Mkulima wa Kuku
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 1,270
- 533
Kwa masikitiko makubwa nashangazwa na ukimya huu wa jumuiya ya kimataifa pamoja na washirika wake wakuu kama Marekani na Uingereza wakinyamazia vitendo vya kihuni vinavyofanywa na serikali ya CCM kwa makusudi ya kuua upinzani ili wajitengenezee mazingira ya kubaki madarakani kiimla.
Nionavyo ni kuwa wameamua kunyamaza kimya kwa ajili ya shosti wao aliyetayari kuwapa rasilimali za nchi yetu kwa manufaa yake binafsi. Haieleweki nchi nyingine kakitokea kajambo kadogo wanaojiita wakuu wa jumuiya hiyo inayoongozwa na Ban Ki Moon akisaidiwa na Dr. Asha Rose Migiro wakiwa wamenyamaza kimya kabisa hata kutoa comment nyepesi tu ya kukemea. Ina maana gani? Ikifanywa ni ccm ruksa, ikifanywa dhidi ya wasio ccm ni laana.
Nimegundua kwa siku hizi yafuatayo:
1. Hakuna maslahi ya nchi kupigiwa kelele -anayepiga kelele anaitwa adui na kuitiwa polisi wa kumdhibiti
2. Kudhibiti kwa kutumia nguvu kila anayedai haki -kuanzia mikopo ya vyuo vikuu, haki ya kudai Umeya wa Arusha umechakachuliwa, wananchi wa Mwanza Mbeya na Iringa (miji iliyo ngome za upinzani) kuendelea kunyanyaswa na majeshi ya polisi
3. Vitisho vya wazi kwa maelekezo uvurugaji nchi
4. wakuu wa mikoa na wilaya kutumiwa kwa maslahi ya chama tawala
5.Zuio la mikutano ya chama cha demokrasia na maendeleo kwa kisingizio cha Al-shabaab (hawajawahi kutuchokoza, ila mkuu wa nchi ameamua kuingiza chokochoko kwa kisingizio cha Kenya) bila ya kujua ukweli wa siasa za Kenya/Somalia (akidhani suala pale ni ugaidi)
6. Sasa suala la katiba ambalo linachezewa na wabunge wasio na uchungu na nchi yetu kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Kwa hiyo:
1. Lazima jumuiya hiyo ya kimataifa ijue kuwa Tanzania ni ya watatnzania na tunastahili kufaidi mali zetu na ni lazima watoe matamko juu ya ukiukwaji mkubwa wa Demokrasia unaondelea sasa
2. Wamkemee Kikwete waziwazi waache unafiki wao wa kutaka Uranium kwa kisingizio cha URAFIKI wao na kwa kumtumia JK
3. Wananchi wa Tanzania sasa wameamka na hawataki tena ujinga uliokuwa unafanywa na ccm kwa miaka 50 bila kuleta maendeleo ya maana.
4. Sasa watanzania wakiandamana kwa ajili ya katiba hakuna bunduki itakayoweza kuwazuia kufanya wanalotaka.
Kama basi Kikiwete amechoka na amani ya nchi yetu, aendelee na ushenzi huu anaoufanya kutumia polisi.
Tumechoka tuko tayari kufia rasilimali zetu!
Nawasilisha
Nionavyo ni kuwa wameamua kunyamaza kimya kwa ajili ya shosti wao aliyetayari kuwapa rasilimali za nchi yetu kwa manufaa yake binafsi. Haieleweki nchi nyingine kakitokea kajambo kadogo wanaojiita wakuu wa jumuiya hiyo inayoongozwa na Ban Ki Moon akisaidiwa na Dr. Asha Rose Migiro wakiwa wamenyamaza kimya kabisa hata kutoa comment nyepesi tu ya kukemea. Ina maana gani? Ikifanywa ni ccm ruksa, ikifanywa dhidi ya wasio ccm ni laana.
Nimegundua kwa siku hizi yafuatayo:
1. Hakuna maslahi ya nchi kupigiwa kelele -anayepiga kelele anaitwa adui na kuitiwa polisi wa kumdhibiti
2. Kudhibiti kwa kutumia nguvu kila anayedai haki -kuanzia mikopo ya vyuo vikuu, haki ya kudai Umeya wa Arusha umechakachuliwa, wananchi wa Mwanza Mbeya na Iringa (miji iliyo ngome za upinzani) kuendelea kunyanyaswa na majeshi ya polisi
3. Vitisho vya wazi kwa maelekezo uvurugaji nchi
4. wakuu wa mikoa na wilaya kutumiwa kwa maslahi ya chama tawala
5.Zuio la mikutano ya chama cha demokrasia na maendeleo kwa kisingizio cha Al-shabaab (hawajawahi kutuchokoza, ila mkuu wa nchi ameamua kuingiza chokochoko kwa kisingizio cha Kenya) bila ya kujua ukweli wa siasa za Kenya/Somalia (akidhani suala pale ni ugaidi)
6. Sasa suala la katiba ambalo linachezewa na wabunge wasio na uchungu na nchi yetu kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Kwa hiyo:
1. Lazima jumuiya hiyo ya kimataifa ijue kuwa Tanzania ni ya watatnzania na tunastahili kufaidi mali zetu na ni lazima watoe matamko juu ya ukiukwaji mkubwa wa Demokrasia unaondelea sasa
2. Wamkemee Kikwete waziwazi waache unafiki wao wa kutaka Uranium kwa kisingizio cha URAFIKI wao na kwa kumtumia JK
3. Wananchi wa Tanzania sasa wameamka na hawataki tena ujinga uliokuwa unafanywa na ccm kwa miaka 50 bila kuleta maendeleo ya maana.
4. Sasa watanzania wakiandamana kwa ajili ya katiba hakuna bunduki itakayoweza kuwazuia kufanya wanalotaka.
Kama basi Kikiwete amechoka na amani ya nchi yetu, aendelee na ushenzi huu anaoufanya kutumia polisi.
Tumechoka tuko tayari kufia rasilimali zetu!
Nawasilisha