RAIS Mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume amtetea Mwanawe Fatma Karume kuwa ndio mmiliki halali wa kiwanja kilichopo Mbweni eneo la Mfuuni ambacho kimeingia katika mgogoro kati ya Kanisa la Angalikan na mwanawe huyo.
Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake jana, Mbweni, Karume alisema mwanawe ana hati kamili za kiwanja hicho kutoka serikalini kwa kuwa ametimiza vigezo vyote vinavyohitajika na hivyo anastahiki kujenga kwa kuwa kiwanja hicho ni chake.
Juzi Kasisi Msaidizi wa Kanisa la Angalikan Zanzibar, Mathew Wilfred Mhagama aliongoza maombi maalumu na kumtaja Fatma Karume kuwa ameporwa kiwanja cha kanisa hilo pamoja na sehemu muhimu ya makaburi ya wazazi wao ambayo yamekuwepo kwa miongo kadhaa katika eneo hilo.
Karume alisema kwamba ni yeye aliyechukuwa juhudi za kuyatunza makaburi yaliopo eneo la Mfuuni kutokana na waumini wenyewe kuyatekeleza makaburi yao kwa muda mrefu sana.
Alisema yeye na familia yake imefanya kazi kubwa ya kulilinda na kuliokoa kanisa hilo ikiwa pamoja na kutafuta mlinzi kwa kuwa muda mrefu lilikuwa halina mlinzi na milango yake ilikuwa ikiwa wazi kwa muda wa miaka kadhaa.
Makaburi yale mlioyaona kwa muda wa miaka 20 sasa yanatunzwa na familia yetu ni mimi binafsi na familia yangu yote ndio tunaoyatizama na baadhi ya wakati hupata nafasi ya kutoa pesa kwa ajili ya kulimiwa majani na kufanyiwa usafi katika eneo lote lile la makaburi yaliopo palealisema Karume huku akiwa amekaa na binti yake pembezoni.
Awali Karume alieleza masikitiko yake kutokana na kauli zilizotolewa na viongozi hao wa dini huku akisema hawajasema ukweli na badala yake wameendekeza jazba ambazo zimewafanya waumini wao kwenda moja kwa moja katika kiwanja na kufanya fujo la kuharibu mali ya mwanawe ambaye ni mmiliki halali wa kiwanja hicho.
Karume aliwaita viongozi walioongoza misa juzi katika kanisa la Angalika liliopo Mbweni na kukusanya kundi la waumini wa dini hiyo kwamba ni viongozi waliopotoka na wasiofuata maadili na mafundisho ya kitabu kinachowaongoza.
Alisema viongozi hao wamepotoka kwa kuwa wameshindwa kufuata maadili ya dini yao inavyowaelekeza na kitendo cha kujichukulia sheria mikononi mwao cha kuvunja vunja vifaa vilivyokuwa katika eneo la ujenzi na kuharibu mali ya watu ni kosa kisheria.
Nimeshangazwa sana na hawa viongozi wa dini ni viongozi wa ajabu sana tena wamepotoka kabisa ..kwa sababu wameshindwa kufuata maadili ..naona wanakosa utu na heshima kwa wakubwa zao alisema Rais Mstaafu Karume huku akiwa amekunja uso wake na kutafuna tafuna ulimi wakena kuongeza kwamba.
Tangu enzi za baba yangu pamoja na mimi nimekuwa na uhusiano mzuri na kanisa hilo ..nimehamia hapa katika mwaka 1968 hakuna mtu yoyote katika eneo hili isipokuwa kanisa alisema Karume na kuwageukia waandishi wa habari.
Hata hivyo Rais huyo mstaafu aliwapoza waumini wa kanisa hilo la Angalikan kwa kusema kwamba ujenzi wa mwanawe huyo hautoathiri wala kubomowa makaburi yaliopo jirani ya kiwanja hicho hasa kwa kuzingatia kwamba makaburi hayo yanatunzwa na familia yake kwa miaka mingi tu.
Akiongea baada ya kumaliza baba yake binti huyo Fatma Karume alisema hana mpango wowote wa kuharibu wala kubomoa makaburi ya waumini wa wakrito na ujenzi wake utaheshimu eneo hilo muhimu la makaburi.
