hotuba ya Nassari pale NMC ililenga kulaani mauaji ya mwenyekiti wa CDM Usariver, ambayo hayaja shughulikiwa ipasavyo. Kuna wabunge wa CDM walicharangwa mapanga, na jeshi la polisi lipo kimya. Nassari alitishia kujitenga au kumpiga raisi marufuku, lakini uchambuzi wako wenye "MANTIKI" na wengine wengi mnachambua kama kwamba tayari ameshatoa tamko rasmi la huko kujitenga! Alisema KAMA, polisi wasipo shughulika kuwapata wauaji na kuwachukulia hatua.... Labda hatuna "MANTIKI", tunaongozwa na hisia na ushabiki, lakini nashawishika kuamini kwamba Nassari alisukumwa na mauaji ambayo yana sura ya visasi vya kisiasa na ubutu wa polisi kufanya kazi yao kutoa kauli tunazotumia kumhukumu. Ndo maana naomba tuangalie context kabla ya kufanya hitimisho la uchambuzi wa maneno.
Mimi ni mfuasi na muumini wa Mungu aliye hai, na jina langu hapo juu ni halisi, and I gave you my number. Sina unafiki, na siyo mwanachama wa CDM, lakini naijua haki na ntasimama kwenye haki tu.
Kwa taarifa tu, mh. Nassari aliomba msamaha kupitia Radio Sunrise juzi jioni baada ya kutoka Police Central.
Alipigiwa simu na kufanyiwa mahojiano ambapo alikiri kuteleza nami kwa kweli sikurekodi ila kilikuwa kipindi chao (Sunrise) maarufu cha kuanzia saa 2 usiku cha matukio ya siku. Sasa kwa ushauri wangu/wetu angejitokeza humu JF. aombe msamaha kwani ile radio haisikiki nchi nzima. Kuteleza sio kuanguka.