Jukwaa la Wahariri lamfungia Mkuchika; latoa ripoti ya Tarime

FM, mzee umechanganya mambo mawili. Jukwaa la Wahariri linaongozwa na Datoo. Jukwaa hiloliliunda tume baada ya mazishi ya Wangwe iliyoongozwa na Kubenea. Hii ilikuwa kabla ya kasheshe la Mkuchika. HIvyo katika mkutano wao wa leo Jukwaa lilitoa uamuzi na ile tume (iliyoongozwa na Kubenea) na iliyomaliza ripoti yake kabla ya toleo la wiki iliyopita ilikuwa inatoa ripoti yake leo pia.

Ila ni kwa kiasi gani Kubenea alishiriki katika kuinfluence maamuzi dhidi ya Mkuchika sina uhakika. Nakubaliana na wewe angetakiwa kurecuse.

MKJJ. Asante kwa ufafanuzi. Ilibidi hawa wahariri waweke bayana kuwa huu uamuzi umetokana na ripoti ya tume iliyoundwa na kuwasilishwa kabla ya tukio la hivi karibuni. Bila hivyo, kweli wengi wetu tutaiuunganisha kimakosa na kasheshe ya hivi karibuni. Kuondoa mzizi wa fitina, ingekuwa vizuri zaidi kama hiyo ripoti ingewekwa wazi kwa umma. Waibandike humu, tujisomee.
 
Kaka kama hujui ukweli wa mambo no bora ukaacha uzandiki wako. Hujui hali iliyomfanya SAKINA aondoke SUNDAY CITIZEN.....

Kuhusu kufanya nachotaka MENGI huo ni uzandiki mwingine. Umewahi kuona mkataba wa SAKINA na IPP MEDIA? Kama wewe una tabia ya kuburuzwa na mwajiri wako usidhani kuwa kila mtu ni legelege kama wewe....

Natumai huyu sio PASCHAL MAYALA yule rebel ninayemuheshimu....

Tanzanianjema

Asante Tanzania njema.
1. Pasco na Paschal Mayala are two diferent entities.
Pasco mimi ni mwana JF wa kawaida. Paschal Mayalla
ni mwanahabari/mtangazaji nilisikia alipataga ajali
mbaya na hajapona.
2. Its a comon sense ukisikia mtu ameshift from one media to another tunaamin its in search of greener pasture. Kutojua kilimuhamisha Sakina toka the citizen ndio uzandiki?.
3. Nimesema ' He who pays the Pipper may call the tune' je ni siri ni Mhe. Mengi anamlipa Sakina mshahara?.
Sio yeye anafadhili Jukwaa la Wahariri?. Ama ni siri
yeye ndiye MOAT? Mambo ya kuuona mkataba wa
Sakina na IPP yametokea wapi? Nijuavyo mimi mikataba yote ni siri, hata wewe huna jeuri ya kuuona huo mkataba unless otherwise. Nilichosema Sakina is priceless no one can buy her nikauliza sijui kilimsibu nini!.
4. Hili la kuburuzwa na mwajiri wangu na mimi kuwa legelege limetoka wapi?.

Namalizia kwa kukushukuru kwa kumuheshimu Paschal Mayalla ambaye hata mimi nilimuheshimu sana enzi zake za Kiti Moto na sijui kilifia wapi?.
 
kufungia kuandika habari za mkuchika naona itakuwa ngumu kama ilivyokuwa za mkuu wa mkoa wa morogoro said kalembo hivi karibuni
 
Hebu angalia aibu hii Waandishi wanapotumika na Mafisadi kuilipua Tanzania!
Mwandishi alipotosha umma mazishi ya Wangwe

2008-10-15 10:32:48
Na Muhibu Said


Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, wamepitisha maamuzi kwamba, mwandishi wa habari wa kujitegemea mkoani Mara, George Marato, alikiuka maadili ya taaluma ya uandishi wa habari kwa kuandika habari potofu kuhusu msiba wa aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Marehemu Chacha Wangwe.

Walipendekeza kwamba vyombo anavyoandikia habari Marato vichukue tahadhari katika kupokea habari zake, kwa sababu uchunguzi wa kamati ya wahariri iliyoundwa kuchunguza malalamiko ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) juu ya habari zilizodaiwa kuandikwa na magazeti manne, umegundua dosari kubwa katika habari alizoandika Marato.

Wahariri wamethibitsiha kwamba Marato alipotosha hali halisi ilivyokuwa kijijini Kemakorere wakati mazishi ya Wangwe, yalipoahirishwa Julai 31, mwaka huu.

