NGOSWE.120
JF-Expert Member
- Jul 9, 2011
- 219
- 233
UPDATES a.k. a Feedback about Talaka
Wapendwa Wana MMU nawashukuru sana kwa ushauri mbali mbali mlionipatia juu ya sred yangu hii iliyokuwa inahusu kutaka kumtaliki mke wangu mpenzi. Japokuwa michango iliyokuwa mingi ilikua bias kuegemea upande mmoja huku ikiambatana na lugha kali zingine zisizoweza vumilika binafsi niliona ni busara kupokea yote hayo kama changamoto ili kuweza kupata suluhu ya huu mgogoro na huyu mke wangu.
Kifupi ni kuwa hadi muda huu bibie bado sijamkabidhi talaka yake na wala sijamtakia kuhusu hilo jambo. Nimezidi kuwa mvumilivu juu ya hiyo hali yake ya kuninunia hadi hii leo. Kwa kuwa wengi mmesema mimi ndio mkorofi nimelipokea hilo lakini naomba mtambue kuwa mimi sipo hivyo mnifikiriavyo, na pamoja na hayo yote afanyayo juu yangu lakini ndani ya moyo wake anatambua thamani ya upendo wangu kwake.
Nimefuta wazo la kumpa talaka toka nipate ushauri wenu hasa juu usumbufu wa malezi ambao ataupata mtoto wetu mpendwa lakini jana nikiwa kazini saa 4 asubuhi I was so surprised nilipopata sms kutoka kwa mke wangu akiniambia kuwa yeye anataka akaishi peke yake kwa sasa hivyo nimpe muda ajipange, atakapokuwa tayari ataniambia. Sijamuelewa kwanini aseme hivyo au ni kosa gani hasa aliloona nimefanya.
KUVUNJA UKIMYA:
Leo nilikaa nae na kuweza kumuuliza kwa upole na utaratibu huku nikimuuliza kama kuna jambo lolote lile linalomsibu hadi kufikia hatua ya kununa kwa muda wote huu bila kuzungumza nami(akiondoa salamu tu ..ambayo mimi ndio huanzisha hiyo salamu). Wapendwa wana MMU huwezi amini...kwa kujiamini kabisa ameniambia yeye hana tatizo lolote na huo mnuno wake kwangu ni kwa sababu yupo busy na mambo yake. Kwa hilo jibu nikawa hoi na hata baada ya kumbembeleza awe muwazi kama kuna jambo namkwaza amesema hapana ila yeye yupo tu busy na mambo yake.
Kuhusu kunitumia msg amesema hiyo niielewe hivyo hivyo ..kuwa anataka akaishi peke yake na kwa sasa anajipanga na atakapokuwa tayari ataniambia. Nikamuuliza usemayo ni sahihi au unatania ...amesema ni sahihi tena kwa asilimia mia tatu....!
HITIMISHO:
Ndoa ni makubaliano ya watu wawili...wapendanao...kama upendo hakuna ...that means hakuna ndoa....ila ni maigizo tu ya ndoa. Kwa kuzingatia ushauri wenu juu ya matunzo ya mtoto nitajitahidi kwa hali na mali kuhakikisha nampatia malenzi/matunzo stahiki. Atakapokuwa tayari na kunipa taarifa kuwa sasa anaondoka hapo ndio maisha yangu ya ubachelor yataanza rasmi.
NB: Sina sababu ya kuita wazee au wazazi wa pande zote mbili kujadili hili suala kwa sababu ndoa hii ni ya mimi na yeye hivyo kuwaita wazee au wazazi ni kama kulazimisha mahusiano yaendelee na kesho yakitokea mengine tuwaite..tena kusuluhisha...hiyo haitakuwa tena ndoa bali ni maigizo ya ndoa.
Poleni kwa maelezo marefu lakini nia yangu ilikuwa ni kufafanua jambo hili kwa kina hasa baada ya kupata ushauri wenu.
