Pendekezo lako ni zuri. Ila mimi nilikuwa nadhani kuna listi ndeeefu ya viongozi ambao wanastahili kuhojiwa kwanza kabla hatujakimbilia kumhoji Mheshimiwa Mbowe. Mimi nilikuwa nafikiri wahojiwe kwanza;
1. Benjamin Mkapa - Kwa kuingia dili chafu (kiwira etc) akiwa ikulu, kinyume na maadili ya uongozi.
2. Mkurugenzi wa TAKUKURU - Kwa kukiri hadharani kwamba RICHMOND ni safi, kitu ambacho baadaye kiligundulika kuwa si kweli.
3. JK - (a) Kwa kutotekeleza ahadi yake ya "Maisha Bora kwa wote" aliyoitoa mwaka 2005
( b) Kwa kutoifanyia kazi mpaka leo hii listi ya wauza unga aliyopewa na Amina Chifupa (RIP) pamoja na mikwara yote ya kutaka watu wampelekee majina.
(c) Kwa kutotumia executive power aliyonayo kumweka kifungoni Rais aliyemtangulia licha ya kuwa na vielelezo vyote kwamba alikiuka maadili ya uongozi akiwa Rais wa Jamhuri ya wadanganyika
( d ) Kwa kutowachukulia hatua watendaji wakuu wa serikali (wengine bado wamo madarakani) walioshirikiana na Balali (RIP) katika deals chafu za kuwaongezea wadanganyika umaskini
(e) .............
4. etc etc ...
Kuna wengi sana wa kuwahoji kabla hatujamfikia Mbowe. Kuna maswali mengi sana ambayo wadanganyika tunajiuliza na hatupati majibu yake ambayo niliowataja hapo juu na wengine niliowasahau wangeweza kutupatia kabla hatujamfikiria Mheshimiwa Mbowe.
Wakishahojiwa hao kwanza then ndio ulete rasmi pendekezo la kutaka kumhoji Mbowe. Ama wewe unaonaje ndugu Kada?
Mtetezi wa ufisadi huyo unadhani atakujibu hapa, umesoma chochote siku za karibuni akipondea wizi wa ccm na ufisadi wao? Huyu kuanzia atangaze rasmi kuwa upande wa mafisadi amekuwa hakemei chochote kuhusu ufisadi.
Mimi nawashauri ccm wamfungulie kesi Mbowe ili yote yaliyo sirini yaje wazi na ijulikane kama kweli huyo Ballali amekufa au la.