Mabagala
JF-Expert Member
- Nov 27, 2009
- 1,477
- 325
Hasa hasa nimeuona Zanzibar, naskia ni ugonjwa upo sana maeneo ya pwani pwani. Ile hali ya kujambishwa, yaani mtu anapita na kupuliza mdomo na kutoa sauti ya ushuzi basi jamaa wa pembeni yake anaumia, ama anaweza akajikunja au akavunja au kuchana vitu mbele yake. wakati niko zanzibar alimanusra huyu jamaa avunje computer yangu. Huku Ukerewe sijaona mtu akitokewa na hiyo hali, ni nini hii kitu jamani? ni samaki wanaokula ama wanakuwaje kuwaje ile sound ya hewa chafu iwaumize?. Na kwanini itokee huko pwani tu? Nisaidieni maana hata kugoogle nimeshindwa kizungu chake nitaanzaje