Asanteni sana wana MMU.
@Ngoswe.120
Wapendwa Wana MMU nawashukuru sana kwa ushauri mbali mbali mlionipatia juu ya sred yangu hii iliyokuwa inahusu kutaka kumtaliki mke wangu mpenzi. Japokuwa michango iliyokuwa mingi ilikua bias kuegemea upande mmoja huku ikiambatana na lugha kali zingine zisizoweza vumilika binafsi niliona ni busara kupokea yote hayo kama changamoto ili kuweza kupata suluhu ya huu mgogoro na huyu mke wangu.
Kifupi ni kuwa hadi muda huu bibie bado sijamkabidhi talaka yake na wala sijamtakia kuhusu hilo jambo. Nimezidi kuwa mvumilivu juu ya hiyo hali yake ya kuninunia hadi hii leo. Kwa kuwa wengi mmesema mimi ndio mkorofi nimelipokea hilo lakini naomba mtambue kuwa mimi sipo hivyo mnifikiriavyo, na pamoja na hayo yote afanyayo juu yangu lakini ndani ya moyo wake anatambua thamani ya upendo wangu kwake.
Nimefuta wazo la kumpa talaka toka nipate ushauri wenu hasa juu usumbufu wa malezi ambao ataupata mtoto wetu mpendwa lakini jana nikiwa kazini saa 4 asubuhi I was so surprised nilipopata sms kutoka kwa mke wangu akiniambia kuwa yeye anataka akaishi peke yake kwa sasa hivyo nimpe muda ajipange, atakapokuwa tayari ataniambia. Sijamuelewa kwanini aseme hivyo au ni kosa gani hasa aliloona nimefanya.
KUVUNJA UKIMYA:
Leo nilikaa nae na kuweza kumuuliza kwa upole na utaratibu huku nikimuuliza kama kuna jambo lolote lile linalomsibu hadi kufikia hatua ya kununa kwa muda wote huu bila kuzungumza nami(akiondoa salamu tu ..ambayo mimi ndio huanzisha hiyo salamu). Wapendwa wana MMU huwezi amini...kwa kujiamini kabisa ameniambia yeye hana tatizo lolote na huo mnuno wake kwangu ni kwa sababu yupo busy na mambo yake. Kwa hilo jibu nikawa hoi na hata baada ya kumbembeleza awe muwazi kama kuna jambo namkwaza amesema hapana ila yeye yupo tu busy na mambo yake.
Kuhusu kunitumia msg amesema hiyo niielewe hivyo hivyo ..kuwa anataka akaishi peke yake na kwa sasa anajipanga na atakapokuwa tayari ataniambia. Nikamuuliza usemayo ni sahihi au unatania ...amesema ni sahihi tena kwa asilimia mia tatu....!
HITIMISHO:
Ndoa ni makubaliano ya watu wawili...wapendanao...kama upendo hakuna ...that means hakuna ndoa....ila ni maigizo tu ya ndoa. Kwa kuzingatia ushauri wenu juu ya matunzo ya mtoto nitajitahidi kwa hali na mali kuhakikisha nampatia malenzi/matunzo stahiki. Atakapokuwa tayari na kunipa taarifa kuwa sasa anaondoka hapo ndio maisha yangu ya ubachelor yataanza rasmi.
NB: Sina sababu ya kuita wazee au wazazi wa pande zote mbili kujadili hili suala kwa sababu ndoa hii ni ya mimi na yeye hivyo kuwaita wazee au wazazi ni kama kulazimisha mahusiano yaendelee na kesho yakitokea mengine tuwaite..tena kusuluhisha...hiyo haitakuwa tena ndoa bali ni maigizo ya ndoa.
Poleni kwa maelezo marefu lakini nia yangu ilikuwa ni kufafanua jambo hili kwa kina hasa baada ya kupata ushauri wenu.
Asanteni sana wana MMU.
@Ngoswe.120