Nauliza Mh Warioba mbona kimya,hapo zamani alikuwa na kawaida ya kutoa maoni au kushauri juu ya mustakabali wa nchi yetu pale Wakubwa walipokuwa wanafanya madudu yao.Lakini baadaye tukasikie kuwa nae anatishwa na wakubwa kuwa watampeleka mahakamani kwa madai ya ufisadi,hapo akajitetea kidogo na sasa sijui ndio KANYWEA kwa kuogopa kufikisha mahakamani kwani kwa jinsi masuala yanavyoenda ndani ya chama chake cha CCM na yeye kukaa kimya nashindwa kumwelewa kama yule Warioba jasiri kakaa kimya au ndio kaona ni kama KUMPIGIA MBUZI ZEZE?