Kafulila na Hamad Rashid wametoswa?

Owosumbaku

Member
Jan 25, 2011
10
1
KAtika matokeo ya uchagizi wa wenyeviti wa kamati za bunge sijaona majina ya HAMAD RASHID na KAFULILA. Kwa kuwa ninaamini wamegombea nafasi mojawapo kati ya zile zilizowatuma kuomba bunge kuwafungisha ndoa ya LAZIMA na CHADEMA ili waziongoze, je wametoswa?

Tunaomba mtujuze wenye taarifa.
 
KAtika matokeo ya uchagizi wa wenyeviti wa kamati za bunge sijaona majina ya HAMAD RASHID na KAFULILA. Kwa kuwa ninaamini wamegombea nafasi mojawapo kati ya zile zilizowatuma kuomba bunge kuwafungisha ndoa ya LAZIMA na CHADEMA ili waziongoze, je wametoswa?

Tunaomba mtujuze wenye taarifa.

Inawezekana mkuu?
 
KAtika matokeo ya uchagizi wa wenyeviti wa kamati za bunge sijaona majina ya HAMAD RASHID na KAFULILA. Kwa kuwa ninaamini wamegombea nafasi mojawapo kati ya zile zilizowatuma kuomba bunge kuwafungisha ndoa ya LAZIMA na CHADEMA ili waziongoze, je wametoswa?

Tunaomba mtujuze wenye taarifa.

Mkuu taarifa hii unatujuza wewe, mimi nilitaraji nilipoona heading ningekuta majina ya wenyeviti wote waliochaguliwa ili tuwe kwenye position nzuri ya kuchangia, kumbe wewe unauliza swali!
 
Inawezekana mkuu?

Mkuu Masanilo, hadi dakika hii jina la KAFULILA na HAMAD halijatokea kushinda kwenye kamati yeyote. Ninaimani kuwa hoja yao jana haikuwa kwa lengo la kushika kibendera. Sasa nauliza, ina maana hata wenzao wa CCM A wamewatosa?
 
KAtika matokeo ya uchagizi wa wenyeviti wa kamati za bunge sijaona majina ya HAMAD RASHID na KAFULILA. Kwa kuwa ninaamini wamegombea nafasi mojawapo kati ya zile zilizowatuma kuomba bunge kuwafungisha ndoa ya LAZIMA na CHADEMA ili waziongoze, je wametoswa?

Tunaomba mtujuze wenye taarifa.
Walifurahia vijembe bila kujua wenzao walikuwa wakifurahia wamepitia mgongoni kwao kupitisha wanayoyataka.
 
Mkuu taarifa hii unatujuza wewe, mimi nilitaraji nilipoona heading ningekuta majina ya wenyeviti wote waliochaguliwa ili tuwe kwenye position nzuri ya kuchangia, kumbe wewe unauliza swali!

PAULSS , here are the names of the WATEULE
(i) Mwenyekiti wa kamati ya fedha na uchumi ni Abdallah Kigoda
(ii) Mwenyekiti wa kamati ya katiba ,sheria na utawala ni Pindi Chana
(iii) Mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje, ulinzi na usalama ni Edward Nyoyai Lowassa
(iv)Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii ni Magreth Sitta
(v) Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya jamii ni Jenista Mhagama
(vi)Mwenyekiti wa kamati ya ardhi, maliasili na mazingira ni ………….
(viiMwenyekiti wa kamati ya kilimo,mifugo na maji ni Prof.David Mwakyusa
(viiiMwenyekiti wa kamati ya Miundombinu ni Peter Serukamba.
(ixMwenyekiti kamati ya hesabu za za serikali za mitaa ni Augustino Mrema.
(x)Mwenyekiti wa kamati ya hesabu za mashirika ya umma ni Zitto Kabwe
(xiMwenyekiti wa kamati ya heswabu za serikali ni John Momose Cheyo.
(xMwenyekiti wa kamati ya viwanda na Biashara ni Mahamoud
(xiiMwenyekiti wa kamati ya nishati na madini ni January Makamba
 
MZAHA WA CUF KUWA 'CHAMA TAWALA' NA 'CHAMA CHA UPINZANI' KWA WAKATI MMOJA KWA KIPINDI KILE KILE NDANI YA TAIFA MOJA!!!




22.JPG

525 × 700 - David Kafulila, Kigoma Kusini. Mkutano

Ni gharama kubwa sana kwetu sisi wapigakura kuchagua baadhi ya vijana wasiokua na msimamo thabiti kwenda bungeni kutuwakilisha.

