babykailama
JF-Expert Member
- Mar 5, 2012
- 251
- 243
Ni wazi kuwa siku za karibuni, vipindi vilivyoanza vyema vya ITV kv. Dakika 45, Malumbano ya Hoja na Kipima Joto sasa vinapwaya na kukosa mvuto.
Tafadhali fuatilia uone ni wapi hao waandaaji wa vipindi wamekosea Kitaaluma.
1. Kijana wa kipindi cha Dk 45 akaribishe mchanganyiko wa Wataalam mbalimbali na si viongozi tu wa Serikali na maswali yake yaonyeshe umahiri ktk tasnia ya habari. Mwonyeshe hata vipande tu vya Hard Talk kwa wiki yote akiwa peke yake studio ajifunze!!
Mfano. vipindi vijavyo waite, Kiongozi wa Chama cha Madaktari, Kiongozi wa TUCTA, Viongozi wa vyama vya upinzani, Viongozi wa vyama vya Walemavu, Viongozi wa Taasisiza Haki za binadamu, Watu waliokuwa tishio ambao wamejirudi na kuwa watu wema ktk jamii, Kiongozi wa Wazee waliotumika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
2. Couple (Original wa awali) wa kipindi cha Malumbano ya Hoja, kama wasimamizi wawe serious katika ku moderate mijadala na uchaguzi wa washiriki uwe 'balanced'. Waache kuongea sana wao, vinginevyo wawe washiriki tujue moja.
3. Mzee wa kipindi cha kipima joto, angalia kwa upya uchaguzi wa mada nyeti na pia urudi kama zamani ambapo wawakilishi wa makundi mbalimbali walikaribishwa bila kukosa wawakilishi wa wananchi - walala hoi na pia wanaharakati. Na kwa nini hampokei simu zetu kila wakati mnajidai mko buzy??? Tena wa kutoka nje ya nchi nadhani ndio kabisaaaaa,mnaogopa nini?
Mada nyeti zaweza kuwa: Marekebisho ya Katiba , Muungano - Tanzania, Mafisadi Tz, Digrii feki nchini, Maslahi vs wajibu wa Wabunge, Sayansi & Teknolojia Tanzania, Michango ya Mitandao ya habari ktk maendeleo ya nchi na dunia kwa ujumla, Malalamiko ya wananchi ya migogoro ya ardhi.
Bado sijapoteza kabisa imani yangu katika ITV, Mhavile you can make it!
Tafadhali fuatilia uone ni wapi hao waandaaji wa vipindi wamekosea Kitaaluma.
1. Kijana wa kipindi cha Dk 45 akaribishe mchanganyiko wa Wataalam mbalimbali na si viongozi tu wa Serikali na maswali yake yaonyeshe umahiri ktk tasnia ya habari. Mwonyeshe hata vipande tu vya Hard Talk kwa wiki yote akiwa peke yake studio ajifunze!!
Mfano. vipindi vijavyo waite, Kiongozi wa Chama cha Madaktari, Kiongozi wa TUCTA, Viongozi wa vyama vya upinzani, Viongozi wa vyama vya Walemavu, Viongozi wa Taasisiza Haki za binadamu, Watu waliokuwa tishio ambao wamejirudi na kuwa watu wema ktk jamii, Kiongozi wa Wazee waliotumika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
2. Couple (Original wa awali) wa kipindi cha Malumbano ya Hoja, kama wasimamizi wawe serious katika ku moderate mijadala na uchaguzi wa washiriki uwe 'balanced'. Waache kuongea sana wao, vinginevyo wawe washiriki tujue moja.
3. Mzee wa kipindi cha kipima joto, angalia kwa upya uchaguzi wa mada nyeti na pia urudi kama zamani ambapo wawakilishi wa makundi mbalimbali walikaribishwa bila kukosa wawakilishi wa wananchi - walala hoi na pia wanaharakati. Na kwa nini hampokei simu zetu kila wakati mnajidai mko buzy??? Tena wa kutoka nje ya nchi nadhani ndio kabisaaaaa,mnaogopa nini?
Mada nyeti zaweza kuwa: Marekebisho ya Katiba , Muungano - Tanzania, Mafisadi Tz, Digrii feki nchini, Maslahi vs wajibu wa Wabunge, Sayansi & Teknolojia Tanzania, Michango ya Mitandao ya habari ktk maendeleo ya nchi na dunia kwa ujumla, Malalamiko ya wananchi ya migogoro ya ardhi.
Bado sijapoteza kabisa imani yangu katika ITV, Mhavile you can make it!