Jukwaa la Wahariri lamfungia Mkuchika; latoa ripoti ya Tarime

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,988
Jukwaa la Wahariri limechukua maamuzi kadhaa kuhusiana na kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo. Habari kutoka Dar-es-Salaam zinasema kuwa maamuzi hayo yamefikiwa baada ya jitihada zote za kuitaka Wizara hiyo kubatilisha (rescind) uamuzi wake wa kulifungia gazeti hilo kushindikana.

Maamuzi yaliyochukuliwa na Jukwaa hilo ambalo linawakusanya Wahariri wa magazeti nchini ni haya yafuatayo:

a. Kuanzia jana kutoandika habari zozote zinazomhusu Kapt. George Mkuchika kama Waziri wa Habari kwa muda wa siku tisini. Uamuzi kama huo uliwahi pia kuchukuliwa huko nyuma dhidi ya Waziri wa Mambo ya Ndani Bw. Omar Ramadhani Mapuri ambaye naye alisusiwa na vyombo vya habari baada ya kuonekana amehalalilsha matumizi ya mabavu kwenye kuwadhibiti waandishi wa habari waliokuwa wameenda kuripoti na kupiga picha sakata la Jeshi la Magereza na wananchi waliohamishwa kwa nguvu kutoka nyumba zao baada ya Jeshi hilo kuzichukua kwa nguvu.

b. Kumuandikia Rais Kikwete barua ya kumtafa afikiria uteuzi wake wa Kapt. George Mkuchika kama Waziri wa Habari nchini. Wahariri wamedai kuwa Bw. Mkuchika amekuwa kikwazo cha uhuru wa habari na itakuwa ni kwa maslahi ya Taifa kama atahamishwa au kupangiwa jukumu jingine.

c. Kufungua kesi ambayo itazuia kuendelea kutumika kwa baadhi ya sheria (kama ile ya Magazeti ya 1976) kutokana na ukweli kuwa tayari mapendekezo ya mswada wa sheria ya Uhuru wa Habari yameshawasilishwa kwa Mkuchika na mojawapo ya sheria ambazo zinalalamikiwa ni hiyo. Kimsingi wanataka kuhakikisha mahakama inazitangaza sheria hizo kuwa ni kinyume na Katiba na hivyo kutaka hatimaye kupitishwa kwa sheria mpya ya Uhuru wa Habari.

d. Kufanya maandamano makubwa ambapo yatahusisha waandishi wa habari na mashabiki wa vyombo huru vya habari wakiwa wamejifumba vitambaa midomoni kuashiria kunyamazishwa kwa vyombo vya habari nchini. Haya yatatangazwa lini na wapi.

e. Kuanza kukampeni kwa wafadhili, mabalozi, na taasisi za kimataifa juu ya uvunjaji wa haki ya uhuru wa maoni ambao umeanza kuonekana Tanzania na hivyo kutishia demokrasia yetu.

Jukwaa la Wahariri latoa ripoti ya Tarime


Wakati huo huo, Jukwaa hilo la Wahariri limetoa ripoti yake kuhusu madai na habari iliyotolewa kutoka Tarime mara baada ya kifo cha Mhe. Chacha Wangwe kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia Bw. Freeman Mbowe aliokolewa na Polisi baada ya kutishiwa na mapanga. Habari hiyo iliyotolewa kwenye magazeti kadhaa ikiwa imefanana karibu neno kwa neno ilionekana imeleta utata na kizaa zaa hasa baada ya kudaiwa kuwa ilikuwa imehusisha plagiarizing (kukopi maneno ya mtu mwingine neno kwa neno na kuyafanya kama ya kwako).

Tume iliyoundwa na Jukwaa hilo ikiongozwa na Bw. Saed Kubenea imetoa taarifa hiyo na kuhitimisha mambo kadhaa. Miongoni mwa mambo ambayo yametajwa ni kuwa:

a. Hakukuwa na mapanga yeyote yaliyokuwa yameoneshwa hadharani kiasi cha kusababisha madai kuwa alikuwa nusura Mbowe auawe na hivyo kulazimika kuokolewa na Polisi.

b. Hakukuwa na tukio hilo la majaribio ya kumdhuru Bw. Freeman kama lilivyoripotiwa.

c. Habari zote zilikuwa zimeandikwa na mwandishi mmoja.

(to be updated)
 
Jukwaa la Wahariri limechukua maamuzi kadhaa kuhusiana na kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo.

Mbona unanichanganya, sasa huyo Mkuchika hilo jukwaa limemfungia kivipi, kwa madaraka gani na anaathirikaje kwa kufungiwa huko?
 
Jukwaa la Wahariri limechukua maamuzi kadhaa kuhusiana na kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo. ...........................

a. Kuanzia jana kutoandika habari zozote zinazomhusu Kapt. George Mkuchika kama Waziri wa Habari kwa muda wa siku tisini. Uamuzi kama huo uliwahi pia kuchukuliwa huko nyuma dhidi ya Waziri mwingine wa Habari Bw. Mohammed Seif Khatib??

b. ...............

c. .............

d. .................................

e. ................................

