Kafulila na Zitto wanaivuruga NCCR - Moses Machali

Status
Not open for further replies.
.......dogo (zito) simkubali kabisa siku hizi kwa sababu sio yeye yule tunayemfahamu, siku hizi ama anatumika au kutumikia kitu/watu
Gazeti la mwanahalisi lina habari nzito tena za kushtusha.

Mbunge wa Kasulu mjini Moses Machali amemshutumu vikali David Kafulila kwamba anatumiwa na Naibu Katibu mkuu wa Chadema Zitto Kabwe kukivuruga chama hicho.

Mbunge huyo wa Kasulu anadai lengo kubwa la Kafulila ni kumwondoa mwenyekiti wa chama hicho James Mbatia ili yeye awe mwenyekiti.

Pili Machali amedai kwamba baada ya Kafulila kuwa mwenyekiti atamkaribisha Naibu Katibu mkuu wa Chadema Zitto Kabwe ili awe mgombea Urais kupitia NCCR.

Moses machali ameendelea kudai kuwa baada ya mpango huo kukamilika watatumia mbinu mbalimbali kuivuruga Chadema kwa kuhama na kundi kubwa la wanachama wake.

Mbunge huyo ameendelea kudai kuwa kamwe hatakubali mbinu hiyo kwani Zitto na Kafulila wanatumika kuua upinzani.

Alipoulizwa kwanini watake kumuondoa Mbatia kwanza amesema hiyo ni kutokana na sababu kwamba kamwe Mbatia hatamkubalia Zitto kugombea urais kupitia NCCR.

Source: MwanaHalisi
 
Mbatia haonekani kama mwanasiasa bali mganga njaa tu, hivyo akiondolewa kwa maslahi ya growth ya chama sioni tatizo hata kidogo. Na hata kama Zitto anataka kugombea Urais sioni tatizo pia. Tatizo ni wale wenye mawazo mgando ambao hawaijui demokrasia vizuri bali wanaendekeza ushabiki wa siasa tu.
 
Nilishasema na nitaendelea kusema ndoto ya ZITO ni kuongoza nchi akiwa na umri wa miaka 39 kama alivyopata kuwa Mwl JK Nyerere. Sasa anaona hawezi kupata opportunity hiyo akiwa CDM hivyo anajaribu kutafuta njia mbadala kupitia NCCR.
Zito hiyo nightmare dream unayoota haitakaa itokee hata ukienda CCM.
 
Moja, sina mpango wowote wa kuhama CHADEMA. Kila siku nasema nimekuwa mwanachama wa chama kimoja tu cha siasa maisha yangu yote, nimekuwa mwanachama wa CHADEMA toka nikiwa na umri wa miaka 16 na namwomba Mungu kila siku nife nikiwa ndani ya chama hiki. Najua kuna watu wanapenda sana nitoke CHADEMA kwa maslahi yao ya kisiasa wakiniona mimi ni tishio kwao. Napenda kuwaambia nimetumia nguvu nyingi sana kujenga chama hiki na sitahama. Waache kabisa kunizushia na kunijengea chuki mbele ya umma.

Pili, sihusikikwa lolote lile na yanayoendelea ndani ya NCCR na wala sina interest ya kuyajua. Mbunge wa Kasulu mjini ambaye alikuwa mwanachadema na kushinda Ubunge kwa sababu ya kutumia jina langu huko kwao Kasulu anaropoka (kama kweli kasema maneno hayo) na nitakapotoka Hospitali nitamtaka anithbitishie anayoyasema. Vijana wanapojiingiza kwenye siasa za uwongo kama wazee wao ni hatari sana kwa nchi. Sihitaji kwenda NCCR ili kugombea Urais kwani chama changu ni kikubwa zaidi na kitanipa Urais kwa urahisi kuliko NCCR ambacho ni chama kisicho na rekodi yeyote ya kupigania maslahi ya nchi hata wakati kilipokuwa chama kikuu cha upinzani nchini. Katiba hainiruhusu kugombea Urais mwaka 2015 na hata kama ikibadilishwa na kuniruhusu kugombea kwangu kutategemea sana mwafaka ndani ya chama changu. Anayedhani kwamba nia yangu ya kuwa Rais wa Tanzania ni ya kufa na kupona hamjui Zitto. Sifanyi siasa za kufa na kupona. Ninao uwezo wa kuwa Rais bora maana nina ajenda na ninatoka chama bora. Lakini pia nipo tayari kufanya kazi yeyote ile ambayo chama changu kitanipa.

