Julius Mtatiro kushitakiwa kwa uchochezi

Jeshi la Polisi linaendelea kumshikilia Julius Mtatiro na habari za ndani zinadokeza kuwa baada ya habari ya kukamatwa kwake kuwekwa hadharani na wenu mtiifu Jeshi la POlisi limepania kutoa funzo. Baada ya kutoa siri kuwa Mtatiro anashikiliiwa kituo cha POlisi Msimbazi, habari za uhakika zinasema kuwa Jeshi hilo linaloongozwa na Said Mwema, na Kanda ya Dar na Suleiman Kova limeanza mtindo wa kumhamisha hamisha ili hatimaye wamfikishe mahakamani.

Vyanzo hivyo vimeithibitishia KLHN kuwa Bw. Mtatiro amekuwa subjected to mental torture ili aweze kukubali kuwa yeye ndiye kinara wa mgomo wa wanafunzi.

"ndiyo, hajalala kwa siku tatu, chakula kimekuwa cha shida, na hata sasa jeshi halitaki kusema wazi kuwa linamshikilia na linamshikilia kwa misingi gani" kilisema chanzo chetu ambacho kiko karibu kabisa na suala hili.

Mipango ya kumfikisha mahakamani imeandaliwa licha ya ukweli kuwa hadi sasa imekuwa ni zaidi ya masaa 48 tangu akamatwe kininja siku ya Jumapili. Habari hizo zinasema kuwa Bw. Mtatiro anashikiliwa kwenye kituo cha Salenda ambapo Mkuu wa Upelelezi wa Kanda ya Dar Bw. Mkumbo akidai kuwa "watatoa funzo" kwa wale wote wanaoeneza migomo.

Juhudi za kumpata msemaji wa Polisi zimeshindikana baada ya simu yake kuita bila kujibiwa.

Mwanakijiji, hatuwezi kuvumilia ujinga huu katika zama hizi, hizo zilikuwa zama za Mfumo wa Chama Kimoja.

Kwa kuwa uko Majuu jitahidi kuwasiliana na Amnest International, haiwezekani mtu ashilikiliwe siku 3 bila kufikishwa mahakamani na bila kupewa haki ya kumwona Wakili wake. Ni ukiukwaji mkubwa wa haki ya Mwanadamu, we need to shout. Badala ya watawala wetu kupambana kwa hoja sasa wanaanza kuweka watu vizuizini, very unfair.

Mbona Mafisadi wa EPA waliosababisha vifo vya Watoto, Wamama Wajawazito kwa kukosa dawa walifikishwa Mahakamani na hawakuzuiliwa? Shame!
 
Hivi Daruso siku hizi haina mwanasheria. Kwa nini viongozi wa Daruso na mwanasheria wao wasijikusanye na kwenda huko polisi makao makuu kuhusu hili halafu bidae kwenye vyombo vya habari??????????
 
Hivi Daruso siku hizi haina mwanasheria. Kwa nini viongozi wa Daruso na mwanasheria wao wasijikusanye na kwenda huko polisi makao makuu kuhusu hili halafu bidae kwenye vyombo vya habari??????????

Nyambala, Jeshi la Polisi hawataki hata kukiri kuwa wanamshikilia licha ya kuonekana naye Msimbazi, Central na sasa Salenda, labda anafanya the proverbial "kuisaidia Polisi". Nadhani ndugu zake wanaona fahari kuwa Jeshi linamhitaji kiasi hicho!
 
Du pole sana Mtatiro!sasa inakuwaje mtamsaidiaje huyu Mtatiro?

Jamani hakuna mawakili wa kujitolea kumsaidia huyu kijana? Invisible jaribu kuangalia ni jinsi gani tunaweza kutoa michango mie nikiwa wa kwanza. Nitumie PM kama kuna utaratibu huo ili tuangalie jinsi ya kusaidiana.
Nahamasisha, invisible take from here.
 
Sijui nitapata wapi contacts za viongozi wengine wa TAHLISO na DARUSO. Tutahakikisha tunaifundisha adabu hii serikali ya kiimla.

