Golden city
Member
- Jul 7, 2014
- 9
- 3
Kutokana na nyuzi nyingi kuja humu jukwaani kwa minajili ya kuomba kubadilishana vituo vya kazi kwa kada ya Afya, ipo haja ya kuwa na uzi mmoja utakaokusanya, kujadili na kujibu maombi yote ya aina hii.
Uwe Mganga Mwandamizi, Mganga wa Kawaida, Afisa Tabibu, Muuguzi, Mkunga au Muhudumu wa Afya karibu kwenye uzi huu ukutane na wenzako wenye mahitaji kama ya kwako.
Kwenye andiko lako ni vema ukasema ulipo, mkoa na wilaya ambako ungependa kwenda na mawasiliano yako. Tunashauri mtumie barua pepe kuliko nambari za simu kwa usalama zaidi.
ZIADA: Kama ilivyoripotiwa kwenye uzi wa Walimu Wanaotaka Kubadilishana Vituo, hata humu kunaweza kuwa na hatari ya matapeli ambao watatumia fursa kujipatia fedha, kukudhuru na wakati fulani kutaka kunufaika kingono (hasa kwa wanawake). IWENI MAKINI!
Uwe Mganga Mwandamizi, Mganga wa Kawaida, Afisa Tabibu, Muuguzi, Mkunga au Muhudumu wa Afya karibu kwenye uzi huu ukutane na wenzako wenye mahitaji kama ya kwako.
Kwenye andiko lako ni vema ukasema ulipo, mkoa na wilaya ambako ungependa kwenda na mawasiliano yako. Tunashauri mtumie barua pepe kuliko nambari za simu kwa usalama zaidi.
ZIADA: Kama ilivyoripotiwa kwenye uzi wa Walimu Wanaotaka Kubadilishana Vituo, hata humu kunaweza kuwa na hatari ya matapeli ambao watatumia fursa kujipatia fedha, kukudhuru na wakati fulani kutaka kunufaika kingono (hasa kwa wanawake). IWENI MAKINI!