Uamuzi huo ulifikiwa na wahariri hao baada ya kupokea ripoti ya kamati ya hiari ya wahariri ya kuchunguza habari zilizolalamikiwa na Chadema kwamba magazeti kadhaa yaliandika habari za kupotosha kwamba Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe, aliondoshwa msibani na polisi kwa kuwa kulikuwa na watu waliokuwa na mapanga wakitaka kumuua.

Habari hizo ziliandikwa kwenye magazeti ya Nipashe, Uhuru, Kulikoni na Majira, zikieleza kwamba Mbowe aliondoshwa na polisi kwa sababu maisha yake yalikuwa hatarini.

Wahariri hao walisema kwamba habari za magazeti hayo zimethibitika kuandikwa na mwandishi mmoja, Marato, baada ya yeye mwenyewe kuithibitishia kamati hiyo kwamba ndiye aliyeziandika.

Pia, wameamua kuandaa malalamiko dhidi ya Klabu ya Waandishi wa Habari mkoani Mara kwa madai ya kukebehi na kujaribu kufifisha kazi ya Kamati ya Hiari ya Wahariri iliyochunguza habari zilizoandikwa na baadhi ya magazeti juu ya kuahirishwa kwa mazishi hayo.

Maamuzi hayo yalipitishwa na wahariri hao baada ya kamati hiyo kusoma ripoti yake ya uchunguzi wa habari za msiba wa Wangwe, katika kikao kilichofanyika katika Hoteli ya New Africa, jijini Dar es Salaam jana. Kikao hicho kiliandaliwa na Jukwaa la Wahariri na kuongozwa na Mwenyekiti wake, Sakina Datoo.

Awali, akisoma ripoti hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Saed Kubenea, alisema Marato alipotosha ukweli kuhusu suala hilo kwa kuandika kwenye magazeti manne ya kila siku yanayotolewa kwa lugha ya Kiswahili kwamba, Mbowe alinusurika kuuawa.

Kubenea alisema katika habari iliyoripotiwa na Marato, ilieleza kuwa katika vurugu hizo, vijana waliobeba silaha walitaka kumdhuru Mbowe, ambaye polisi walimwondoa katika eneo hilo kunusuru maisha yake kutokana na hasira ya umati wa vijana hao.

Alisema upotoshaji wa habari hiyo ulilalamikiwa na Chadema kupitia Naibu Katibu Mkuu wake, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, ambaye aliwasilisha malalamiko rasmi kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Sakina Datoo.

Kubenea alisema katika uchunguzi wake, kamati ilibaini kwamba, ni kweli vurugu zilitokea katika msiba wa Wangwe, lakini hazikumlenga Mbowe, bali zilikuwa na mlolongo mrefu wa maslahi binafsi na malalamiko ya muda mrefu, ambayo hayajafanyiwa kazi katika wilaya ya Tarime.

SOURCE: Nipashe
 
Hebu angalia aibu hii Waandishi wanapotumika na Mafisadi kuilipua Tanzania!
Mwandishi alipotosha umma mazishi ya Wangwe

2008-10-15 10:32:48
Na Muhibu Said


Wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, wamepitisha maamuzi kwamba, mwandishi wa habari wa kujitegemea mkoani Mara, George Marato, alikiuka maadili ya taaluma ya uandishi wa habari kwa kuandika habari potofu kuhusu msiba wa aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Marehemu Chacha Wangwe.

Walipendekeza kwamba vyombo anavyoandikia habari Marato vichukue tahadhari katika kupokea habari zake, kwa sababu uchunguzi wa kamati ya wahariri iliyoundwa kuchunguza malalamiko ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) juu ya habari zilizodaiwa kuandikwa na magazeti manne, umegundua dosari kubwa katika habari alizoandika Marato.

Wahariri wamethibitsiha kwamba Marato alipotosha hali halisi ilivyokuwa kijijini Kemakorere wakati mazishi ya Wangwe, yalipoahirishwa Julai 31, mwaka huu.

Uamuzi huo ulifikiwa na wahariri hao baada ya kupokea ripoti ya kamati ya hiari ya wahariri ya kuchunguza habari zilizolalamikiwa na Chadema kwamba magazeti kadhaa yaliandika habari za kupotosha kwamba Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe, aliondoshwa msibani na polisi kwa kuwa kulikuwa na watu waliokuwa na mapanga wakitaka kumuua.