Nilimtaza huyu Ndugu Kafulila kwa uchungu mkubwa sana jinsi alivyokua anaongea bungeni kutaka kulazimisha ndoa ya kisiasa kati ya CHADEMA na CUF wakati anafahamu fika kwamba CUF ni chama tawala ndani ya mipaka yetu hii ya Tanzania kwa mujibu wa mwafaka wake na CCM.

Mtu asitfute njia ya mkato wa kutafuta CHADEMA kusaidia kusafisha uchafu wa utawal wa kisheria na kidemokrsia kama ambavyo CCM na CUF walivyojisababishia kwa MWAFAKA WA MAKAMBA kule Visiwani na sasa Mwafaka huo ulivyowaletea mikanganyiko ndani ya bunge la Muungano na hata kutishia kuvunja muungano wetu misingi ya kisheria itakapolazimika kuzingatiwa.

Kwa mtaji wa kitendo tu cha bunge letu tukufu kule Dodoma ITAKAPOSHAWISHIKA KULAZIMISHA KUBADILISHWA KWA KANUNI YA BUNGE inayozungumzia sifa na muundo wa chama rasmi cha Upinzani bungeni basi moja kwa moja tangu hapo tujue kwamba taifa letu litakua limeingia moja kwa moja KATIKA MGOGORO WA KIKATIBA ambayo matokea yake huenda yasipendeze sana kwa wengi wwetu.

Hakika mara baada ya CCM kulazimisha ndoa kati ya CUF na CHADEMA huku bara wakati wakijua kwamba kula Zanzibar ndoa ni kati ya CUF na CCM basi naona kuna uwezekano mkubwa wa WA KUZUKA KWA MISURURU YA KESI JUU YA MGOGORO WA KIKATIBA NA KUHITAJIKA KWEPO KWA MAHAKAMA YA KIKATIBA NCHINI AU WATU NA VIKUNDI VISIVYOAFIKI HIYO HALI KULAZIMIKA KWENDA MAHAKAMA YA KIMATAIFA KUTAFUTA HAKI ILI KUNUSURU MUUNGANO WETU TANZANIA.

Mhe Kafulila, ulichukua angalau muda wako kuyafikiria haya kabla ya kuanza na mazungumzo yako kule bungeni???????????? Jamani tusipende kuleta majibu rahisi sana kwa swala ngumu kama hili.

Mwafaka wa Zanzibar ulikua na nia nzuri kwa kutulete utulivu kule visiwani lakini kwa kuwa wahusika huenda walikosa ushauri mzuri kisheria na matokeo ya utekelezaji wa mwafaka wenyewe ndani ya muungano wetu hasa kwa vyama vingine ambavyo havikuhushishwa kwenye mwafaka huo ndio leo hii imetufikisha hapa.

Nakumbuka sana Mhe James Mbatia alilipigia sana kelele wakati ule akitaka vyama vyote vya upinzani vihusishwa lakini kwa bahati maya sana hakusikilizwa na CCM. Inamaana Mbatia hakumpa briefing mbunge wake Kafulila juu ya ukwel huo???

Kwa mantiki hii hata mtu akilazimisha kubadilisha kanuni za mchezo bungeni wakati timu tayari ziko uwanjani tayari kucheza, jamba ambalo kwanza si la kawaida na ni ukiukwaji mkubwa wa misingi ya demokrasia ya vyama vingi ndani ya himaya ya nchi za jumuiya ya madola, pamoja na yote CUF bado haingii kisheria ndani ya kambi ya upinzani mpaka kwanza ama:

(1) CUF kijivue kutoka ndani ya mwafaka na CCM kule visiwani.

(2) au Serikali itangaze wazi kwamba kwa mwafaka wa CCM na CUF basi tayari walishavunja Muungano wetu na Zanzibar ili Watanzania tujue kabisaa kwamba kumbe mpaka sasa hatuna muungano ndipo CUF ipate kukubalika Bara kama chama cha upinzani bila kutupa jicho kwamba kule Visiwani chama hiki kimekaeje bungeni huko.

(3) Na kama hoja namba mbili ndio ukweli wa mambo ulivyo nchini mwetu basi kabla CUF haijavuka sakafu la bunge letu la muungano kule Dodoma kuja upande wa upinzani, kwa maana ya kwamba yanayoendelea bunge la Zanzibar sasa ionekane kana kwamba haituhusu huku Bara, basi kwanza ni sharti wabunge wote wa Zanzibar waondoke bungeni hapo bila kujali chama kilichomleta hapo bungeni.

