VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Katika hali isiyotarajiwa,Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limegoma kutoa Madaktari kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Madaktari wanaogoma katika Hospitali mbalimbali za Rufaa, Teule na nyinginezo.
Viongozi waandamizi wa Jeshi hilo Makao Makuu wameitaka Serikali kutafuta haraka suluhu ya mgomo huo badala ya kukimbilia kwa Jeshi kwa msaada huku tatizo likibaki.
'Tumewaambia waende wakatafute suluhisho' alisema mmoja wa Maafisa Waandamizi wa JWTZ mwenye cheo cha Brigedia Jenerali. 'Hii tabia siyo njema. Tatizo halitakwisha kwakuwa Serikali itakuwa na uhakika wa huduma ingawa si rasmi' aliongeza.
Serikali ifanye nini sasa?
Viongozi waandamizi wa Jeshi hilo Makao Makuu wameitaka Serikali kutafuta haraka suluhu ya mgomo huo badala ya kukimbilia kwa Jeshi kwa msaada huku tatizo likibaki.
'Tumewaambia waende wakatafute suluhisho' alisema mmoja wa Maafisa Waandamizi wa JWTZ mwenye cheo cha Brigedia Jenerali. 'Hii tabia siyo njema. Tatizo halitakwisha kwakuwa Serikali itakuwa na uhakika wa huduma ingawa si rasmi' aliongeza.
Serikali ifanye nini sasa?