Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Kuna mambo mengi yanatokea nchini ambayo yanagusa maslahi ya wafanyakazi. Mambo ambayo kuendelea kwake kunahatarisha maslahi ya wafanyakazi na mambo mengine ambayo yamesababisha ukimya na utulivu wa vyama hivyo kusimamia watawala. Vyama vya wafanyakazi kwa asili yake viliibuka ili kuzuia nguvu ya mabepari kunyonya nguvu kazi za wafanyakazi na kudai maslahi bora zaidi ya kazi n.k Lakini katika sehemu nyingi vyama vya wafanyakazi vimeendelea kuwa speed governors dhidi ya utawala unaojaribu kujinufaisha kwa migongo ya wafanyakazi na hivyo kutokana na mbinu mbalimbali vyama hivyo vimeweza kusababisha hata mabadiliko ya kisiasa na kisheria kwnye nchi mbalimbali.
Kwa Tanzania vyama vya wafanyakazi vina historia ndefu ya kubadilisha mwelekeo wa kisiasa nchini. Sasa hivi vyama hivi vinaonekana vimekaa pembeeni na kuacha vyama vya upinzani kufanya yale ambayo yalitakiwa kufanywa na vyama vya wafanyakazi. Ni kitu gani kimetokea nchini na kusababisha hii docility ya vyama vya wafanyakazi nchini? Ni kwanini vyama vya wafanyakazi havina uthubutu wa kusimama na kudai maslahi bora ya kweli ya wananchi lakini wakati huo huo kuzuia ufujaji mkubwa wa raslimali zetu ili raslimali hizo zitumike kuinua maslahi ya wafanyakazi? Yawezekana vyama vya wafanyakazi nchini havina tena nafasi isipokuwa wakati wa kudai kima cha chini cha mishahara na siyo mambo mengine? Je bado vina umuhimu wa watu kujiunga navyo? Je vyama hivi vinaweza kuwa na nguvu ya kubadilisha maisha ya wanachama wake bila kugongana na wanasiasa?
Michango yenu itanisaidia katika hoja yangu ya Jumatano.
Kwa Tanzania vyama vya wafanyakazi vina historia ndefu ya kubadilisha mwelekeo wa kisiasa nchini. Sasa hivi vyama hivi vinaonekana vimekaa pembeeni na kuacha vyama vya upinzani kufanya yale ambayo yalitakiwa kufanywa na vyama vya wafanyakazi. Ni kitu gani kimetokea nchini na kusababisha hii docility ya vyama vya wafanyakazi nchini? Ni kwanini vyama vya wafanyakazi havina uthubutu wa kusimama na kudai maslahi bora ya kweli ya wananchi lakini wakati huo huo kuzuia ufujaji mkubwa wa raslimali zetu ili raslimali hizo zitumike kuinua maslahi ya wafanyakazi? Yawezekana vyama vya wafanyakazi nchini havina tena nafasi isipokuwa wakati wa kudai kima cha chini cha mishahara na siyo mambo mengine? Je bado vina umuhimu wa watu kujiunga navyo? Je vyama hivi vinaweza kuwa na nguvu ya kubadilisha maisha ya wanachama wake bila kugongana na wanasiasa?
Michango yenu itanisaidia katika hoja yangu ya Jumatano.