Mgoyangi
Senior Member
- Feb 6, 2008
- 184
- 9
Najaribu kupitia makala mbali mbali zinzohusu, Jumuia za Kiraia Tanzania ikiwa ni pamoja na NGO, nakuta lawama kuwa, hivi ni vijiwe vya wasomi wanajipachika huko kupata ajira na kuganga njaa, na kisha kujipachika majina kama Wanaharakati, wakati Mwingine Marais.
Lakini pia naona Wapinzani na Chama Tawala nao pia wanazishambulia asasi hizi wakati mwingine, na wakati huo huo naona pia serikali imewahi kuwa kwenye mivutano na asasi hizi zisizo za kiserikali, Haki Elimu na kufutwa kwa BAWATA ni mifano halisi.
Je kwa Jumuia hizi za Kiraia zikiwemo NGO, Serikali, Wanasiasa, wote hawa wanafanya kazi kwa maslahi ya umma?
Je kuna tafiti gani ya uhakika ambayo imewahi kufanywa kama tathmini ya hali ya Jumuia za Kiraia Tanzania, mahusiano yake kwa umma, changamoto na mafanikio yaliyokwisha patikana?
Mwenye nondo naomba anishushie hapa.
Lakini pia naona Wapinzani na Chama Tawala nao pia wanazishambulia asasi hizi wakati mwingine, na wakati huo huo naona pia serikali imewahi kuwa kwenye mivutano na asasi hizi zisizo za kiserikali, Haki Elimu na kufutwa kwa BAWATA ni mifano halisi.
Je kwa Jumuia hizi za Kiraia zikiwemo NGO, Serikali, Wanasiasa, wote hawa wanafanya kazi kwa maslahi ya umma?
Je kuna tafiti gani ya uhakika ambayo imewahi kufanywa kama tathmini ya hali ya Jumuia za Kiraia Tanzania, mahusiano yake kwa umma, changamoto na mafanikio yaliyokwisha patikana?
Mwenye nondo naomba anishushie hapa.