Kwanza na waandishi wa habari huko nyumbani wajitahidi kuufahamisha umma kwamba serikali yetu imeamua kutumia nguvu kunyamazisha wanaodai haki zao.Jana nilitoa wito tena kwamba wanafunzi wote na viongozi wa vyuo vilivyofungwa popote walipo wahamasishane na kufanya maandamano yasiyo na kikomo kuhakikisha wenzao woote waliokamatwa wanaachiwa

Pili,viongozi wa vyama vya siasa na wanaharakati wa makundi mengine ya kijamii waingilie kati hili suala. Kwanza kumfungia,kumhoji na kumtesa mtu kwa muda wa masaa 48 bila kumfikisha mahakamani ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Kwa hili serikali yetu tutaipa heshima gani au kuitofautisha vipi na serikali ya IDD AMIN au akina Sani Abacha.HATUWEZI kukubali kwa gharama yoyote.
 
Jamani hakuna mawakili wa kujitolea kumsaidia huyu kijana? Invisible jaribu kuangalia ni jinsi gani tunaweza kutoa michango mie nikiwa wa kwanza. Nitumie PM kama kuna utaratibu huo ili tuangalie jinsi ya kusaidiana.
Nahamasisha, invisible take from here.

Shukrani ubarikiwe baba.... Hii nguvu polisi wetu wangeitumia kupambana na wanao ua na kutesa maalbino naona tatizo lingeisha.
 
Nyambala, Jeshi la Polisi hawataki hata kukiri kuwa wanamshikilia licha ya kuonekana naye Msimbazi, Central na sasa Salenda, labda anafanya the proverbial "kuisaidia Polisi". Nadhani ndugu zake wanaona fahari kuwa Jeshi linamhitaji kiasi hicho!

Hii inabidi ijulikane kwa umma thru vyombo vya habari. Nadhani si sahihi kulaumu ndugu zake especially kwa sasa maana inategemea wako kona ipi ya nchi na je hizi habari wanazo. Nnachokishangaa ni kwa nini yule mwanasheria wa Daruso mpaka sasa hajasikika au naye yuko mbaroni which I don't think it is.
 
Habari nilizozipata zinasema kuwa Bw. Mtatiro ameachiliwa na Polisi muda si mrefu uliopita kwa dhamana. KLHN inatarajiwa kuzungumza naye baadaye mchana huu katika Exclusive Interview...
 
Huyu Mtatiro inakuwaje hadi leo awe kiongozi wa wanafunzi hadi leo? hao TAHLISO huwa hawafanyi uchaguzi hadi baada ya graduation?
 
ooh, okay.....kwa hiyo huyo anainfluence kuanzia primary schools, wazee wa iliyokuwa jumuiya ya afrika masharika, walimu na wanafunzi wa vyuo vyote na wote wanaojiandaa kugoma kumbe.
 
ooh, okay.....kwa hiyo huyo anainfluence kuanzia primary schools, wazee wa iliyokuwa jumuiya ya afrika masharika, walimu na wanafunzi wa vyuo vyote na wote wanaojiandaa kugoma kumbe.

Hivyo ndivyo inaonekana Polisi wanaamini
 
ooh, okay.....kwa hiyo huyo anainfluence kuanzia primary schools, wazee wa iliyokuwa jumuiya ya afrika masharika, walimu na wanafunzi wa vyuo vyote na wote wanaojiandaa kugoma kumbe.

Hivyo ndivyo inaonekana Polisi wanaamini.
 
Taarifa ni kuwa Mtatiro leo kapelekwa mahakamani kwenye mahakama ya Kisutu na kusomewa shitaka la uchochezi kwa mujibu wa newspaper act ya mwaka 1976 , ila aliweza kuwekewa dhamana na kutolewa na ndugu jamaa na marafiki na hata kati nyetu wengine tulikuwa mahakamani hapo.

Pili kijana Odwar Odong yeye mpaka sasa unafanyika utaratibu kupitia idara ya uhamiaji ili aweze kurudishwa nchini mwake Uganda.

