Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Musa Mkama
MNAJIMU Mkuu Afrika Mashariki Sheikh Yahya Hussein, ametabiri kuwa kutokea kwa madhara mengi ikiwamo kiongozi mmoja wa nchi za Mashariki ya Afrika kutekwa nyara.
Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake Magomeni jijini Dar es Salaam Sheikh Yahya bila kutaja wala kufafanua alisema kuwa kiongozi huyo atatekwa na kupinduliwa akiwa katika ndege.
"Natabiri kuwa kutatokea madhara mengi kama vile mitetemeko ya ardhi, mafuriko, hali mbaya ya hewa, migomo , mapinduzi na utovu wa nidhamu wa raia kwa viongozi wao... natabiri kuna kiongozi mmoja wa nchi za mashariki ya kiafrika kutekwa nyara au kuinduliwa akiwa katika ndege,"alisema.
Alitabiri matukio makubwa yatakayotokea na kuwakumba viongozi kuwa wabunge kufungwa au kufikwa na vifo vya ghafla pamoja na kupata kashfa mbaya na kufukuzwa kazi wakiwa nje.
Alisema kuwa kutatokea matatizo katika mambo ya Ulinzi na usalama hasa kwa viongozi wakuu wa nchi mabalimbali, waliolala wataamka na kutatokea mabadiliko makubwa katika mambo mbalimbali ya kisiasa kijamii.
"Nawatahadharisha viongozi wa kisisasa kwamba kila fikra na mawazo lazima yazingatiwe kwa uangalifu au inaweza kuleta mfarakano," alisema na kuongeza kuwa'
"Upinzani katika vyama vya siasa vinavyoatwala na visivyo tawala kupata nguvu na kutokea mabadiliko makubwa katika vyama hivyo".
Alitabiri pia kuwa waliolala wataamka bila kuwataja ni kina nani na kwamba kutokana na kuamka huko kutatokea mabadiliko makubwa katika mambo mbalimbali ya kisiasa na kijamii, watu kukumbatia tabia ya kizamani na kukuza mazingira mapya.
SOURCE: MWANANCHI.
MNAJIMU Mkuu Afrika Mashariki Sheikh Yahya Hussein, ametabiri kuwa kutokea kwa madhara mengi ikiwamo kiongozi mmoja wa nchi za Mashariki ya Afrika kutekwa nyara.
Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake Magomeni jijini Dar es Salaam Sheikh Yahya bila kutaja wala kufafanua alisema kuwa kiongozi huyo atatekwa na kupinduliwa akiwa katika ndege.
"Natabiri kuwa kutatokea madhara mengi kama vile mitetemeko ya ardhi, mafuriko, hali mbaya ya hewa, migomo , mapinduzi na utovu wa nidhamu wa raia kwa viongozi wao... natabiri kuna kiongozi mmoja wa nchi za mashariki ya kiafrika kutekwa nyara au kuinduliwa akiwa katika ndege,"alisema.
Alitabiri matukio makubwa yatakayotokea na kuwakumba viongozi kuwa wabunge kufungwa au kufikwa na vifo vya ghafla pamoja na kupata kashfa mbaya na kufukuzwa kazi wakiwa nje.
Alisema kuwa kutatokea matatizo katika mambo ya Ulinzi na usalama hasa kwa viongozi wakuu wa nchi mabalimbali, waliolala wataamka na kutatokea mabadiliko makubwa katika mambo mbalimbali ya kisiasa kijamii.
"Nawatahadharisha viongozi wa kisisasa kwamba kila fikra na mawazo lazima yazingatiwe kwa uangalifu au inaweza kuleta mfarakano," alisema na kuongeza kuwa'
"Upinzani katika vyama vya siasa vinavyoatwala na visivyo tawala kupata nguvu na kutokea mabadiliko makubwa katika vyama hivyo".
Alitabiri pia kuwa waliolala wataamka bila kuwataja ni kina nani na kwamba kutokana na kuamka huko kutatokea mabadiliko makubwa katika mambo mbalimbali ya kisiasa na kijamii, watu kukumbatia tabia ya kizamani na kukuza mazingira mapya.
SOURCE: MWANANCHI.