Habari hizo ziliandikwa kwenye magazeti ya Nipashe, Uhuru, Kulikoni na Majira, zikieleza kwamba Mbowe aliondoshwa na polisi kwa sababu maisha yake yalikuwa hatarini.

Wahariri hao walisema kwamba habari za magazeti hayo zimethibitika kuandikwa na mwandishi mmoja, Marato, baada ya yeye mwenyewe kuithibitishia kamati hiyo kwamba ndiye aliyeziandika.

Pia, wameamua kuandaa malalamiko dhidi ya Klabu ya Waandishi wa Habari mkoani Mara kwa madai ya kukebehi na kujaribu kufifisha kazi ya Kamati ya Hiari ya Wahariri iliyochunguza habari zilizoandikwa na baadhi ya magazeti juu ya kuahirishwa kwa mazishi hayo.

Maamuzi hayo yalipitishwa na wahariri hao baada ya kamati hiyo kusoma ripoti yake ya uchunguzi wa habari za msiba wa Wangwe, katika kikao kilichofanyika katika Hoteli ya New Africa, jijini Dar es Salaam jana. Kikao hicho kiliandaliwa na Jukwaa la Wahariri na kuongozwa na Mwenyekiti wake, Sakina Datoo.

Awali, akisoma ripoti hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Saed Kubenea, alisema Marato alipotosha ukweli kuhusu suala hilo kwa kuandika kwenye magazeti manne ya kila siku yanayotolewa kwa lugha ya Kiswahili kwamba, Mbowe alinusurika kuuawa.

Kubenea alisema katika habari iliyoripotiwa na Marato, ilieleza kuwa katika vurugu hizo, vijana waliobeba silaha walitaka kumdhuru Mbowe, ambaye polisi walimwondoa katika eneo hilo kunusuru maisha yake kutokana na hasira ya umati wa vijana hao.

Alisema upotoshaji wa habari hiyo ulilalamikiwa na Chadema kupitia Naibu Katibu Mkuu wake, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, ambaye aliwasilisha malalamiko rasmi kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Sakina Datoo.

Kubenea alisema katika uchunguzi wake, kamati ilibaini kwamba, ni kweli vurugu zilitokea katika msiba wa Wangwe, lakini hazikumlenga Mbowe, bali zilikuwa na mlolongo mrefu wa maslahi binafsi na malalamiko ya muda mrefu, ambayo hayajafanyiwa kazi katika wilaya ya Tarime.

SOURCE: Nipashe
Kwa nini hakuhudhuria mazishi?hawa wahariri ndo wanapotosha jamii!
 
Kwa mtu makini lazima alijua kabisa kuwa habari ile ilipikwa. Tunashukuru wanatarime kwa kuwakata ngebe mafisadi waliomtumia Marato kwa kumuandalia Mbowe mapokezi yaliyovunja rekodi huko Tarime pamoja na kulirudisha tena jimbo mikononi mwa wanyonge

Tunaishukuru pia ITV kwa kumtimua Marato kwa sababu ni mtu hatari ambaye alitaka kutumia taaluma yake kusababisha maafa

Kushindwa kwa CCM tarime ni bao lingine la kisigino kwa mafisadi waliokuwa wanatumia kifo cha wangwe kuzima juhudi za CHADEMA na wananchi wengine wenye uchungu na nchi yao katika kutetea maslahi ya wanyonge

Kweli huu ni mwaka wa Shetani kwa mafisadi na vibaraka wao akina Mtikila
 
Du,,, kali
Na sasa tusubiri tuone George Marato anachukuliwa hatua gani za kinidhamu kwa hili. Kupotosha Uma kwa kuandika habari ambazo si za kweli ni kutaka kuibua jambo fulani. Je alinunuliwa na mtu aandike hayo aliyoyaandika ama ni kwa interest ya nani.
 
Du,,, kali
Na sasa tusubiri tuone George Marato anachukuliwa hatua gani za kinidhamu kwa hili. Kupotosha Uma kwa kuandika habari ambazo si za kweli ni kutaka kuibua jambo fulani. Je alinunuliwa na mtu aandike hayo aliyoyaandika ama ni kwa interest ya nani.

hatua ya kwanza ITV wameshasimamisha kuchukua habari zake...
 
CCM balaaa mmemponza Mtikila akapigwa mawe,
Mmemponza George Marato kibarua kimeota nyasi kwa kutudanganya.
Mme mnunua Rais wa CWT jana kapigwa mawe na walimu....
Who is next..................
Njama zenu za kununua watu wadanganyika wamesha washtukia,...kazi mnayo na miti sasa isha anza kuteleza.
 