Zittophobics wanaishi kwa siasa za kumwaza Zitto na wamo kwenye vyama vyote vya siasa hapa nchini. Ninafanya kazi zangu za Ubunge kwa ufanisi na mafanikio makubwa sana, ninafanya kazi zangu za Uenyekiti wa Kamati ya Mashirika ya Umma kwa umakini mkubwa na ninafanya kazi zangu za Uwaziri Kivuli wa fedha katika hali ya kuridhisha sana. Maadui zangu wa kisiasa wanatamani nianguke. Kwa uwezo wa Mungu sitaanguka.

Tatu, Gazeti la Mwanahalisi limekuwa ni gazeti linalonisakama sana kila kukicha lina ajenda yake. Gazeti ambalo limepoteza mvuto wake kwa jamii halinishughulishi. Hata juzi Mzee Samweli Sitta amelishutumu kwa kununuliwa na mafisadi na kutumiwa. Niseme nini zaidi kuhusu gazeti hili linaloongozwa na mtu ambaye hata hajamaliza darasa la saba. Mwanahalisi wanajua kwamba wakiandika habari yenye jina langu mauzo yao yanakua makubwa. Hili ni gazeti mufilisi ambalo kazi yake ni kutumiwa tu.

Nne, WanaJF mnasema hili ni jukwaa ni Great Thinkers. Great thinkers huwa hawadaki habari na kuziamini na kuanza kutoa maoni bila kwanza kupata uhakika wa habari hizo.

Nasikitika kwamba watu wenye ugonjwa wa Zittophobiasis ni wengi sana humu. Ninawashauri kwamba jitahidini muwe objective na muone upande wa pili wa shilingi.

Habari hii ya Mwanahalisi ni habari ya kijinga sana kujaribu tu kunihusisha na vurugu za chama ambacho mimi si mwanachama wake. Kafulila na mimi ni marafiki na ni wabunge wa Kigoma. Lakini Kafulila na mimi hatuongei mambo ya vyama vyetu hata kidogo na yeye anajua kwamba sina interest na NCCR Mageuzi.

WanaJF msicheze ngoma isiyo yenu.

Good! Ndio maana ninasema Chadema ni chama cha watu makini.Kujitokeza mara moja kujibu hoja hii kunakupa credit kubwa.

Endelea kupigania Chadema na hakika Mungu akipenda baada ya zama za Slaa huenda ukawa wewe.

Kila la kheri.
 
CDM ni zaidi ya K.Zitto chijani,ila nabaki na swali kwa machali anaposema yuko tayari kumkaribisha Zitto ili 2015 agombee urais alafu hapohapo anawataja Kafulila na Zitto kuvihujumu vyama vya upinzani ana maanisha nini?kwamba sasa kama ndivyo NCCR itapona kwa Zitto akiingia kwao
 
Kama vipi, Mbatia aitishe mkutano na kma mwenyekiti atoe hoja ya kuwatimua uanachama Kafulila na Mkosamali ili na ubunge uwatoke turudi kwa uchaguzi-Km Mrema alivyofanya. Hatari hapa ni NCCR kuyaretain majimbo hayo wakiyatoa sadaka kwa kuwafukuza uanachama! Tafakari
 
Moja, sina mpango wowote wa kuhama CHADEMA. Kila siku nasema nimekuwa mwanachama wa chama kimoja tu cha siasa maisha yangu yote, nimekuwa mwanachama wa CHADEMA toka nikiwa na umri wa miaka 16 na namwomba Mungu kila siku nife nikiwa ndani ya chama hiki. Najua kuna watu wanapenda sana nitoke CHADEMA kwa maslahi yao ya kisiasa wakiniona mimi ni tishio kwao. Napenda kuwaambia nimetumia nguvu nyingi sana kujenga chama hiki na sitahama. Waache kabisa kunizushia na kunijengea chuki mbele ya umma.