Mimi ndio mmiliki wa eneo hili kihalali na hati zote kamili za kisheria ninazo mimi dini yangu ya kiislamu na madhehebu yangu yananiagiza kuheshimu dini nyengine kwa hivyo sina matatizo wala nia ya kuharibu wala kubomoa makaburi wa dini nyengine kwa sababu ninaheshimu dini zote alisema Fatma Karume ambaye kitaaluma ni mwanasheria.
Fatma naye kama baba yake alishangazwa na waumini wa madhehebu hayo ya kiangalikan kutokana na kuiruhusu kampuni moja ya Kichina inayojenga hoteli karibu na eneo la makaburi ambapo udongo unaochimbwa katika ujenzi wa hoteli hiyo inayojengwa humiminwa makaburi hapo kwa kuwa uongozi wa kanisa hilo umetoa ruhusa wenyewe.
Aliulaumu uongozi wa kanisa la Anglikana kwa kuruhusu kampuni inayojenga hoteli na kuweka kifusi na udongo katika makaburi ya Wakristo na hivyo kuyaharibu makaburi hayo ambayo waumini hao wanasema kwamba makaburi yao yamechimbwa na kungolewa misalaba yao wakati uongozi ndio uliotoka kibali cha uharibifu huo.
Nimeshangazwa sana na uongozi wa kanisa hili kwa kwa kuiruhusu kampuni hiyo ya kichina kumwaga kifusi wanachokichota kule katika hoteli na kukimwaga katika eneo lile la makaburi .nimekuwa najiuliza nani anayepuuza na kudharau makaburi haya ni mimi au wao wenyewe walioruhusu hii kampuni kumwaga udongo?alihoji Fatma Karume.
Juzi kanisa la Angalikan liliitisha misa maalumu ya maombi yaliongozwa na Kasisi Msaidizi, Mathew Wilfred Mhagama wa kanisa Mkunazini Zanzibar, kumshitakia Mungu wakidai wameporwa ardhi yao na binti wa rais mastaafu na kuwataka waumini hao kutembea kwa mguu hadi kwenye kiwanja kilichopo mbweni na kushuhudia ujenzi wa jengo linalomilikiwa na Fatma Karume.
Na Salma Said
Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake jana, Mbweni, Karume alisema mwanawe ana hati kamili za kiwanja hicho kutoka serikalini kwa kuwa ametimiza vigezo vyote vinavyohitajika na hivyo anastahiki kujenga kwa kuwa kiwanja hicho ni chake.
Juzi Kasisi Msaidizi wa Kanisa la Angalikan Zanzibar, Mathew Wilfred Mhagama aliongoza maombi maalumu na kumtaja Fatma Karume kuwa ameporwa kiwanja cha kanisa hilo pamoja na sehemu muhimu ya makaburi ya wazazi wao ambayo yamekuwepo kwa miongo kadhaa katika eneo hilo.
Karume alisema kwamba ni yeye aliyechukuwa juhudi za kuyatunza makaburi yaliopo eneo la Mfuuni kutokana na waumini wenyewe kuyatekeleza makaburi yao kwa muda mrefu sana.
Alisema yeye na familia yake imefanya kazi kubwa ya kulilinda na kuliokoa kanisa hilo ikiwa pamoja na kutafuta mlinzi kwa kuwa muda mrefu lilikuwa halina mlinzi na milango yake ilikuwa ikiwa wazi kwa muda wa miaka kadhaa.
Makaburi yale mlioyaona kwa muda wa miaka 20 sasa yanatunzwa na familia yetu ni mimi binafsi na familia yangu yote ndio tunaoyatizama na baadhi ya wakati hupata nafasi ya kutoa pesa kwa ajili ya kulimiwa majani na kufanyiwa usafi katika eneo lote lile la makaburi yaliopo palealisema Karume huku akiwa amekaa na binti yake pembezoni.
Awali Karume alieleza masikitiko yake kutokana na kauli zilizotolewa na viongozi hao wa dini huku akisema hawajasema ukweli na badala yake wameendekeza jazba ambazo zimewafanya waumini wao kwenda moja kwa moja katika kiwanja na kufanya fujo la kuharibu mali ya mwanawe ambaye ni mmiliki halali wa kiwanja hicho.