..................................


Mkjj, Waziri aliyewahi kupata dhahama kama hii ni Waziri Omari Ramadhan Mapuri, wakati akiwa Waziri wa Mambo Ya Ndani katika awamu ya tatu. Yalimpata hayo baada ya kutoa kauli kuwa kupigwa kwa waandishi wa habari kule Ukonga ni sawa kwani walijitia kimbelembele kutetea raia waliopigwa na kuhamishwa kwa nguvu kwenye nyumba za ATC - Ukonga, ambazo Magereza walizichukua kwa nguvu.
 
Mkjj, Waziri aliyewahi kupata dhahama kama hii ni Waziri Omari Ramadhan Mapuri, wakati akiwa Waziri wa Mambo Ya Ndani katika awamu ya tatu. Yalimpata hayo baada ya kutoa kauli kuwa kupigwa kwa waandishi wa habari kule Ukonga ni sawa kwani walijitia kimbelembele kutetea raia waliopigwa na kuhamishwa kwa nguvu kwenye nyumba za ATC - Ukonga, ambazo Magereza walizichukua kwa nguvu.

sawa sawa... mawazoni nilikuwa namfikiria Waziri aliyehamishiwa na kupelekwa China, lakini jina la Mapuri likawa limenitoka ndio maana nikaweka hizo question marks... thanks. Nitaisahihisha.
 
Mzee Mwanakijiji,

Mbona na wao wanamfungia bila kumpa nafasi ya kujitetea? Inaelekea hata wao hawana tofauti na huyo Mkuchika
 
Sasa hayo magazeti yatajificha wapi yaliyokopi hizo habari za uongo huko Tarime. AU na yenyewe tuyasusie kuyasoma for 90 days?
 
Mzee Mwanakijiji,

Mbona na wao wanamfungia bila kumpa nafasi ya kujitetea? Inaelekea hata wao hawana tofauti na huyo Mkuchika

Wao siyo wanaoweza kumuwajibisha Waziri, na hivyo Waziri hawajibiki kwao na hivyo hawezi kujitetea kwao. Wao wametumia nguvu pekee waliyonayo nayo ni kalamu yao.

By the way, KLHN imepata nafasi ya kuzungumza na Mkuchika mapema leo kwa kirefu pamoja na Wakiri wa Halihalisi Bw. Mabere Marando....
 
Kitila,'
Hayo magazeti hayana aibu. Yalishamaliza kazi waliyotumwa. Lini ukaona fisadi ana aibu?
 
What Mkuchika did is a "sliver lining" for press freedom in the country.He has shot himself in the foot! All measures taken by the Forum are commendable.
 
c. Kufungua kesi ambayo itazuia kuendelea kutumika kwa baadhi ya sheria (kama ile ya Magazeti ya 1976) kutokana na ukweli kuwa tayari mapendekezo ya mswada wa sheria ya Uhuru wa Habari yameshawasilishwa kwa Mkuchika na mojawapo ya sheria ambazo zinalalamikiwa ni hiyo. Kimsingi wanataka kuhakikisha mahakama inazitangaza sheria hizo kuwa ni kinyume na Katiba na hivyo kutaka hatimaye kupitishwa kwa sheria mpya ya Uhuru wa Habari.

Hapo ndio naona watakuwa wameshughulikia tatizo kwenye chanzo. Hii ya kugomea kuandika itawapa nafasi waandishi "vibaraka" kutupa habari zilizopindishwa ama za propaganda bila upinzani kwa siku tisini. Kulishwa "sumu" kwa siku tisini ni muda mrefu sana, labda mniambie hata waandishi wa magazeti ya serikali (kina HabariLeo) na wale vibaraka wa mafisadi watafuata huo msimamo wa jukwaa la wahariri?

Kwa kuwa suala la kesi litachukua muda mrefu, katika muda huu wa kusubiria utatuzi wa kisheria ndipo wanaweza kufanya hayo maandamano, kuhamasisha uungwaji mkono wa kitaifa na kimataifa, na kumshinikiza rais kuondoa watendaji wanaoumiza uhuru wa habari (hii ngumu maana hatuna uhakika rais yuko upande gani, lakini kwa uzoefu kelele ikipigwa sana inaweza kusaidia japo kidogo).
 
Na hao wahariri walioshiriki kuandika habari hiyo moja ya kutungwa wamefanywa nini?
 
Wao siyo wanaoweza kumuwajibisha Waziri, na hivyo Waziri hawajibiki kwao na hivyo hawezi kujitetea kwao. Wao wametumia nguvu pekee waliyonayo nayo ni kalamu yao.

