Maskini Mkulima
Member
- Dec 27, 2011
- 27
- 38
Nimepata shida kidogo kuhusiana na suala la Kafulila lilivyoendeshwa na lilipofikia. Napata wasiwasi kwamba kuna mchezo mchafu na pengine Zitto anahusika na mchezo huo ndo maana akawa wa kwanza kutueleza humu kwamba Kafulila anaendelea kuwa mbunge. Wanasheria wajitokeze watuweke sawa kwa sababu hata maelezo ya Dr. Mvungi sijayaelewa pengine kwa sababu sikuhudhuria press conference yake nimekuwa nikipata vipiece vipiece tu vya alichokisema. Nijuavyo mimi uamuzi wa NEC ya NCCR unaheshimiwa mpaka hapo mahakama itakapoutengua kwenye kesi ya msingi iliyofunguliwa na Kafulila na kwa kuwa uamuzi huo unaamanisha kwamba hana chama tena anachokiwakilisha kwa sasa (kwa mujibu wa katiba mbovu tunayoitumia kwa sasa), then na ubunge anasimama. Isipokuwa court injuction sasa inazuia taratibu nyingine kuendelea kuanzia hapo ilipotoka, kwa maana kwamba Tume ya Uchaguzi haitatangaza uchaguzi mdogo mpaka kesi ya msingi iamriwe. Na ndicho kilichotokea kwa akina Erasto Tumbo na Danny Makanga walipofungua kesi mwaka 2001 kupinga kufukuzwa uanachama wa UDP. Na ndicho pia kilichotokea kwa madiwani wa CHADEMA waliofukuzwa uanachama na Kamati Kuu ya chama hicho. Hapakufanyika uchaguzi wala waziri hakuitaarifu tume ya uchaguzi kwamba nafasi zao ziko wazi ila waliendelea kuwa pembeni ya udiwani na ndo maana waziri alipotaka kuchakachua ili waendelee kuwa madiwani umma ulimwakia sana. Sasa hii ya Kafulila inakuwaje aendelee kuwa mbunge? Zitto na wenzako jitokezeni mtuambie kama mlimhonga Jaji ama ni nini mmefanya.
S
S