Julius mtatiro aeleza kinachomkera cuf

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Julius Mtatiro amefanya mahojiano na gazeti la Mwanahalisi na kusema kinachomkera na kumuumiza roho ni dhana iliyojengeka kwamba CUF ni chama cha Kiislamu.Amepinga vikali dhana hiyo na kusema hakuna upendeleo wowote wa kidini ndani ya CUF na ndio maana yeye Mkristo akapewa nafasi ya Naibu Katibu Mkuu.Amesema ataanzisha moto nchi nzima kudai katiba mpya na kufuta hiyo dhana ya udini dhidi ya chama chake.Amesema atahakikisha ule umaarufu wa kale wa CUF utarudi na chama chake kitavipiku vyama vyote hapa nchini.
Wadau imekaaje hii? Kweli Julius Mtatiro ataweza kufuta dhana hii....................
 
Kaza buti mtatiro, hiyo dhana tu wala siyo issue...waache waislamu waje kwa wingi CUF hata walioko huko CCM then itakula kwao, zana hiyo ipo hata kwa Chadema kwamba ni wakristu tena catholics, who cares? twende tudai katiba mpya. tuko pamoja.
 
Mtatiro wazo lako nizuri sana lakini huna uwezo wa kugeuza misingi iliyo ijenga CUF........na huna uwezo wa kuijenga CUF na kuwa maarufu kama unavyo nadi ushauri wangu ondoka CUF mapema kabisa kajiunge na kafulila NCCR mwaka 2015 uta weza kubahatika kupata ubunge sio huko uliko. Na usijaribu kuja CDM kwasababu tumesha acha kupokea mamluki shibuda anatutosha
 
Mtatiro wazo lako nizuri sana lakini huna uwezo wa kugeuza misingi iliyo ijenga CUF........na huna uwezo wa kuijenga CUF na kuwa maarufu kama unavyo nadi ushauri wangu ondoka CUF mapema kabisa kajiunge na kafulila NCCR mwaka 2015 uta weza kubahatika kupata ubunge sio huko uliko. Na usijaribu kuja CDM kwasababu tumesha acha kupokea mamluki shibuda anatutosha

Huwezi kumshauri mtu makini atoke kwenye chama makini aende kwenye shauri yako!

CDM mmeacha kupokea mamluki sijakusoma? wewe una cheo gani huko cdm?

cdm hiyo sera ya ubaguzi ilianza lini?
 
Yahaya
unamtaja zitto hivi zitto ndio nani mbona simkumbuki vizuri ....... alisha wahi kuwa maarufu hapa nchini? na umaarufu wake ulipoteaje mpaka nikawa na msahau namna hiii....
 
Hii inatufunza kuanzia sasa kwamba tuache kuitambua CUF kama chama cha waislamu na chadema kama chama cha wakristo. sisi hapa JF ni sehemu ya watanzania hivyo tunaweza kuanza kuamsha moto wa kukataa kupandikiza mbegu za kidini kisha mbegu ya kukataa udini ikachipua na kumfikia mtu mmoja mmoja katika jamii.
 
Tropical
Mimi nimpiga kura na kura yangu pale CDM inanguvu sana kwasababu haichakachuliwi kama zinavyo fanywa na tume ya taifa ya uchaguzi....au mwenzangu unadhani mpiga kura nimtu mdogo sana.....nakuwa sikuelewi vile unacho taka kusema au unamaanisha CDM wanamfumo wa zidumu fikra za mwenyekiti...Halafu unasema CDM hawana sera ya ubaguzi hivi ni ubaguzi gani umezungumzwa na kereng'ende? au una shindwa kuelewa tofauti ya kubagua na kukataa? sisi hatutaki watu wasio eleweka katika mitazamo na itikadi zao na hatuelewi wanaamini nini juu ya mstakabali wanchi hii.Nimemsikia maranyingi Mtatilo akizungumzia suala la katiba kama sera ya CUF,sasa mwenzangu mtu kama huyu unamwelewa vizuri? CDM sisi hiyo sio sera ni jukumu la watanzania wote na CCM wakiwemo sisi tuna hamasisha na kuona jambo hili lina tekelezeka kwa nguvu ya uma sio kutenga watu eti hii sio hoja /sera yao kama anavyo fanya mtatilo na kutoa reference eti alianzisha lipumba mpaka police wakamvunja mkono so? ndio maana nimemwambia aende kwakafulia akatafute ubunge
 
