JWTZ: Msemaji wa Jeshi, Kanali Mgawe atoa kauli kuhusu Jeshi kulinda amani nchini

Hapa kuna kitu kinatengenezwa, nyie subirini huko mbeleni kama hawa jamaa hawajang'ang'ania magogoni kwa mgongo wa usalama wa nchi. Hehehe yangu macho!!
 
hujanielewa siongelei kikatiba hapa naongelea kivita...nchi ishashindikana so ni bora jeshi lichukue nchi...katiba yenyewe ingekua inafuatiliwa tusingekua hapa tulipo
kwa hiyo busara yako inakutuma kuvunja katiba ili kumchukulia hatua mtu anayevunja katiba!!
 
......... Mkwala mzito sana .... lakini kama inafanyika kwa haki na usawa hakuna tatizo ............ ila tu wasije wakaingiliana na akina Kamuhanda!
 
Kama hawatakuwa wanawarushia raia wema vile vitu vyenye ncha kali (Vile vya Chagonja vile) haina shida waache wongeze nguvu cause polisi wanaua sana bila sababu za msingi
 
Kwa tafsiri nyepesi ni kwamba Sheik Said Mwema na Maalim Kova kazi imewashinda. Wanakamata wahalifu, halafu waandamanaji wanakuja mpaka mlangoni kwako, unaogopa, unawaachia. Sijawahi ona duniani jeshi la namna hiyo.
 
Kama jeshi litatumika kusaidia polisi kuwadhibiti "WAHUNI" sina tatizo na hilo. Kama vipi hii mikutano na maandamano yoote ripoti iwe inapelekwa polisi na nakala kwa mkuu wa kambi ya jeshi iliyopo karibu ili atume ujumbe wake kuona nani ataanzisha fujo!
 
tyt.jpg

Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe

--
JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limewataka wananchi kuepuka vurugu zinazohatarisha usalama, na kulinda amani iliyopo nchini

JWTZ imetoa kauli hiyo siku moja baada ya waumini wa dini ya Kiislamu jijini Dar es Salaam kuandamana sababu ya malalamiko kadhaa kama kukamatwa kwa Sheikh Issa Ponda na wafuasi wake 49 wiki iliyopita kwa tuhuma mbalimbali, kutoweka kwa kiongozi wa UAMSHO Sheikh Amir Farid Hadi, na malalamiko mengine.

Msemaji wa JWTZ, Kanali Kapambala Mgawe, amesema hatua ya wanajeshi kujitokeza katika kuzima vurugu zilizotokea jijini juzi, ilikua na lengo la kuwaonyesha wananchi kwamba JWTZ ipo kikazi zaidi, na anayetaka vurugu atashughulikiwa kisheria.


“Juzi tulionyesha ‘talent show force’ ili watujue kama tupo kazini, hata kama wametuona tupo kimya, hatuna mzaha katika kulinda na kusimamia ulinzi na usalama wa taifa hili, kwa hiyo tulikuwa kwenye sehemu ya utekelezaji wa majukumu yetu, na kwamba atakayekwenda kinyume tutamshughulikia,” alisema Mgawe.

Alisema zoezi hilo litaendelea kwa maandamano yoyote yatakayoonyesha dalili za kuhatarisha usalama wa nchi. Aliongeza kwamba wanajeshi watashiriki kikamilifu ili kuhakikisha kuwa wananchi wanafuata sheria na taratibu zilizopangwa, bila ya kuathiri usalama wa nchi.

Alisema kwa sasa wanasubiri kibali cha polisi cha kuhusu kuhitaji msaada ili waweze kuungana nao katika kushughulikia maandamano yenye lengo la kuhatarisha amani na utulivu.

“Tunawataka wananchi kufuata sheria na taratibu zilizopo na kuepuka kuhatarisha amani ya nchi, kama wanataka tuingie kazini tutafanya hivyo, ila tunachowaasa ni kufuata taratibu zilizopo,” alisisitiza.

Katika vurugu za juzi, watu 53 walitiwa mbaroni kwa tuhuma za kushiriki kwenye maandamano. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, watu hao watafikishwa mahakamani Oktoba 22 mwaka huu.

Nimepata wasiwasi na kauli hii hususani hapo kwenye RED Hii inaonyesha tunakoelekea sio kuzuri tumeshuhudia polisi wakiua kwenye maandamano sasa naona CCM wanabadilisha utaratibu wanataka kutumia Jeshi sasa kuthibiti upinzani hususani CDM. nachohisi muda sio mrefu tutaingia katika umwagaji wa damu kwa matumizi ya nguvu yasiyo ya lazima.
 
Naunga mkono hoja Mgawe yuko sahihi.
Unaunga mkono kwa mtazamo husio mpana lakini mwisho wa siku utajua kwa nini kasema hivyo pale nao watakapoanza kuingilia mikutano ya kisiasa kwa hicho kisingizio cha usalama wa nchi.
 
Safi sana JWTZ, hakikisheni usalama wa taifa hili unadumishwa. Ninawaunga mkono kwa 100%. Najiskikia kujivuna kwa kuwa na jeshi mahiri na la kizalendo kama ninyi. Keep it up.
 
Wakuu kuna jambo moja ambalo nililionyesha katika hoja yangu ya juzi kwamba JWTZ wamekosea kuingia barabarani huku wakiwa hawajawasiliana na polisi.

Hii ndio kosa la kiufundi nililolitanabaisha.

Kamanda Kova alipohojiwa na BBC siku ya Ijumaa alisema kwamba JWTZ walikuwa barabarani kwa shughuli zao na wao polisi nao walikuwa na shughuli zao kutuliza ghasia. Hivyo majibu ya kamanda Kova yalimaanisha kwamba hata polisi hawakupenda uwepo wa JWTZ mabarabarani, kwamba ingeonekana polisi wameshindwa kazi.

Nikatoa nafasi kwa wanachama wenzangu kusaidia kutoa majibu kwamba ni kwanini kosa lile la kiufundi lilijitokeza, lakini kwa bahati mbaya hakuna aliekuja na moja ya sababu ya JWTZ kuamua kuingia barabarani.

Sasa Kanali Mgawe anasema kwamba wansubiri kibali kutoka polisi ili kiwaruhusu kuingia tena barabarani hivyo kumaanisha kwamba JWTZ waliingia barabarani kimakosa au kwa kukosa mawasiliano mazuri na polisi.

Wakuu, kama hali ni hii basi Tanzania watu wanakuwa hawako na taaluma muhimu inayohusu mawasiliano kiasi cha kila mtu kujiamulia anachoona kinafaa.

Ha hiyo ni hatari.
 
Nawapongeza JWTZ kwa mlichofanya. Kwa watanzania wapenda amani wote wataunga mkono kila hatua ya kulinda amani ya nchi yetu. Hawa waislamu wamezoea vibaya. Wameaminishwa kuwa maandamano ndo yatawapa kila wanachokitaka. Walipoandamana na kuwatoa wagomea sensa wakajua ndo fashion yao ya ushindi. Wanastahili kupigwa sana na ikibidi wafe kadhaa ili akili zao zikae kitaifa. Very good JWTZ.... Kanyagieni hapo hapo... You have made my day!!! BRAVOOOOOO!!!!!:A S tongue:
 
Chonde chone '' GARI JUEPE LA NISSAN PATROL LENYE TINTED, NDANI WAMO WATU WENYE SILAHA WANARANDA MAENEO MBALI MBALI ZANZIBAR KUWATAFUTA MAADUI WA KIISLAMU, HAO NI WAPIGANAJI WA UAMSHO WANA SILAHA ZA JADI MAPANGA NA ZA KISASA, WAMEFUNIKA USO, INAWACHUKUA SECONDE CHACHE KUMALIZA KAZI NA KUKIMBIA, GARI YAO HAINA NAMBA'' mtahadharishe unaempenda.
 
Kwangu Chadema si muhimu kuliko amani ndani ya nchi, anayeogopa tamko la jeshi yeye ni mhalifu tu, hakuna swala la kuwa eti Chadema ndio Targeted huu ni uongo ambao hauwezi kuingia akilini mwangu, watu wanaotaka kuleta machafuko wanajulikana na ndio maana wameonywa ili wasije kusema hawakuonywa. Jeshi halina mpango wowote na Chadema. I don't buy this ****.
 
hii serikali haieleweki, juzi baada ya maandamano kova aliulizwa kuhusu magari ya kijeshi kuwepo mitaani akakanusha kua alikua hana habari na wanajeshi hao na kwamba labda walikuwepo hapo kwa shuhuli zao zingine..leo msemaji wa jeshi anasema walikuwepo pale ili kujionyesha kua wapo kazini na eti wanasubiri kibali cha polisi..huo ni uongo mtupu..hata siku moja jeshi halisubiri kibali kutoka popote hata kwa Rais..

MKUU wa majeshi akiona hali ya nchi si shwari basi ana nguvu ya kuingia mtaani na jeshi lake bila kibali kutoka ikulu wala mahali popote...na mimi ningeomba mkuu wa majeshi akiona hali ya usalama inazidi kua mbaya na wananchi wanazidi kupoteza maisha yao basi waingie na ikulu wawatoe wote tufanye uchaguzi mpya nchi ianze upya.....

Naunga mkono hoja (√)
 
Back
Top Bottom