Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,770
- 59,118
Lizzy,
Kuna vitu ni vigumu sana kuvibadilisha...Wenzio tumeishi na bibi zenu hadi tunazeeka ila hatukuwahi kuwa na vitu nyie mnaita love at first sight...Mwanamume unampenda mwanamke baada ya kuwa ama vigezo vyako vimetimia au vingine umeachana navyo.
Kama huamini wewe endelea hivyo hivyo...ila ipo siku utaujua ukweli...I wish ungerudi haraka kumsimulia Babu DC!!
Babu hata mimi sio mmoja wa wanaoanguka (japo naamini ipo) kwenye hiyo dhana ya love at first sight.
Kinachonisumbua ni kwamba hicho tunachodhani mwanakaka anaweza akawa anampendea au kinamsukuma kuoa huyo dada hakitoshi kutrngeneza ndoa iliyo imara.Maana kama ni hicho tu, yani inawezekana akawa hana hisia za kimapenzi(ana mapendo nae tu) na huyo dada wa watu hiyo ndoa ya kazi gani?Sindo kesho na kesho kutwa ataebda kuridhisha hizo hisia kwingine?
Yani kama hiyo ndio hali halisi (kumpendea malezi) hana tofauti na wale wanaooa ili wapikiwe na kusafishiwa nyumba alafu baadae wanatafuta nyumba ndogo kwaajili ya mahitaji yao mengine.