Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,708
Hebu tuchukulie kwamba umeolewa au kuoa,halafu una mafanikio makubwa kifedha mpaka inafikia mahali ndugu jamaa na marafiki zako na hata watu wengine wanatamani hayo mafanikio yako. . . . . . . .Kwa upande wa ndoa yako pia si haba umefanikiwa kupata mwenza anaekujali,mwenye upendo na anaejua hasa ndoa ni nini,anakufanya ujisikie mwenye thamani na mwenye furaha duniani.Kila anaekufahamu anatamani ndoa yako,wewe na mwandani wako ni kucheka tu.Mmefanikiwa kufahamika na mmejijengea heshima kutokana na mafanikio hayo ya ndoa na fedha!. . . . .Sasa anakuja malaika kutoka kwa Mungu anakuambia "nimeagizwa nikuondolee kimoja kati ya mwenza wako au mali zako,ila nimeambiwa nikuulize kwanza,utakachochagua ndicho nitakiondoa"!Je ungechagua nini na kwanini?