Watanzania tuliowengi sana hatupendi hata kidogo tunu letu 'Muungano' kuvunjwa na mtu yeyote lakini mantiki hoja yenyewe inatuelekeza hivyo kwamba CUF kuingia kambi ya upinzani huku bara basi maana yake Muungano ulishavunja na wabunge wote kutoka Visiwani ni sharti waondoke bungeni Dodoma.
 
..mpinzani serious aliyepata uenyekiti ni Zitto Kabwe.

..sasa hapo ndipo unapoona ujanja wa CCM kuchagua, Cheyo na Mrema, vichwa maji wa upinzani, kuongoza kamati muhimu za bunge.
 
Ni vizuri mtoa hoja(uliyeanzisha thread hii) ungetujuza ni kamati zipi ambazo Kafulila David na Hamad Rashid Mohammed waligombea na kushindwa/kutoswa...
 
PAULSS , here are the names of the WATEULE
(i) Mwenyekiti wa kamati ya fedha na uchumi ni Abdallah Kigoda
(ii) Mwenyekiti wa kamati ya katiba ,sheria na utawala ni Pindi Chana
(iii) Mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje, ulinzi na usalama ni Edward Nyoyai Lowassa
(iv)Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii ni Magreth Sitta
(v) Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya jamii ni Jenista Mhagama
(vi)Mwenyekiti wa kamati ya ardhi, maliasili na mazingira ni ………….
(viiMwenyekiti wa kamati ya kilimo,mifugo na maji ni Prof.David Mwakyusa
(viiiMwenyekiti wa kamati ya Miundombinu ni Peter Serukamba.
(ixMwenyekiti kamati ya hesabu za za serikali za mitaa ni Augustino Mrema.
(x)Mwenyekiti wa kamati ya hesabu za mashirika ya umma ni Zitto Kabwe
(xiMwenyekiti wa kamati ya heswabu za serikali ni John Momose Cheyo.
(xMwenyekiti wa kamati ya viwanda na Biashara ni Mahamoud
(xiiMwenyekiti wa kamati ya nishati na madini ni January Makamba



Duh hivi Mh. Mrema bado yuko fit kuongoza kamati yoyote makini......mi namuona kama amedata vile...just thinking aloud.
 
Mkuu Masanilo, hadi dakika hii jina la KAFULILA na HAMAD halijatokea kushinda kwenye kamati yeyote. Ninaimani kuwa hoja yao jana haikuwa kwa lengo la kushika kibendera. Sasa nauliza, ina maana hata wenzao wa CCM A wamewatosa?

Rules of the game has probably changed.
 
Maskini hamad rashidi misuli yote ile amechemka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Kafulila nae kachemka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Sasa wanatafuta lipi lingine? Wamekwisha kabisa kabisa! Chadema itaendelea kusimamia msimamo wake na tunaipenda hio -songeni mbele.
 
Maskini hamad rashidi misuli yote ile amechemka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Kafulila nae kachemka!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Sasa wanatafuta lipi lingine? Wamekwisha kabisa kabisa! Chadema itaendelea kusimamia msimamo wake na tunaipenda hio -songeni mbele.

Kwani waligombea kwenye kamati zipi mkuu??...
 
PAULSS , here are the names of the WATEULE
(i) Mwenyekiti wa kamati ya fedha na uchumi ni Abdallah Kigoda
(ii) Mwenyekiti wa kamati ya katiba ,sheria na utawala ni Pindi Chana
(iii) Mwenyekiti wa kamati ya mambo ya nje, ulinzi na usalama ni Edward Nyoyai Lowassa
(iv)Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii ni Magreth Sitta
(v) Mwenyekiti wa kamati ya maendeleo ya jamii ni Jenista Mhagama
(vi)Mwenyekiti wa kamati ya ardhi, maliasili na mazingira ni ………….
(viiMwenyekiti wa kamati ya kilimo,mifugo na maji ni Prof.David Mwakyusa
(viiiMwenyekiti wa kamati ya Miundombinu ni Peter Serukamba.
(ixMwenyekiti kamati ya hesabu za za serikali za mitaa ni Augustino Mrema
(x)Mwenyekiti wa kamati ya hesabu za mashirika ya umma ni Zitto Kabwe
(xiMwenyekiti wa kamati ya heswabu za serikali ni John Momose Cheyo.
(xMwenyekiti wa kamati ya viwanda na Biashara ni Mahamoud
(xiiMwenyekiti wa kamati ya nishati na madini ni January Makamba

Bwahahahaaaaaa
 
Back
Top Bottom