Karume aliwaita viongozi walioongoza misa juzi katika kanisa la Angalika liliopo Mbweni na kukusanya kundi la waumini wa dini hiyo kwamba ni viongozi waliopotoka na wasiofuata maadili na mafundisho ya kitabu kinachowaongoza.
Alisema viongozi hao wamepotoka kwa kuwa wameshindwa kufuata maadili ya dini yao inavyowaelekeza na kitendo cha kujichukulia sheria mikononi mwao cha kuvunja vunja vifaa vilivyokuwa katika eneo la ujenzi na kuharibu mali ya watu ni kosa kisheria.
Nimeshangazwa sana na hawa viongozi wa dini ni viongozi wa ajabu sana tena wamepotoka kabisa ..kwa sababu wameshindwa kufuata maadili ..naona wanakosa utu na heshima kwa wakubwa zao alisema Rais Mstaafu Karume huku akiwa amekunja uso wake na kutafuna tafuna ulimi wakena kuongeza kwamba.
Tangu enzi za baba yangu pamoja na mimi nimekuwa na uhusiano mzuri na kanisa hilo ..nimehamia hapa katika mwaka 1968 hakuna mtu yoyote katika eneo hili isipokuwa kanisa alisema Karume na kuwageukia waandishi wa habari.
Hata hivyo Rais huyo mstaafu aliwapoza waumini wa kanisa hilo la Angalikan kwa kusema kwamba ujenzi wa mwanawe huyo hautoathiri wala kubomowa makaburi yaliopo jirani ya kiwanja hicho hasa kwa kuzingatia kwamba makaburi hayo yanatunzwa na familia yake kwa miaka mingi tu.
Akiongea baada ya kumaliza baba yake binti huyo Fatma Karume alisema hana mpango wowote wa kuharibu wala kubomoa makaburi ya waumini wa wakrito na ujenzi wake utaheshimu eneo hilo muhimu la makaburi.
Mimi ndio mmiliki wa eneo hili kihalali na hati zote kamili za kisheria ninazo mimi dini yangu ya kiislamu na madhehebu yangu yananiagiza kuheshimu dini nyengine kwa hivyo sina matatizo wala nia ya kuharibu wala kubomoa makaburi wa dini nyengine kwa sababu ninaheshimu dini zote alisema Fatma Karume ambaye kitaaluma ni mwanasheria.
Fatma naye kama baba yake alishangazwa na waumini wa madhehebu hayo ya kiangalikan kutokana na kuiruhusu kampuni moja ya Kichina inayojenga hoteli karibu na eneo la makaburi ambapo udongo unaochimbwa katika ujenzi wa hoteli hiyo inayojengwa humiminwa makaburi hapo kwa kuwa uongozi wa kanisa hilo umetoa ruhusa wenyewe.
Aliulaumu uongozi wa kanisa la Anglikana kwa kuruhusu kampuni inayojenga hoteli na kuweka kifusi na udongo katika makaburi ya Wakristo na hivyo kuyaharibu makaburi hayo ambayo waumini hao wanasema kwamba makaburi yao yamechimbwa na kungolewa misalaba yao wakati uongozi ndio uliotoka kibali cha uharibifu huo.
Nimeshangazwa sana na uongozi wa kanisa hili kwa kwa kuiruhusu kampuni hiyo ya kichina kumwaga kifusi wanachokichota kule katika hoteli na kukimwaga katika eneo lile la makaburi .nimekuwa najiuliza nani anayepuuza na kudharau makaburi haya ni mimi au wao wenyewe walioruhusu hii kampuni kumwaga udongo?alihoji Fatma Karume.
Juzi kanisa la Angalikan liliitisha misa maalumu ya maombi yaliongozwa na Kasisi Msaidizi, Mathew Wilfred Mhagama wa kanisa Mkunazini Zanzibar, kumshitakia Mungu wakidai wameporwa ardhi yao na binti wa rais mastaafu na kuwataka waumini hao kutembea kwa mguu hadi kwenye kiwanja kilichopo mbweni na kushuhudia ujenzi wa jengo linalomilikiwa na Fatma Karume.
Na Salma Said