Judgment Day: May 21, 2011 (Really?)

Habari zenu ndugu zangu great thinkers! kwanza kabisa poleni na shida/taabu mbalimbali ya dunia hii, Ok baada ya salaam hizo leo nimekuja na hii hoja baada ya kusikia habari zikienea sana mitaani toka kwa mapaparazi wanaojiita wao ni makachero wa mbinguni wakidai mwisho wa dunia ni 21/5/2011, sasa sijui kama kuna ukweli wowote wa hili jambo?

Hiyo ni kazi ya yule mwovu IBILISI kupitia mtandao wake wa FREE-MANSON na makamanda wao ILUMINANT!! kazi yao kubwa ndo hiyo kupingana na Ukweli wa Mungu! Wao hupenda kuchanganya wanadam kwa kugeuza ukweli kuwa kinyume."HAKUNA AJUAYE SIKU WALA SAA ILA BABA WA MBINGUNI"wao wanakuja na tarehe kabisa.Cha msingi sisi tunatakiwa kuendelea na shughuli zetu kama kawada huku tukimuomba Mungu siku hiyo(IJUAE MUNGU) ituke salama! Wapotoshaji wakubwa hamkumbuki ya mwaka 2000?? Yaliyotokea Uganda je?? Basi kesheni mkiomba maana hamjui siku wala saa; mwana wa Adam atakuja kama mwizi; atakuta watu wakila na kunywa,wengine wakioa na kuolewa n.k!
 
Habari zenu ndugu zangu great thinkers! kwanza kabisa poleni na shida/taabu mbalimbali ya dunia hii, Ok baada ya salaam hizo leo nimekuja na hii hoja baada ya kusikia habari zikienea sana mitaani toka kwa mapaparazi wanaojiita wao ni makachero wa mbinguni wakidai mwisho wa dunia ni 21/5/2011, sasa sijui kama kuna ukweli wowote wa hili jambo?

Mbona mamlaka ya utabiri wa hali ya hewa hawajatutangazia?
 
SOMA MATHAYO 24

'' Wanafunzi wake wakamwendea wakamuuliza Bwana ni lini siku ya kuja kwako au Mwisho wa Dunia?
'' Akawajibu asiwadanganye mtu.
>watakuja wengi kwa jina langu
>Watakuja manabii wa uongo
>watawadanganya wengi yumkini kama wateule
> Watasema yuko huku yupo kule
> Msiwaamini hao

>>Kutakuwa na vita mahali na mahali
>>Ufalme kupigana na Ufalme
>>Taifa kupigana na taifa
>> Huo ndio mwanzo wa Uchungu!!!!!
>>Watu watakuwa wenye kupenda fedha kuliko kumpenda Mungu
>> Watawachukiwa wa kwao
>> Watoto hawatawahesimu wakubwa
>> Mioyo ya wengi itapondeka
>>Kutakuwa na njaa mahali na mahali

PALE MTAKAPOONA CHUKIZO LA UHARIBIFU LINAINGIA PATAKATIFU PAKE MJUE ULE MWISHO UMEKARIBIA
>> Ndipo aliyeko shamba asirudi nyumbani
>>Aliyepo nyumbani asiende sokoni
>>aliyepo darini abaki huko huko
>>>Aliyepo Tanganyika asiende anzibar
>>>Aliyepo Zanzibar asije Tanganyika

MWENYE KUSIKIA NA AFAHAMU MANENO HAYA!


Neno limenigusa sana.Ubarkiwe na Bwana.
TUSALI WOTE:Eee Yesu Kristo mwana wa Mungu nikuaminie nakusihi unipe kwa neema na wala si ustahili ,fursa ya kuingia kwa ufalme wa mbingu siku ya mwisho.
AMEN.
 
Radiation continues to poison water and food in Japan after three Nuclear Reactors were damaged in the Recent 9.0 Earthquake. Since the March 11 Quake, Radiation levels have raised to unsafe, potentially deadly levels in Japan, signifying the coming Doomsday on May 21.
Earthquakes, floods, and natural disasters are mentioned throughout the Bible and Book of Revelations as warning signs that Jesus will return to Earth to rule during the Apocalypse. The Japan Earthquake is a sign of Doomsday. The flood caused by the tsunami that followed is a sign of Judgement Day. The Nuclear Disaster that in Japan is a sign of the Apocalypse. Keep your eyes open, there are signs of the May 21 Doomsday all around us.

 
Last edited by a moderator:
So we also have Hysterics in the JF? Okay, see you in the same world after May 21st.
 
In loving memory of myself mhh!!
ngoja nikachukue mkopo kibaruani niponde raha kuanzia wiki ijayo mpaka tarehe 21 :biggrin1::biggrin1::biggrin1:
 
Crap
Hii ndo kama ile tulioambiwa
mwisho wa duniani 2000..tukalala makanisani.. 10year s later bado tuko hapa
sasa wengine wengi wanadai ni 2012..
Usema ukweli ajuae mwisho wa uhai ni aliekupa pumzika (Mwenyeenzi Mungu)
 
Una mpango wa kwenda kokote katikati ya mwaka huu? Mie nilikuwa na mpango, na bado ninao, wa kwenda kushangaa wanyama huko mbuga ya Mikumi. Pia nina mpango wa kufanya marekebisho madogomadogo katika nyumba ninayoishi kwa sababu mwenye nyumba wangu kagoma kunikarabatia. Pia nina mpango wa kukutana na watu hapa kijijini na kujuzana hili na lile kama ilivyo ada kila siku.

Lakini ati pamoja na kuwa na mipango yote hii ambayo inasubiri utekelezaji jamaa wananambia ati tarehe 21 /05 /2011 dunia yetu inafika tamati, au kwa kiswahili rahisi ni kwamba tarehe hiyo ndio 'mwisho wa dunia', namaanisha ' Kiama'.