Pili, sihusikikwa lolote lile na yanayoendelea ndani ya NCCR na wala sina interest ya kuyajua. Mbunge wa Kasulu mjini ambaye alikuwa mwanachadema na kushinda Ubunge kwa sababu ya kutumia jina langu huko kwao Kasulu anaropoka (kama kweli kasema maneno hayo) na nitakapotoka Hospitali nitamtaka anithbitishie anayoyasema. Vijana wanapojiingiza kwenye siasa za uwongo kama wazee wao ni hatari sana kwa nchi. Sihitaji kwenda NCCR ili kugombea Urais kwani chama changu ni kikubwa zaidi na kitanipa Urais kwa urahisi kuliko NCCR ambacho ni chama kisicho na rekodi yeyote ya kupigania maslahi ya nchi hata wakati kilipokuwa chama kikuu cha upinzani nchini. Katiba hainiruhusu kugombea Urais mwaka 2015 na hata kama ikibadilishwa na kuniruhusu kugombea kwangu kutategemea sana mwafaka ndani ya chama changu. Anayedhani kwamba nia yangu ya kuwa Rais wa Tanzania ni ya kufa na kupona hamjui Zitto. Sifanyi siasa za kufa na kupona. Ninao uwezo wa kuwa Rais bora maana nina ajenda na ninatoka chama bora. Lakini pia nipo tayari kufanya kazi yeyote ile ambayo chama changu kitanipa.

Zittophobics wanaishi kwa siasa za kumwaza Zitto na wamo kwenye vyama vyote vya siasa hapa nchini. Ninafanya kazi zangu za Ubunge kwa ufanisi na mafanikio makubwa sana, ninafanya kazi zangu za Uenyekiti wa Kamati ya Mashirika ya Umma kwa umakini mkubwa na ninafanya kazi zangu za Uwaziri Kivuli wa fedha katika hali ya kuridhisha sana. Maadui zangu wa kisiasa wanatamani nianguke. Kwa uwezo wa Mungu sitaanguka.

Tatu, Gazeti la Mwanahalisi limekuwa ni gazeti linalonisakama sana kila kukicha lina ajenda yake. Gazeti ambalo limepoteza mvuto wake kwa jamii halinishughulishi. Hata juzi Mzee Samweli Sitta amelishutumu kwa kununuliwa na mafisadi na kutumiwa. Niseme nini zaidi kuhusu gazeti hili linaloongozwa na mtu ambaye hata hajamaliza darasa la saba. Mwanahalisi wanajua kwamba wakiandika habari yenye jina langu mauzo yao yanakua makubwa. Hili ni gazeti mufilisi ambalo kazi yake ni kutumiwa tu.

Nne, WanaJF mnasema hili ni jukwaa ni Great Thinkers. Great thinkers huwa hawadaki habari na kuziamini na kuanza kutoa maoni bila kwanza kupata uhakika wa habari hizo.

Nasikitika kwamba watu wenye ugonjwa wa Zittophobiasis ni wengi sana humu. Ninawashauri kwamba jitahidini muwe objective na muone upande wa pili wa shilingi.

Habari hii ya Mwanahalisi ni habari ya kijinga sana kujaribu tu kunihusisha na vurugu za chama ambacho mimi si mwanachama wake. Kafulila na mimi ni marafiki na ni wabunge wa Kigoma. Lakini Kafulila na mimi hatuongei mambo ya vyama vyetu hata kidogo na yeye anajua kwamba sina interest na NCCR Mageuzi.

WanaJF msicheze ngoma isiyo yenu.
Zitto!
ugua pole
Asante kwa kujitokeza usiwe kama MTATIRO aliyejificha kuja JF igunga ikamuumbua.
Hata kama SITTA alidai Mwanahalisi limenunuliwa sii sababu ya kuyakubali madai yako.

SITTA ametutendea dhuluma kubwa kabisa watanzania kwa kuizima Dowans Bungeni.

Mwanahalisi akiandika hili SITTA anakuja juu.

Hata kama Mwandishi hajamaliza daras ala saba ametunikiwa kipaji cha kusema kweli daima.

Wametufikisha wapi wasomi wa Tanzania????mnananishe CHENGE ANDREW, BALALI,MAHALU wametutendea nini???

Agustino Mrema akiwa na DIPLOMA TU miaka ile ubora wa kazi yake hautasahaulika Tanzania
 
Na sisi watanzania tusipende kusema bila kufanya uchunguzi,tujiulize ni kwa nini asemee mwanahalisi.Na yeye anatumiwa na nani.ni mbatia au ni nani hasa.

