani kila mtu anamiliki silaha na kutembea na silaha ni jambo la kawaida kabisa, mgahawa niliokuwa napata chakula (Tanganyika Cafe) baadhi ya wateja walikuwa wanaweka silaha meani huku wanakula. Wakazi wa maeneo hayo walikuwa hawaamini bunduki kwa kuiona bali huamini baada ya kupigwa hewani au kulenga mtu. Walinda usalama wznapata changamoto kubwa sana kwa kuwa wanalinda majambazi yaliyotukuka.
Hii inanifanya niamini ya kwamba usalama wa Afrika Mashariki upo mashakani ikiwa kama Somalia, Eritrea n.k hapatakuwa na usalama wa kutosha.
 
.
Nimesoma na nataka niongeze kidogo. Ni vigumu sana kuishi kwa amani ikiwa kama majirani zako wapo kwenye vita. hii inamaanishaya kwamba ni vigumu kwa nchi kama tanzania kuishi kwa amani ikiwa eneo lamaziwa makuu si shwari, ni rahisi sana, na ndivyo ilivyo, silaha kutoka DRC, Rwanda na Burundi kutumika katika matukio ya kihalifu hapa Tanzania.
Mwaka 2008 nilikuwa iliyokuwa wilaya ya Mpanda, mkoani Rukwa kwa shughuli za kiserekali. Nilipata kuongea na wakazi, ikiumbukwe zaidi ya 75% ya wakazi ni wakimbizi kutoka Rwanda na Burundi, na kujua ya kwamba takribani kila mtu anamiliki silaha na kutembea na silaha ni jambo la kawaida kabisa, mgahawa niliokuwa napata chakula (Tanganyika Cafe) baadhi ya wateja walikuwa wanaweka silaha meani huku wanakula. Wakazi wa maeneo hayo walikuwa hawaamini bunduki kwa kuiona bali huamini baada ya kupigwa hewani au kulenga mtu. Walinda usalama wznapata changamoto kubwa sana kwa kuwa wanalinda majambazi yaliyotukuka.
Hii inanifanya niamini ya kwamba usalama wa Afrika Mashariki upo mashakani ikiwa kama Somalia, Eritrea n.k hapatakuwa na usalama wa kutosha.

hii post yako imejaa uzushi, uongo na uchochezi na uchonganishi: mimi nimeishi na kufanya kazi MPANDA kama ofisa wa serikali, sijaona hao unaowaita 75% ya wakaaji wa mpanda wakitembea na siraha kama unavyodai, ukumbuke kuwa active population yao hao wakimbizi/wahamiaji wamezaliwa hapohapo mpanda na wengi hata vita ya kupigana kwa fimbo hawaijui. Acha uongo na chuki kwa watu wasio na hatia. Nakukumbusha kuwa in the past, aliyekuwa mkuu wa kambi ya Katumba MR MHAGAMA (kwasasa ni marehemu), aliwahi kuvamiwa na majambazi wenye silaha na akaumizwa vibaha, sympathizers walikuwa wakitaja kuwa ni hao wakimbizi ndio wamemvamia, yeye aliwahakikishia kuwa waliomvamia sio hao anaowasimamia bali ni waswahili kutoka sehemu nyingine. Usitumie JF kuendeleza propaganda za kupotosha jamii.
 
Silaha tangu mwaka 1977 takribani miaka 35 mpaka sasa, unasema zipo mpaka leo. Hakuna! Silahi zinatoroshwa kutoka kambi za jeshi jirani na mkoa wa mara ama ndani ya mkoa huo kupitia askari wenye asili ya sehemu hiyo. Kambi kama ya pale Kyabakare na zinginezo.
 
Silaha tangu mwaka 1977 takribani miaka 35 mpaka sasa, unasema zipo mpaka leo. Hakuna! Silahi zinatoroshwa kutoka kambi za jeshi jirani na mkoa wa mara ama ndani ya mkoa huo kupitia askari wenye asili ya sehemu hiyo. Kambi kama ya pale Kyabakare na zinginezo.

Huyu bwana anataka kueleza baada ya miaka zaidi ya 30 tangu vita iishe hadi leo hao Wakurya hawajaishiwa risasi au kuna namna nyingine wanapata silaha? Nakumbu wengi wa waliotorosha silaha baada ya vita walishughulikiwa na Sungusungu miaka ya kati '80 enzi za Sokoine.

Mie naona huu ujambawazi unaosumbua watu siku za karibuni unatokana na vita zinazoendelea kwenye nchi jirani na kufanya upatikanaji wa silaha kuwa rahisi.
 
Ndugu Kulya:

Niliwahi kuishi Tarime kwa muda fulani. Na ni kweli kulikuwa na hizo stori kuwa wanajeshi fulani walirudi na bunduki kutoka kwenye vita. Lakini tusisingizie vita vya Kagera kwa matukio ya sasa. Kwa sababu zifuatazo:

Bunduki haina mafanikio yoyote bila risasi. Vita vya Kagera viliisha 1979. Inawezekana walirudi na bunduki lakini hizo risasi za kutumia kwa zaidi ya miaka 30 wanazitoa wapi? Ukipata jibu zinapotoka risasi basi unapata jibu wapi bunduki zinatoka.