Mkuchika aache kuhangaika na kufungia magazeti.

Gazeti likidai kitu kibaya juu ya mtu hiyo kesi inajulikana kama ya madai.

Waliokuwa wanatakiwa wahangaike na Gazeti ni wale waliodhurika kwa hayo madai ambao ni mtoto wa Kikwete na wale waliotajwa kwenye hiyo makala ndio walipaswa wachukue hatua dhidi ya gazeti hilo kwa taratibu za kimahakama.Huko ndiko kuheshimu utawala wa Sheria.

Kitendo cha Mkuchika kukurupuka na hamasa za kisiasa kufungia gazeti ni uvunjaji wa haki za binadamu na sheria.Sheria zipo.Angeachia gazeti na waliokashifiana wamalizane wenyewe kwa kutumia sheria na mahakama zilizopo na kama kesi hiyo ingefikishwa mahakamani na gazeti likaonekana lina hatia hapo ndipo waziri Mkuchika angekuwa na nguvu hata uhalali wa kulifungia badala ya yeye kukurupuka na kufungia gazeti kwa hukumu za mezani zilizojaa jazba na kujikomba kisiasa.

Mkuchika kulifungia gazeti ina maana anasimama kwa niaba ya Mtoto wa Kikwete Nchimbi na wengineo? Kwa nini wao wasiende mahakamani kama wao wanaona hawakutendewa haki na gazeti?

Mkuchika ajifunze kuheshimu utawala wa sheria ili asiitumbukize nchi kuangukia kwenye kundi lisiloheshimu haki za binadamu bila sababu.

Raisi Kikwete ni vizuri amwondoe Mkuchika sababu hafahamu vizuri utawala wa sheria na hajui mipaka ya lini atetee serikali na lini asitetee watu binafsi kama mtoto wa Kikwete na akina Nchimbi wanaposemwa vibaya na magazeti iwe kihalali au siyo kihalali.

Mkuchika anaonyesha kabisa hajui mipaka yake kama waziri wa habari inaanzia wapi na kuishia wapi?

Jukwaa la wahariri lina haki kumsusia mtu kama Mkuchika..
 
Nina wasiwsi mkubwa na hii tume pamoja na matokeo ya utafiti wao. Kwanza; tuliona kwenye televisheni vurugu na Mbowe na wengine wakisaidiwa kuingia kwenye magari ya polisi. Sijui hili wanakana namna gani. Pili magazeti mengi (na si Nipashe na Majira ambayo George Maratu anayaandikia kama correspondent) yaliandika habari hii juu ya vurugu hiyo kutoka katika vyanzo mbali mbali. Haiingii akilini kuwa mtu mmoja (George Marato) aliweza ku`influence' habari za magazeti yote na haiingii akilini kuwa waandishi wengine waliokuwepo walimwacha afanye hivyo na kushindwa kutuma habari tofauti. Tatu, mbunge Shelukindo ambaye aliongoza kamati ya bunge kwa mazishi alisema bungeni kulikuwa na vurugu kiasi cha wao kushindwa kutoa ubani/salamu za bunge. Nne ni jadi ya watu wa Tarime kutembea na silaha za jadi na kwa ajili ya hilo haiingii akilini kuwa siku hiyo ya mazishi hawakuzibeba.
Hizi ni sababu zinazonifanya nitilie mashaka tume ya waandishi iliyo chini ya Jukwaa la Wahariri. Vile vile sijaona sababu za kutotoa ripoti hii kabla ya uchaguzi.
 
Ndugu zangu, nafikiri tunahitaji kutafakari kwa kina ripoti ya tume ya waandishi. Nina mashaka kama ripoti hii ndio inaelezea ukweli wa mambo yaliyotokea kwenye mazishi ya Mh. Wangwe. nakumbuka vyombo vyote vyote vya habari vilitangaza kuwako kwa vurugu na sio magazeti haya machache ya Kiswahili ambayo George Marato ameyaandikia. Magazeti haya yalikuwa na vyanzo vingine tofauti kama Mkuu wa Polisi wa Mkoa ambaye alithibitisha kuwako kwa hali hiyo. Kwa kuongezea tu Daily News iliwaquote wageni kutoka Kenya ambao nao walithibitisha kulikuwa na vurugu. Pili, tuliona kwenye television hali hiyo na sishawishiki kama ile nayo ilitengenezwa. Na jambo la tatu Mheshimiwa Shelukindo alisema bungeni kuhusu vurugu zile. Kama nitakumbuka vizuri Mh Shelukindo aliongoza kamati fulani ya bunge kwenye mazishi.
Nashauri tutafakari zaidi kabla ya kuichukua ripoti ya tume ya waandishi na kumuhukumu George Marato.
 