Tangu lini Mbatia akawa mpinzani hadi ionekane anayetaka kumpindua ni mhaini asiye na nia nzuri. Ni nani ndani ya hicho chama chao alishawahi kuhoji dhamira ya mbatia hasa pale anaposimamia mstari tata wenye mwelekeo wa mahaba na CCM.

Tatizo wenyeviti wa vyama vya siasa Tanzanzania hawataki challenge wanandhani uenyekiti ni haki ya kuzaliwa.hizi hulka za do or die political mentality zinadumaza demokrasia. Baadhi ya Wenyeviti wa vyama vya siasa na hasa upinzani wana mawazo ya kijima katika kufanya siasa na imefikia hatua wanaogopa watu wanaowapa changamoto za kweli na hasa vijana.Hili ni pigo kwa demokrasia.

Sitaki kuingilia mambo ya ndani ya NCCR lakini tujiulize ina maana huko NCCR hakuna mwenye haki ya kupinga mwenyekiti au kugombea nafasi ya juu ya uongozi ndani ya chama hicho...na je ina maana Mbatia ndiye mwenye kauli ya mwisho katika kupitisha nani awe mgombea urais kupitia NCCR....

WanaJF, ukiona Mbunge anajadili watu bila kuwa na uhakika wa anachosema ujue ni dalili za watu kuwa na ombwe la fikra. Sisi tunaingia mkenge kisa kasema mtu ambaye unamkubali SANA ! ! ! Tunaacha kufikiri kwa sababu mtu unayemkubali sana kasema, tuwe makini yasije yakatukuta yale ya Kibwetere kule Uganda

mkuu ulichosema ni ukweli mtupu.Mbatia sio mpinzani wala hajawahi kua mpinzani ni CCM ya JK.
Hata alipogombea ubunge mwaka jana alikua na lengo la kugawa kura za upinzani ili Halima Mdee asipite CCM washinde.
 
Hii ameitoa wakati akijibu hoja/tuhuma za kuhusu yeye na Kafulila na kuivuruga NCCR kwa malengo yao binafsi..

"Gazeti la Mwanahalisi limekuwa ni gazeti linalonisakama sana kila kukicha lina ajenda yake. Gazeti ambalo limepoteza mvuto wake kwa jamii halinishughulishi. Hata juzi Mzee Samweli Sitta amelishutumu kwa kununuliwa na mafisadi na kutumiwa. Niseme nini zaidi kuhusu gazeti hili linaloongozwa na mtu ambaye hata hajamaliza darasa la saba. Mwanahalisi wanajua kwamba wakiandika habari yenye jina langu mauzo yao yanakua makubwa. Hili ni gazeti mufilisi ambalo kazi yake ni kutumiwa tu."

SOURCE;
JF
 
Zitto ni bora sana kuliko wanasiasa wengi na hata wachangiaji wengi sana humu JF.

Propaganda hizi naona zinatokana na wanasiasa wasiokuwa na vision na wanamuona Zitto kama threat kwa future dreamz zao ndio maana wanaamua kumpaka matope. waingereze wanasema, "You can not strengthen the weak by weakening the strong" Muacheni Zitto aendelee na kazi...akitaka kugombea tutampima na watakao jitokeza wakati huo..!!!
 
Mwakalinga, ili source iwe ni jf lazima
1. Zitto amepost jf.
2. Zitto ameongea na wewe hivyo hiyo nukuu ya Mhe. Zitto ni maneno uliyoyasikia wewe kwa masikio yako.

Vinginevyo source ni ilikotokea hiyo nukuu.
Pasco
 
Nilishasema na nitaendelea kusema ndoto ya ZITO ni kuongoza nchi akiwa na umri wa miaka 39 kama alivyopata kuwa Mwl JK Nyerere. Sasa anaona hawezi kupata opportunity hiyo akiwa CDM hivyo anajaribu kutafuta njia mbadala kupitia NCCR.
Zito hiyo nightmare dream unayoota haitakaa itokee hata ukienda CCM.

we ni nani hasa mpaka umsemee Zito? Au ndo upande wa pili wa Mwanahalisi mnaotaka kumchafua? Ume2mwa?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom