Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
1. Je, ugharamiaji wa Mahakama za Kadhi unaweza kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977? Ndiyo!
Ibara ya 19 (2) inaeleza kwamba "Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za ma mamlaka ya nchi". Kwa kuwa Waislamu wamesema kwamba uendeshaji wa Mahakama za Kadhi ni kuendesha ibada Mamlaka ya nchi haitakiwi kuingilia ibada hizo bali wahusika waachwe waendelee na uendeshaji ambalo ni jambo la mtu binafsi.
2. Je, kuwepo kwa Mahakama za Kadhi Zanzibar ni kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? Hapana!
NYONGEZA YA KWANZA ya Katiba hiyo imetaja Orodha ya Mambo ya Muungano na suala la Uenezaji wa Dini, Kufanya Ibada, Kutangaza Dini sio la Muungano. Pia suala la Mahakama zote isipokuwa Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano sio jambo la Muungano. Kwa hiyo suala hili ni la Tanzania Bara pekee ambapo utangazaji wa dini upo nje ya Mamlaka ya Nchi. Katika Ibara ya 99 (2) (b) ya Katiba ya Zanzibar, 1984 imeandikwa kwamba Mahakama ya Rufaa ya Jamhuri ya Muungano haitahusika na mambo ya Kiislamu ambayo yameanzia katika Mahkama za Kadhi. Kwa hiyo Mahakama za Kadhi za Zanzibar zimeanzishwa kwa Sheria za Zanzibar kama zilivyo Mahakama zingine hadi Mahakama Kuu, isipokuwa Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
3. Je, kuna mtu amewakataza Waislamu kuunda Mahakama za Kadhi? Hapana! Wafuate Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 kuhusu uenezaji wa dini na sio kunukuu Katiba za Kenya, Ethiopia, Uganda, n.k.!
Ibara ya 19 (2) inaeleza kwamba "Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za ma mamlaka ya nchi". Kwa kuwa Waislamu wamesema kwamba uendeshaji wa Mahakama za Kadhi ni kuendesha ibada Mamlaka ya nchi haitakiwi kuingilia ibada hizo bali wahusika waachwe waendelee na uendeshaji ambalo ni jambo la mtu binafsi.
2. Je, kuwepo kwa Mahakama za Kadhi Zanzibar ni kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? Hapana!
NYONGEZA YA KWANZA ya Katiba hiyo imetaja Orodha ya Mambo ya Muungano na suala la Uenezaji wa Dini, Kufanya Ibada, Kutangaza Dini sio la Muungano. Pia suala la Mahakama zote isipokuwa Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano sio jambo la Muungano. Kwa hiyo suala hili ni la Tanzania Bara pekee ambapo utangazaji wa dini upo nje ya Mamlaka ya Nchi. Katika Ibara ya 99 (2) (b) ya Katiba ya Zanzibar, 1984 imeandikwa kwamba Mahakama ya Rufaa ya Jamhuri ya Muungano haitahusika na mambo ya Kiislamu ambayo yameanzia katika Mahkama za Kadhi. Kwa hiyo Mahakama za Kadhi za Zanzibar zimeanzishwa kwa Sheria za Zanzibar kama zilivyo Mahakama zingine hadi Mahakama Kuu, isipokuwa Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
3. Je, kuna mtu amewakataza Waislamu kuunda Mahakama za Kadhi? Hapana! Wafuate Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 kuhusu uenezaji wa dini na sio kunukuu Katiba za Kenya, Ethiopia, Uganda, n.k.!