Waliokuja na habari hizi ni jamaa fulani huko Carlifornia, Marekani, ambao wanasemekana kutumia fursa hiyo kujiongezea umaarufu kwa kutafuta air time kwenye vyombo vya habari.

Jamaa hawa waliokuja na habari hizi za 'mwisho wa dunia' ni wafuasi wa dini ya Kikristo wenye msimamo mkali wanaoongozwa na mtangazaji wa radio, Harold Camping, anayetangaza katika radio ya Family Radio Network.
Akitumia mistari ya Biblia, jamaa huyu amesema kwamba dunia itafika tamati miaka 7 ,000 kutokea mafuriko makubwa katika uso wa dunia, na kwa mujibu wa kalenda yake ni kwamba mwisho wa dunia yetu ni Mei 21.

Inasemekana hii si mara ya kwanza kwa Harold kufanya utabiri kama huu kwani mwaka 1994 kutabiri kuwa mwaka huo dunia ilikuwa ikifikia tamati lakini cha kustaajabisha hadi leo bado yupo pamoja na wafuasi wake. Siku zote amekuwa na namna ya kujitetea utabiri wake unapokwenda kombo, " Kuna wakati Mungu anakuonesha mambo lakini hakuoneshi kwa ukamilifu wote.

Ni miaka mitatu iliyopita ndipo Mungu amenionesha ukweli wote." Lakini mara hii, Harold amekuwa akisisitiza kwamba yuko sahihi kabisa tofauti na mwaka 1994 , na mara hii emungwa mkono na watu wasiopungua 50 , akiwemo Gary Vollmer, mwajiriwa katika wizara ya mambo ya ndani ya Marekani ambaye amechukua likizo ya bila malipo, likizo inayokwisha tarehe 23 Mei.

Gary amesema hategemei kurejea kwa mwajiri wake kwani tarehe 21 Mei atakuwa ' amekwishanyakuliwa'.

Enewei, nimefurahi kufahamiana na kila mmoja tuliyekutana na kubadilishana hili na lile hapa kijijini. Iwapo kweli tarehe 21 litatokea la kutokea tukutane upande wa pili. Chiazzzzz.
 
New Age Movement in action! wajiandae tu kunywa sumu! they will end up like Rev Jones' or Kibwetere's followers
 
Tusubiri tuone,mimi nilisikia 2012 ndo mwisho,sa hii yako ni mpya,lakini kulingana na dini yangu hakuna anayejua siku wala saa,
 
Inabidi dhehebu hilo life kabisa kama Dunia itakatiza 21 May 2011 na kuingia 22 May 2011 na kuendelea. This guy should undergo psychiatric treatment!
 
Una mpango wa kwenda kokote katikati ya mwaka huu? Mie nilikuwa na mpango, na bado ninao, wa kwenda kushangaa wanyama huko mbuga ya Mikumi. Pia nina mpango wa kufanya marekebisho madogomadogo katika nyumba ninayoishi kwa sababu mwenye nyumba wangu kagoma kunikarabatia. Pia nina mpango wa kukutana na watu hapa kijijini na kujuzana hili na lile kama ilivyo ada kila siku.

Lakini ati pamoja na kuwa na mipango yote hii ambayo inasubiri utekelezaji jamaa wananambia ati tarehe 21 /05 /2011 dunia yetu inafika tamati, au kwa kiswahili rahisi ni kwamba tarehe hiyo ndio 'mwisho wa dunia', namaanisha ' Kiama'.

Waliokuja na habari hizi ni jamaa fulani huko Carlifornia, Marekani, ambao wanasemekana kutumia fursa hiyo kujiongezea umaarufu kwa kutafuta air time kwenye vyombo vya habari.

Jamaa hawa waliokuja na habari hizi za 'mwisho wa dunia' ni wafuasi wa dini ya Kikristo wenye msimamo mkali wanaoongozwa na mtangazaji wa radio, Harold Camping, anayetangaza katika radio ya Family Radio Network.
Akitumia mistari ya Biblia, jamaa huyu amesema kwamba dunia itafika tamati miaka 7 ,000 kutokea mafuriko makubwa katika uso wa dunia, na kwa mujibu wa kalenda yake ni kwamba mwisho wa dunia yetu ni Mei 21.

Inasemekana hii si mara ya kwanza kwa Harold kufanya utabiri kama huu kwani mwaka 1994 kutabiri kuwa mwaka huo dunia ilikuwa ikifikia tamati lakini cha kustaajabisha hadi leo bado yupo pamoja na wafuasi wake. Siku zote amekuwa na namna ya kujitetea utabiri wake unapokwenda kombo, " Kuna wakati Mungu anakuonesha mambo lakini hakuoneshi kwa ukamilifu wote.

Ni miaka mitatu iliyopita ndipo Mungu amenionesha ukweli wote." Lakini mara hii, Harold amekuwa akisisitiza kwamba yuko sahihi kabisa tofauti na mwaka 1994 , na mara hii emungwa mkono na watu wasiopungua 50 , akiwemo Gary Vollmer, mwajiriwa katika wizara ya mambo ya ndani ya Marekani ambaye amechukua likizo ya bila malipo, likizo inayokwisha tarehe 23 Mei.

Gary amesema hategemei kurejea kwa mwajiri wake kwani tarehe 21 Mei atakuwa ' amekwishanyakuliwa'.

Enewei, nimefurahi kufahamiana na kila mmoja tuliyekutana na kubadilishana hili na lile hapa kijijini. Iwapo kweli tarehe 21 litatokea la kutokea tukutane upande wa pili. Chiazzzzz.

Tihi tihi...nitarudi 22 May
 
Back
Top Bottom