Julius Mtatiro kushitakiwa kwa uchochezi

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Vyanzo vyangu ndani ya jeshi la Polisi vinaninong'oneza kuwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa TAHLISO Bw. Julius Mtatiro anashikiliwa na Polisi kwa madai ya kuhusika na mgomo wa wanafunzi wa elimu ya juu. Bw. Mtatiro (kwa mujibu wa vyanzo hivyo) amekuwa akihojiwa bila ya kuruhusiwa mwanasheria wake kuwepo na kwa muda wa zaidi ya masaa 24. Tangu jana ambako ka nzi kamekuwa kakifuatilia Bw. Mtatiro amekuwa akihamishwa kutoka kituo kimoja cha POlisi na hatimaye kurundikwa pale Msimbazi ambako Polisi wamekataa mtu yeyote kumuona..

Licha ya kumhoji inadaiwa mbinu za "kulazimisha" zimekuwa zikitumika dhidi yake..

Kama kuna Mwanasheria yeyote natoa wito ajaribu kufika Mzimbazi ili kumwakilisha kwani inaonekana kwa mara nyingine tena kijana huyo anajikuta yuko matatani hasa baada ya serikali pia kumnyima nafasi ya kuwa Mwalimu baada ya kukataa kumpatia kazi licha ya qualifications zote alizonazo na baada ya kuambiwa kuwa hatopatiwa kazi mahali popote Tanzania...

Free Julius Mtatiro NOW!! and Stop the Harrassment!
 
Last edited by a moderator:
Vyanzo vyangu ndani ya jeshi la Polisi vinaninong'oneza kuwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa TAHLISO Bw. Julius Mtatiro anashikiliwa na Polisi kwa madai ya kuhusika na mgomo wa wanafunzi wa elimu ya juu. Bw. Mtatiro (kwa mujibu wa vyanzo hivyo) amekuwa akihojiwa bila ya kuruhusiwa mwanasheria wake kuwepo na kwa muda wa zaidi ya masaa 24. Tangu jana ambako ka nzi kamekuwa kakifuatilia Bw. Mtatiro amekuwa akihamishwa kutoka kituo kimoja cha POlisi na hatimaye kurundikwa pale Msimbazi ambako Polisi wamekataa mtu yeyote kumuona..

Licha ya kumhoji inadaiwa mbinu za "kulazimisha" zimekuwa zikitumika dhidi yake..

Kama kuna Mwanasheria yeyote natoa wito ajaribu kufika Mzimbazi ili kumwakilisha kwani inaonekana kwa mara nyingine tena kijana huyo anajikuta yuko matatani hasa baada ya serikali pia kumnyima nafasi ya kuwa Mwalimu baada ya kukataa kumpatia kazi licha ya qualifications zote alizonazo na baada ya kuambiwa kuwa hatopatiwa kazi mahali popote Tanzania...

Free Julius Mtatiro NOW!! and Stop the Harrassment!

Ohooooooo! Mauji ya kisirsiri yanataka kuanza tena; nakumbuka miaka ya 1990 wakati wa Mzee Punch na migomo pale UDSM aliyekuwa Rais wa DARUSO somebody Matiku vyombo ya dola vilimfanyia hivyohivyo na baada ya kufukuzwa Chuo haikupita muda mrefu tulisikia kuwa amekufa kwa kujinyonga huko kwao Mara. God forbid yasijirudie hayo.

Sasa kule DUCE na Mkwawa nao watakamatwa? Kainzi hakajatua huko?
 
Naomba anayefahamu walipo vijana hawa, Katibu Mkuu wa Umoja wa marais wa Taasisi za Elimu ya Juu nchini (TAHLISO), Mtatiro Julius na Odwang Odong.

Kuna taarifa kwamba wamekamatwa na wanausalama tokea Jumamosi na hawajulikani wako katika kituo gani ama kama wako salama, yeyote anayejua usalama wao aseme.
 
HATUSHANGAI kwani mlipowapigia debe hawa jamaa, nyie waandishi wa habari ukiwemo wewe mwanakijiji hamkujua wanaolilia sana au kutokwa na udenda sana kwa tamaa ya kitu huwa hawawezi.

Na wakishindwa hugeuka mbogo na kuanza kuonesha makucha yao ya udikteta na police state? Haya sasa wafichueni. Kugoma kwani dhambi. Kama mambo hayaendi wanataka tufantye nini? Au wanataka tuwaambie kaka zetu waturudishe kulekule mwaka 1964?
 
Waandishi waalimu wanafunzi mapolisi majeshi mahakimu na majaji wacha ya wakute haya au hizi ndizo ahadi za CCM hakuna jingine ,japo wengine hawamo lakini idadi kubwa ni wapigia debe CCM,ndio wapiga kura wa CCM baba yao ni ccm maana huwaga nawasikia wakisema CCM ndio baba.
Sijui kama watu hubadilika na kama wamisikia kuwa Wamerakani wamempigia na kumpa ushindi wa kishindo Mwafrika Baraka huseini Obama Onyango, hapa watu ukiwambia wabadilishe Chama wao wanabadilisha mtu kwa kuwa tu CCM ndio baba ,mambo badu kwa hali ya uchumi inavyokwenda mambu yatakuwa mengi si hasha Muungwana akaingia mitini uchaguzi ujao.
 
Utawala wa kiimla unaogopa sana mwamko wa wanafunzi wa elimu ya juu! Unajua hawa jamaa kama wangeweza kumkamata kile mtu anayewapinga na isijulikane wangekamata kila mtu; tusipoangalia tutaanza kuokota miili in reminiscent of Idi Amin Dada...
 