Pili ujambazi mkubwa unaofanyika Tarime unahusisha makundi wezi wa mifugo na majangiri yaliopo Tanzania, Kenya na Somalia. Hivyo silaha zinazotumika kwa ujambazi huko Tarime kwa sasa sio lazima zitoke kwenye vita vya Kagera, Rwanda, Burundi au DRC. Zinaweza kutoka Somalia.

Mifugo inaibiwa Tanzania inakwenda mpaka Somalia kupitia Kenya. Na kutoka Somalia inapelekwa mpaka Yemen. Na bidhaa zinazorudi ni pamoja na silaha.

Zaidi ya hapo, maofisa wa wizara ya ulinzi wa Tanzania wanahusika na uingizaji wa silaha. Kwa kutumia jina la wizara wanaagiza silaha ambazo zinapitia bandari ya DSM. Lakini zikitoka bandarini hazipelekwi kwenye makambi ya jeshi. Zinaenda kwa majambazi na makundi yanaopigana vita dhidi ya serikali zao.

Kwa kumalizia tu, baada ya kuvunjika kwa ukomunisti, uuzaji wa silaha zinazotoka nchi za mashariki zipo mikononi mwa watu binafsi. Hivyo ni pesa yako tu itakayokufanya kupata silaha.
 
Silaha tangu mwaka 1977 takribani miaka 35 mpaka sasa, unasema zipo mpaka leo. Hakuna! Silahi zinatoroshwa kutoka kambi za jeshi jirani na mkoa wa mara ama ndani ya mkoa huo kupitia askari wenye asili ya sehemu hiyo. Kambi kama ya pale Kyabakare na zinginezo.
Mkuu, silaha za post war bado zipo! Tena nyingi tu! Ila risasi ndio another issue, na sijazungumza kama hizo risasi za post war bado zipo! Hapo sasa kuna utashi mwingine unatumika kufanikisha kupatikana kwa risasi. Ila for the case of post war weapons, they are still plenty in stock and are yet to expire!
 
Ndugu Kulya:

Niliwahi kuishi Tarime kwa muda fulani. Na ni kweli kulikuwa na hizo stori kuwa wanajeshi fulani walirudi na bunduki kutoka kwenye vita. Lakini tusisingizie vita vya Kagera kwa matukio ya sasa. Kwa sababu zifuatazo:

Bunduki haina mafanikio yoyote bila risasi. Vita vya Kagera viliisha 1979. Inawezekana walirudi na bunduki lakini hizo risasi za kutumia kwa zaidi ya miaka 30 wanazitoa wapi? Ukipata jibu zinapotoka risasi basi unapata jibu wapi bunduki zinatoka.

Pili ujambazi mkubwa unaofanyika Tarime unahusisha makundi wezi wa mifugo na majangiri yaliopo Tanzania, Kenya na Somalia. Hivyo silaha zinazotumika kwa ujambazi huko Tarime kwa sasa sio lazima zitoke kwenye vita vya Kagera, Rwanda, Burundi au DRC. Zinaweza kutoka Somalia.

Mifugo inaibiwa Tanzania inakwenda mpaka Somalia kupitia Kenya. Na kutoka Somalia inapelekwa mpaka Yemen. Na bidhaa zinazorudi ni pamoja na silaha.

Zaidi ya hapo, maofisa wa wizara ya ulinzi wa Tanzania wanahusika na uingizaji wa silaha. Kwa kutumia jina la wizara wanaagiza silaha ambazo zinapitia bandari ya DSM. Lakini zikitoka bandarini hazipelekwi kwenye makambi ya jeshi. Zinaenda kwa majambazi na makundi yanaopigana vita dhidi ya serikali zao.

Kwa kumalizia tu, baada ya kuvunjika kwa ukomunisti, uuzaji wa silaha zinazotoka nchi za mashariki zipo mikononi mwa watu binafsi. Hivyo ni pesa yako tu itakayokufanya kupata silaha.

Ahsante mkuu, ila stock iliyoko Tarime imetoa mchango mkubwa sana kwa civil wars and insurgency zinazoendelea hapa eneo la maziwa makuu. Kuna tafiti zisizo rasmi, naomba nini-rely kwazo ila nitoe to taarifa; kutokana na JWTZ kustaafisha maafisa wake wapiganaji wa vyeo vya Captain, Luten, Officer cardet, na wengine wa vyeo vya chini, wastaafu hawa ambao hustaafu katika 47 years, wamekuwa wakitumika kama military consultants kwa insurgents in Congo, Uganda hadi huko central africa!

Sasa, hawa jamaa, mathalani kama wa Tarime, stock ya silaha walikuwa nayo ya kutosha, na sasa wamepata vibarua vya kuwa watshauri waelekezi wa majeshi yasiyo rasmi....
 
Back
Top Bottom