Hii inatufunza kuanzia sasa kwamba tuache kuitambua CUF kama chama cha waislamu na chadema kama chama cha wakristo. sisi hapa JF ni sehemu ya watanzania hivyo tunaweza kuanza kuamsha moto wa kukataa kupandikiza mbegu za kidini kisha mbegu ya kukataa udini ikachipua na kumfikia mtu mmoja mmoja katika jamii.

Mimi nashauri hivyo vyama vijipambanue kuwa wanatetea maslahi ya wananchi period!

vikjengwa kwa misingi ya kidini ndio nzuri zaidi...

christian party vs. Islamic party kama wanatetea maslahi ya nchi na wanacnhi wake wote who cares? i don't?
 
Hiyo dhana haiwezi toka ,mfano we angalia cuf kipo hasa maeneo gani? Ni maenel ambayo ni waisalamu wengi kwa bara ni ukanda wa pwani tanga ,kilwa,lindi,zanzabar
 
Tatizo la CUF ni wanachama wengi wanaokwenda kwenye mikutano yao, kuvaa kanzu na balaghashia kwa akina baba na hijabu kwa akina mama. Vinginevyo ni chama cha kawaida na hakija elemea kwenye dini yeyote. Ndio maana kina viongozi kama akina Wilfred Rwakatare, Julius Mtatiro nk ambao hakuna hata mmoja aliyelalamikia udini katika chama hicho.
Ni mtazamo tu wa watu walio nje ya chama ambao hujenga picha ya kanzu na hijabu, nakumalizia kuzipeleka msikitini, yaani kwenye Uislam. Kiukweli hakuna uhusiano kati ya CUF na Uislam. Ingawa kwenye algebra wanakuwa sahihi kabisa, hasa ukiangalia mlinganyo huu. Kama A=B,na B=C,basi A=C. (A=Uislam;B=Hijabu na kanzu; C=CUF).
 
Tropical
Mimi nimpiga kura na kura yangu pale CDM inanguvu sana kwasababu haichakachuliwi kama zinavyo fanywa na tume ya taifa ya uchaguzi....au mwenzangu unadhani mpiga kura nimtu mdogo sana.....nakuwa sikuelewi vile unacho taka kusema au unamaanisha CDM wanamfumo wa zidumu fikra za mwenyekiti...Halafu unasema CDM hawana sera ya ubaguzi hivi ni ubaguzi gani umezungumzwa na kereng'ende? au una shindwa kuelewa tofauti ya kubagua na kukataa? sisi hatutaki watu wasio eleweka katika mitazamo na itikadi zao na hatuelewi wanaamini nini juu ya mstakabali wanchi hii.Nimemsikia maranyingi Mtatilo akizungumzia suala la katiba kama sera ya CUF,sasa mwenzangu mtu kama huyu unamwelewa vizuri? CDM sisi hiyo sio sera ni jukumu la watanzania wote na CCM wakiwemo sisi tuna hamasisha na kuona jambo hili lina tekelezeka kwa nguvu ya uma sio kutenga watu eti hii sio hoja /sera yao kama anavyo fanya mtatilo na kutoa reference eti alianzisha lipumba mpaka police wakamvunja mkono so? ndio maana nimemwambia aende kwakafulia akatafute ubunge

Nimekusoma asante,
chama cha siasa hakina uwezo wa kukataa kupokea watu (call them mamluki or whetever), mtu kama wewe ambaye unahisi wenzako ni mamluki inawezekana wewe ni mamluki bila kufahamu!