Kazi ipo sasa...maana wakimaliza hapo watahamia kwa Mkoba wa Chama cha Walimu...........
 
nadhani wakati umefika wa kuitisha maandamano makubwa zaidi ya wanafunzi wote na kukomesha mara moja unyanyasaji huu; maana inaonekana punda hendi bila ya fimbo!
 
Utawala wa kiimla hautakubalika Tanzania, na kwa maoni yangu Serikali ya JK inaanza kuelekea huko. Watanzania naamini wako makini sana katika hilo. Wanafunzi wanadai haki yao, leo hii unawakamata wawakilishi wao. Hii haiwezi kuleta tija katika migomo zaidi ya kuongeza chuki kwa serikali. Kuna thread moja nilichangia kuhusu mgomo wa walimu kuwa Bw. Chiligati anaielekeza serikali kumfikisha Bw. Mukoba (Rais wa CWT). Kisa, mgomo. Hawa watu ni wawakilishi wa victims ambao ni wanafunzi wa vyuo vikuu pamoja na walimu nchini. Sasa kuwakamata au kuwafungulia mashitaka ndiyo ita-solve matatizo hayo!! Serikali pamoja na Rais JK wanatakiwa kuwa serious na matatizo yanayowakabili wananchi. Leo hii wanafunzi wa vyuo vikuu, walimu wana mgomo ili kudai haki zao. Siku zijazo wananchi wengine nao wataleta vuguvungu la kudai haki zao za maendeleo katika maeneo yao kama vile maji, umeme, madawa hospitalini n.k

Serikali inatakiwa kuacha mambo ya kijanjajanja na kuwa serious na matatizo ya wananchi. Hawa watu wananoshikiliwa na wana usalama wanatakiwa kuachiwa huru mara moja bila ya vikwazo vyovyote. Tanzania haiwezi kuwa salama kwa kutumia vitisho kuwafunga wananchi midomo kudai haki zao. Mwaka huu na kuendelea lazima kuwe na mabadiliko makubwa katika maendeleo ya wananchi na si danganya toto kama ya Msekwa kudai oooh JK kafanya kazi nzuri kwa wananchi. Bull@@<*%t.
 
Kazi ipo sasa...maana wakimaliza hapo watahamia kwa Mkoba wa Chama cha Walimu...........

Kuna hatari ya hawa vijana kufikishwa mahakamani kesho chini ya ulinzi mkali, huku jamaa wa EPA wakila kuku kwa mrija, wengine wakiwa wamekwenda kujiliwaza nje ya nchi, mmoja akiwa Marekani na mwingine nchi za Ghuba..... Tutaendelea kuzugwa hadi tongo tongo zitutoke tuache kushabikia kila kitu
 
Kuna hatari ya hawa vijana kufikishwa mahakamani kesho chini ya ulinzi mkali, huku jamaa wa EPA wakila kuku kwa mrija, wengine wakiwa wamekwenda kujiliwaza nje ya nchi, mmoja akiwa Marekani na mwingine nchi za Ghuba..... Tutaendelea kuzugwa hadi tongo tongo zitutoke tuache kushabikia kila kitu

Tusubiri hayo mashtaka kwani hii issue inaelekea ni deeper than this migomo stuff.
Naona issue hii inaweza kuwa coincedence mbaya kwasababu EPA nayo iko makahamani...Haya mambo ya siasa huwa yanageuka ghafla ghafla mno na si ajabu moshi unafuka kwani moto hauko mbali.

Sasa wanafunzi wote Tanzania nzima wakigoma nani atanufaika?
Ama wandhani vijana hao wanataka kupinduwa nchi? Wanausalama kuwanyanyasa wasomi wetu kwa kisingizio cha kuwa wao ni upinzani hakina maana kabisa....Wapewe haki zao na wanafunzi waandamane EPA iwape na ufisadi mwingine ushughulikiwe kwanza ili wanafunzi hao wapate huduma na elimu bora badala ya mafisadi kujiendeleza wao wenyewe.
 
Ndio maana hadi sasa miye sijasema lolote kuhusu watu wa EPA kufikishwa mahakamani.. kwani mazingaombwe siyo lazima kuficha kila kitu wakati mwingine ni kufanya vitu vionekane hadharani!
 
Kwani hiyo pesa ya EPA si ingetosha mara mia kuyashughulikia matatizo sugu ya wanafunzi? Matatizo ya wanafunzi hayajaanza leo..Lakini kwasababu na wao wana upeo...Wanajuwa wazi kuwa viongozi wetu wanakotupeleka siko, Ufisadi uliofanyika hakuna hata jambo moja lilikuwa solved na matatizo ndiyo yanazidi kuongezeka kwasababu wao mafisadi si ndio walianzisha kwa kupeleka siasa badala ya kutatuwa matatizo yao?
Yamewakuta sasa na mimi naungana na wanafunzi hao kudai haki za msingi na kuupiga vita ufisadi kwa nguvu zote na nawaombea Mungu awalinde na ubaradhuli wa mafisadi hao hatari kabisa kwa jamii na usalama wake.
 
Kubalini tu yaishe.. madaraka ni matamu sana na sasa hivi migomo yanatishia madaraka ya watu... so tuna uamuzi wa kufanya.
 
kuna habari nimepata hivi punde kwamba wanafunzi wa Primary/Secondary nao wamegoma leo Dar ili kushinikiza serikali kuwaachia Je ni kweli???????
 
Back
Top Bottom