Ndugu zangu, nafikiri tunahitaji kutafakari kwa kina ripoti ya tume ya waandishi. Nina mashaka kama ripoti hii ndio inaelezea ukweli wa mambo yaliyotokea kwenye mazishi ya Mh. Wangwe. nakumbuka vyombo vyote vyote vya habari vilitangaza kuwako kwa vurugu na sio magazeti haya machache ya Kiswahili ambayo George Marato ameyaandikia. Magazeti haya yalikuwa na vyanzo vingine tofauti kama Mkuu wa Polisi wa Mkoa ambaye alithibitisha kuwako kwa hali hiyo. Kwa kuongezea tu Daily News iliwaquote wageni kutoka Kenya ambao nao walithibitisha kulikuwa na vurugu. Pili, tuliona kwenye television hali hiyo na sishawishiki kama ile nayo ilitengenezwa. Na jambo la tatu Mheshimiwa Shelukindo alisema bungeni kuhusu vurugu zile. Kama nitakumbuka vizuri Mh Shelukindo aliongoza kamati fulani ya bunge kwenye mazishi.
Nashauri tutafakari zaidi kabla ya kuichukua ripoti ya tume ya waandishi na kumuhukumu George Marato.

Naona mkuu hujasoma vizuri ripoti hiyo, ripoti inasema vurugu zilikuwepo lakini hazikumlenga Mbowe kama taarifa za Marato zilivyosema
 
...............Kubenea alisema katika uchunguzi wake, kamati ilibaini kwamba, ni kweli vurugu zilitokea katika msiba wa Wangwe, lakini hazikumlenga Mbowe, bali zilikuwa na mlolongo mrefu wa maslahi binafsi na malalamiko ya muda mrefu, ambayo hayajafanyiwa kazi katika wilaya ya Tarime.

SOURCE: Nipashe

kwa msisitizo zaidi..
 
Huyu mvaa viatu hana tofauti na ISABELLA wa sinema ya SARAFINA.Unauza utu wako uwaangamize nduguzo,aibu kweli.
 
Kuna mtu ameomba picha yake:
Pengine ni vema kumwelewa George Marato kimatendo na kitabia kuliko kitaswira.
Huyu ni mmoja wa watumishi walevi na wasio na maadili yeyote ya kiuandishi. Haiitaji kuita takururu kumkamatisha rushwa huyu kijana.
Ukimuhitaji Marato nenda kwa walevi (sio Bar) maana huwa hatafuti news huko bali huwa analewa kila siku ya Mungu.
Mpe fedha na lolote unalomwambia aandike atariporti hivyo bila uchunguzi wowote hata kama si kweli. Kwa kifupi huyu ni mmoja tu wa mawakala wa yellow jornalism in Tz.
 
Haka ka bwana mdogo; kalikuwa kanakula h ela za akina Mkonona viongozi wengine wakifika huko; Nilishangaa eti Gaudensia kabaka kaenda kupiga kura akaonyeshwa ktk TV; why; kwani alikuwa na maslkahi gani ktk uchaguzi ule; huyu bwana alificha ukweli mwingi sana huko tarime muda wote na kuna mtu mmoja humu ktk Jamii alishawahi kudokeza; sasa ni muda muafaka; jana ilikuwa siku mbaya kwa akina GEORGE na mafisadi wote watapukutika
 
b. Kumuandikia Rais Kikwete barua ya kumtafa afikiria uteuzi wake wa Kapt. George Mkuchika kama Waziri wa Habari nchini. Wahariri wamedai kuwa Bw. Mkuchika amekuwa kikwazo cha uhuru wa habari na itakuwa ni kwa maslahi ya Taifa kama atahamishwa au kupangiwa jukumu jingine.

Ndio haya mambo ninayoyakataa, kwa nini walead kwa kuomba apangiwe majukumu mengine badala la kutolifanyia kazi taifa kabisa... huyu ameshindwa hii kazi ataweza ipi... akalime huyo... asaidie kulilisha taifa uongozi hauwezi
 
Back
Top Bottom