EMT udaku haufanani na wewe aisee
Mie nilikuwepo, mbona sijamsikia akitangaza?
Mie nilikuwepo, mbona sijamsikia akitangaza?
Mie nilikuwepo, mbona sijamsikia akitangaza?
Nilikuwepo kweli pale alipotakiwa na WanaCDM Halima Mdee awasalimie WanaCDM waliofurika pale na ndipo akasema akiwafurahisha wanainchi lakini hakuwa na ukweli ktk msemo wake!
Na hata ingekuwa hivyo ingependeza sana kwn ni kila kitu na wakati wake!!
Ingependeza sanaaaaaaaaa!!
Mie nilikuwepo, mbona sijamsikia akitangaza?
Huyu anadai alikuwepo na hukusikia hayo
Labda hakusikia kutokana na shamrashamra nyingi iliyokuwa imetanda anga ile,Ila hakika H. Mdee alifurahisha halaiki ile kwa neno hilo but hakuwa serias!
Kwa maelezo yako hakuna kitu kama hicho-kuolewa na Nassari. Kwanini kuzua na kutunga wakati wahusika wapo? Kufurahi na kuolewa mbona ni vitu viwili tofauti na wazi? It is the matter of using just common sense even sense commonly if you cannot use common sense.
Kwa mujibu wa tovuti ya Habari Leo mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema) amesema sasa yuko tayari kufunga ndoa na Mbunge mteule wa chama hicho wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari. Nafurahi kwamba Nassari hatimaye ameshinda ubunge katika uchaguzi mdogo, alisema Mdee wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa Arusha na Meru.
Mdee alifafanua, kwamba yeye na chama chake walikuwa wamebanwa na kampeni za kuhakikisha Chadema inatwaa jimbo la Arumeru Mashariki na ndiyo sababu hakujibu mara moja maombi ya Nassari ya kumwoa aliyoyatoa katika moja ya mikutano yake ya kampeni.
Naondoka kwenda Dar es Salaam kujiandaa kwa Mkutano ujao wa Bunge, kisha nitakwenda Dodoma ambako nitamsubiri Nassari na kwa pamoja tutafanya maandalizi, alisema Mdee huku akishangiliwa na hadhira hiyo huku wakiimba na kucheza katikati ya mvua iliyokuwa ikinyesha.
Mdee alisema ndoa kati ya wabunge hao wawili wa Chadema ni wazo zuri na itatangazwa sana na kuandika historia. Alipoona anashambuliwa sana na wapinzani wake juu ya useja wake katika kampeni hizo, Nassari hatimaye alitangaza kumwoa Mdee ambaye pia hajaolewa.
Na katika moja ya mikutano ya hadhara, alisimama naye jukwaani kukampeni. Kuna viongozi wengi wa kidini Dodoma, ikiwa ni pamoja na ndani ya Bunge ambao watatushauri jinsi ya kulitimiza hili, alisema Mdee na kuongeza kwamba baba yake Joshua, Mchungaji Samuel Nassari alipata kusema, mwanamke mzuri ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Chadema ina idadi kubwa ya wabunge vijana ambao hawajaoa, ikiwa ni pamoja na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi Mr Sugu; wa Ubungo, John Mnyika; wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na sasa Nassari.
Source: Habaroleo: HabariLeo | Halima Mdee atangaza kuolewa na Nassari
Mwanzoni nilidhani ni habari ya April fool lakini imeandikwa tarehe 3 Machi baada ya uchaguzi.