Superman
JF-Expert Member
- Mar 31, 2007
- 5,695
- 1,696
Kwa upande wake mgombea ubunge, Bw. Joshua Nassari, naye alimvaa Bw. Wassira kwa kauli yake ya kutaka wananchi wasimchague kwa kuwa hajaoa.
"Kwa kuwa wameniambia sijaoa, nitamuoa Halima Mdee (mbunge wa Jimbo la Kawe) ili wananchi wa jimbo hili wanufaike mara mbili, hivyo jimbo litakuwa na wabunge wawili," alisema.
Alisema anaomba Mungu usiku na mchana ili afanikiwe kumuona, Bi. Halima Mdee, ili akishinda ubunge wananchi wa Arumeru wawe na wabunge wawili, ambao watakuwa mke na mume.
Source: MAJIRA - GAZETI HURU LA KILA SIKU:: Slaa afunika
Food for Thought . . Sasa Dogo Janja Joshua ameshashinda Ubunge; Je imekaaje hii ya Kumwoa Halima Mdee?