Mtatiro ni kijana mdogo sana mwenye poiltical career nzuri hapo CUF unamshauri atoke kweye chama makini aende nccr hivi kweli wewe unapenda mageuzi au ndio wale die hard cdm, ambao wanafikiri vyama vingine ni feki..pole sana

watu wote makini tunaungana na kauli ya mtatiro, tatizo naloliona ni kwamba badala kuongelea udini angewasha moto, kuongelea udini ni kupalilia na siyo kuufuta..

Natamani waislamu wote wa CUF and Wakristo wote wa chadema hapo tumeiangusha CCM period!
 
Mtatiro asijisumbue kamwe. Cuf ni uislam na uislam ni cuf. Hiyo haina ubishi. Angalia kwenye mikutano ya hadhara ya cuf uone 'vibandiko' na hijab. Ni mtindo mmoja tu.
 
Mtatiro asijisumbue kamwe. Cuf ni uislam na uislam ni cuf. Hiyo haina ubishi. Angalia kwenye mikutano ya hadhara ya cuf uone 'vibandiko' na hijab. Ni mtindo mmoja tu.

Sijakupata
"Unasema Slaa asijisumbue kamwe. Chadema ni Ukristo na Ukristo ni Chadema. Hiyo haina ubishi. Angalia kwenye mikutano ya hadhara ya Chadema uone vichwa wazi na vimini. Ni mtindo mmoja tu.

wabongo wana akili sana..wengi wao wana akili kama zako..wanapenda kujudge kitu kwa nje bila kusoma ..wavivu..gosbert ni moja katika hao.
 
Tatizo la CUF ni wanachama wengi wanaokwenda kwenye mikutano yao, kuvaa kanzu na balaghashia kwa akina baba na hijabu kwa akina mama. Vinginevyo ni chama cha kawaida na hakija elemea kwenye dini yeyote. Ndio maana kina viongozi kama akina Wilfred Rwakatare, Julius Mtatiro nk ambao hakuna hata mmoja aliyelalamikia udini katika chama hicho.
Ni mtazamo tu wa watu walio nje ya chama ambao hujenga picha ya kanzu na hijabu, nakumalizia kuzipeleka msikitini, yaani kwenye Uislam. Kiukweli hakuna uhusiano kati ya CUF na Uislam. Ingawa kwenye algebra wanakuwa sahihi kabisa, hasa ukiangalia mlinganyo huu. Kama A=B,na B=C,basi A=C. (A=Uislam;B=Hijabu na kanzu; C=CUF).
Hivi Wilfred Rwakatare bado ni kiongozi wa CUF?
 
Topical
Rwakatere yuko wapi? Maharagande yuko wapi? hiyo nimifano tu .....nadhani humpendi mtatilo, suala la katiba bado huja mwelewa mtatilo analichukulia kirahisi sana na kudhani ni sera ya CUF na wao ndio wataleta mabadiliko ya katiba na sio watanzania hicho ndicho kinachonifanya nimwone kwa taswira isio eleweka katika mstakabali wa nchi hii juu ya suala hili anadiliki kuiponda CDM kuwa hiyo sio hoja yao? hii inamaanisha nini kama sio utani suala la kushirikisha wananchi wote wewe unataka kulibeba na chama chenye wabunge watatu bara? huna sababu ya kuniambia mimi ni mamluki katika hili vinginevyo mshauri taswira yake juu ya jambo hili asionekane hivyo ambavyo anaonekana.kwauchemvu huo hawezi kuwa asset CDM ....abaki huko huko na njaa au akatafute ubunge kupitia NCCR........
 
Kwakweli mjada umekua mzito mpaka watu wana-intergrate. Naweza sema Zito amekuala pesa za mafisadi, Anahama na juzi Kanunua
Horse Spot, na mambo mengine mengi tu kafanyiwa na CCM-mafisadi. Hana issue tena kisiasa na ameanza kufilisika kisiasa. Kwakweli mtatiro inatakiwa ahamie
 
Back
Top Bottom