Tatu wale wafuatiliaji wa mambo watakumbuka kuwa mwaka 1971 mwanafunzi wa UDSM aliyekuwa anajulikana kama Akivaga alirudishwa kwao Kenya kwenye mazingira kama haya na hii ilipelekea wanafunzi kugoma mpaka serikali ilipotii amri na kumrudisha chuoni hapo mtakumbuka wakina Spika Sitta walikuwa ndio vinara enzi hizo na wengineo wengi.

Ntawajulisha yaliyojiri kadiri nitakavyoyapata , nategemea kiukutana nae muda wowote kutoka sasa kwa ajili ya kunipa yaliyojiri humo alimokuwa na kuweza kuchukua taarifa zote muhimu.

Odwar Odong yeye bado anashikiliwa na polisi mpaka sasa na utaratibu unafanyika uhamiaji na hata Suleiman Kova leo amekiri suala hilo kuwa wanatarajia kumrudisha kwao UGANDA.

How about EAC ? TUTAFIKA?
 
Hivyo ndivyo inaonekana Polisi wanaamini

hawa polisi wana akili nyingi sana......sijui mafunzo walipatia wapi maana wanajua kusoma alama za nyakati mnooooo. Anyway, huyu kijana atakuja kuwa kiongozi URT (may be Tanganyika) miaka ijayo. Mpeni salamu zangu.
 
Hivi Daruso siku hizi haina mwanasheria. Kwa nini viongozi wa Daruso na mwanasheria wao wasijikusanye na kwenda huko polisi makao makuu kuhusu hili halafu bidae kwenye vyombo vya habari??????????

Mkuu DARUSO yenyewe iko wapi wakati wametimuliwa? Jana kuna viongozi wa Ardhi University wamekamatwa wakati wapo kwenye mahojiano pale CHANNEL TEN (source taarifa ya habari ya saa moja, Channel 10)! Sasa unafikiri hawa wa udsm watakusanyana vipi katika hali hiyo?

Mi nafikiri independent people kama sisi ndio tuingilie kati kwenye suala hili, just we need good strategy!
 
Polisi wanapaswa kujua kuwa Mtatiro ni mtu mwenye asili ya mkoa wa Mara na hawa ni watu majasiri ambao wapo tayari kutetea haki zao kwa njia zozote zile , hivyo wasifikiri wataweza kumfanya asalimu amri za kipuuzi hata kama watamtesa sana .

Tuendelee kusema kwani nauona mwanga mbeleni na hatimaye Tanzania tunayoitaka itaweza kufikiwa soon ,

watakamata sana mwaka huu, na wakishindwa huenda wakaanza kutumia mbinu nyingine za elimination na pindi wakifikia hapo ndio utakuwa mwisho wa manyanyaso na dhuluma nchini mwetu......
 
hawa polisi wana akili nyingi sana......sijui mafunzo walipatia wapi maana wanajua kusoma alama za nyakati mnooooo. Anyway, huyu kijana atakuja kuwa kiongozi URT (may be Tanganyika) miaka ijayo. Mpeni salamu zangu.


mmmm....mama unachokonoa Muungano apo... hiyo tanganyika si nasikia ilishazikwa, ila mwenzio hakuzikwa?:confused:
 
Hivi kuna watu wamefanya ufisadi nchi hii, ambao umechochea watu kuichukia serekali yao, nao mbona wasishtakiwe kwa uchochezi?
 
Hii ni kesi nzuri sana kwani kwa mujibu wa historia nya Taifa letu ni kuwa mtu wa kwanza kushitakiwa kwa kosa kama hilo la uchochezi alikuwa ni Hayati baba wa Taifa Mwal.Nyerere ambaye alishitakiwa na wakoloni wa kiingereza akiwa yeye na watanganyika wenzake 3 kwa ajili ya kuupinga utawala wao , hivyo huyu kushitakiwa kwa kosa kama hilo ni sahihi kabisa kwani anashiriki kupinga utawala dhalimu ambao asababisha mateso makubwa kwa vijana wa kitanzania na wazazi wao ambao ni masikini sana.

Tuendelee kumtia moyo japokuwa simu yake bado imeshikiliwa na Polisi sijui wanatafuta huko kitu gani ama mawasiliano gani humo ndani .
 
Back
Top Bottom