By the way, KLHN imepata nafasi ya kuzungumza na Mkuchika mapema leo kwa kirefu pamoja na Wakiri wa Halihalisi Bw. Mabere Marando....

Mzee Mwanakijiji,

Huoni kwamba wameamua kutokuandika habari zake kwa miezi mitatu? Je walimwita hata kumhoji kabla ya kuchukua hiyo hatua?

Naona wanafanya makosa hayo hayo ambayo Mkuchila ameyafanya kwa Mwanahalisi.
 
Jukwa la wahariri ni kijiwe tuu wanamtishia nyau Mhe.Mkuchika!. Liko kama kikao cha harusi cha watu fulani kutangaza kususia kufanya sherehe yao ukumbi fulani. Hili jukwaa halina any legal status wala registration ya aina yoyote. Afadhali kidogo MOAT japo haipo kisheria imesajiliwa kama kampuni.

Chombo halali chenye nguvu ya kisheria kumuadhibu Mkuchika ni Media Council of Tanzania (MCT) na Tanzania Journalist Association(TAJA) ambacho nadhani kiko ICU.
Wahariri wa Jukwaa la wahariri hawana ubavu wa kweli kumuadhibu Mkuchika ni magazeti machache tuu ndiyo yenye uwezo wa kweli haswa yale ambayo wahariri wake ni wamiliki kama Kubenea wengine hawana jeuri hiyo kwa vile wamiliki wanajikomba serikalini hiv
yo huo ndio mwanzo wa kugeukana na kusalitiana.
Mtathibitisha kauli yangu soon. Mhe. Mkuchika ni JK type, mbabe,Jeuri, hasikilizi wala hashauriki. Kumshauri JK kumuadhibu Mkuchika ni kesi ya nyani kuipeleka kwa ngedere
 
Mzee Mwanakijiji,

Huoni kwamba wameamua kutokuandika habari zake kwa miezi mitatu? Je walimwita hata kumhoji kabla ya kuchukua hiyo hatua?

Uamuzi wa kuandika au kutomuandika mtu ni uamuzi wa mhariri. Wao wahariri hawana nguvu yeyote au uwezo wowote wa kumuita Waziri na kumhoji.

Naona wanafanya makosa hayo hayo ambayo Mkuchila ameyafanya kwa Mwanahalisi.

Hapana; Mkuchika ana nguvu za kisheria za kumuita Mhariri na hata kuliwajibisha gazeti lake. Jukwaa la Wahariri hawana nguvu ya kumuita Waziri na kabisa hawana nguvu ya kumhoji.
 
Tatizo ni kuwa kwa kuwa vyombo vingine vinamilikiwa na mafisadi, kifungo cha Mkuchika hakitakuwa na nguvu kwa sababu habari zake zitaandikwa na magazeti hayo
 
Chombo halali chenye nguvu ya kisheria kumuadhibu Mkuchika ni Media Council of Tanzania (MCT) na Tanzania Journalist Association(TAJA) ambacho nadhani kiko ICU.

Hata vyombo hivyo havina uwezo wa kisheria "kumwadhibu" Waziri. Ni Rais peke yake ndiye anaweza kumuwajibiwa Waziri wake. Nguvu pekee waliyonayo ni kusema, kutoa maoni na kuandika wanavyoandika nje yapo wanaweza kunung'unika au kwenda mahakamani (na hapo si kwa lengo la kutengua uamuzi wa Waziri kwa mujibu wa sheria ya 1976)


Wahariri wa Jukwaa la wahariri hawana ubavu wa kweli kumuadhibu Mkuchika ni magazeti machache tuu ndiyo yenye uwezo wa kweli haswa yale ambayo wahariri wake ni wamiliki kama Kubenea wengine hawana jeuri hiyo kwa vile wamiliki wanajikomba serikalini hivyo huo ndio mwanzo wa kugeukana na kusalitiana.

Tutaona hapa lakini wasiposimama kunyongwa pamoja, watajikuta wananyongwa mmoja mmoja...

Mtathibitisha kauli yangu soon. Mhe. Mkuchika ni JK type, mbabe,Jeuri, hasikilizi wala hashauriki. Kumshauri JK kumuadhibu Mkuchika ni kesi ya nyani kuipeleka kwa ngedere

Hili haliwezi kuwa la ajabu sana kwani wanasemaga kwenye msafara wa mamba hata kenge nao wamo...
 
Hiyo ndo maana yake. Na kwanini wanatoa kauli hiyo baada ya uchaguzi?
BTW: Welcome back Kitila!

Na hiyo ripoti ingeathiri vipi uchaguzi wa Tarime ? Je, ni vibaya wananchi kwa ujumla wao wakijua ukweli wa mambo ? Je, hiyo ripoti ingetolewa ina maana ingesaidia CCM na Chadema haingeshinda ? Kwa hakika nashindwa kuelewa msimamo wa hili jukwaa !!
 
Back
Top Bottom