John Momose Cheyo: Mwanasiasa wa Kweli au Mganga Njaa?

Mdau

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,789
470
Ndugu wadau, kwa mtizamo wangu, naona kwamba huyu mheshimiwa anajipendekeza mno kwa CCM/serikali.... Chukulia mfano wa matukio haya:....jinsi alivyocheza ngoma wakati wa ziara ya Rais na kumsifu sana, kana kwamba serikali imetimiza yote kwa wananchi, wakati ukweli ni kwamba hata jimboni kwake Bariadi Mashariki, hali ya kipato cha mwananchi wa kawida inasikitisha sana.......pia kitendo cha kupingana na wenzake wa kambi ya Upinzani Bungeni ktk kikao kinachoendelea,ambapo alifukuzwa toka kambi ya upinzani na pia Sitta leo, kuthibitisha adhabu hiyo kimezidi kunipa wasiwasi....
Kama mchambuzi wa siasa,nachukulia mambo haya anayofanya kama ni kutojiamini, woga, kujipendekeza, na kutaka CCM wamuonee huruma ili wasimpe upinzani wa dhati jimboni kwake...(nakumbuka katika moja ya mikutano yake ya kampeni, aliwahi kudai kwamba CCM ni wezi sana,waliwahi kukosea ktk kuiba kura kwenye kituo alichopigia kura yeye na familia yake na wakamuachia kura moja tu!!!). Kwa hali hii,nathubutu kusema Cheyo kageuza ubunge wake kama ajira na si mtumishi wa kweli wa wananchi,jimboni na hata taifani pia....Watanzania tuzidi kuamka,tuweze kutofautisha sasa wanasiasa njaa na wa kweli...
 
sasa mbona umetoa hukumu?

cheyo anajua siasa,
cheyo anajua kuchambua mambo
cheyo ana mawazo chanya sana katika sisa za nchi hii.

hivi kwa mtazamo wako angejiunga na hao wenzie juzi kati hapa huu ya bajeti,unadhani bajeti isingepita?

think beyond the next meal man!
 
sasa mbona umetoa hukumu?

cheyo anajua siasa,
cheyo anajua kuchambua mambo
cheyo ana mawazo chanya sana katika sisa za nchi hii.

hivi kwa mtazamo wako angejiunga na hao wenzie juzi kati hapa huu ya bajeti,unadhani bajeti isingepita?

think beyond the next meal man!

mkuu; soma upya sehemu nilizo-bold kisha ufafanue maelezo yako,nadhani sijaelewa sijui!!??? navyofahamu mm, kwenye msimamo wa kambi,hata kama bajeti inapita,kupinga ni kielelezo cha kwamba wao kama wapinzani,hawajaridhika na mambo kadhaa kwenye bajeti,na ni utaratibu wa democracy pia,na wataendelea kuwa wabunge, ila changamoto wanakua wametoa tayari....
pili, ukisoma kwa makini post yangu,nimetoa maoni yangu na si hukumu mkuu....hata hivyo,naheshimu maoni yako..
 
Mpinzani wa kweli ni yupi?, tatitizo mpinzani hata ufanye mema milioni lakini ukiunga mkono jambo la ccm basi wewe si mpinzani, ukweli wa cheyo wanaujua wananchi wa jimboni kwake na kile anacho amini yeye
 
mwacheni jamani......njaaaa....njaaaa...........njaaa......jamani hakuna mtetea haki wote njaaa.....na kutaKA KUONEWA HURUMA baadae.............zito kabwe...njaaaaaa..........mrema...njaaaaaaa.........
Ndugu wadau, kwa mtizamo wangu, naona kwamba huyu mheshimiwa anajipendekeza mno kwa CCM/serikali.... Chukulia mfano wa matukio haya:....jinsi alivyocheza ngoma wakati wa ziara ya Rais na kumsifu sana, kana kwamba serikali imetimiza yote kwa wananchi, wakati ukweli ni kwamba hata jimboni kwake Bariadi Mashariki, hali ya kipato cha mwananchi wa kawida inasikitisha sana.......pia kitendo cha kupingana na wenzake wa kambi ya Upinzani Bungeni ktk kikao kinachoendelea,ambapo alifukuzwa toka kambi ya upinzani na pia Sitta leo, kuthibitisha adhabu hiyo kimezidi kunipa wasiwasi....
Kama mchambuzi wa siasa,nachukulia mambo haya anayofanya kama ni kutojiamini, woga, kujipendekeza, na kutaka CCM wamuonee huruma ili wasimpe upinzani wa dhati jimboni kwake...(nakumbuka katika moja ya mikutano yake ya kampeni, aliwahi kudai kwamba CCM ni wezi sana,waliwahi kukosea ktk kuiba kura kwenye kituo alichopigia kura yeye na familia yake na wakamuachia kura moja tu!!!). Kwa hali hii,nathubutu kusema Cheyo kageuza ubunge wake kama ajira na si mtumishi wa kweli wa wananchi,jimboni na hata taifani pia....Watanzania tuzidi kuamka,tuweze kutofautisha sasa wanasiasa njaa na wa kweli...
 
Mpinzani wa kweli ni yupi?, tatitizo mpinzani hata ufanye mema milioni lakini ukiunga mkono jambo la ccm basi wewe si mpinzani, ukweli wa cheyo wanaujua wananchi wa jimboni kwake na kile anacho amini yeye
Mbunge pamoja na kuwakilisha jimbo lake pia anawakilisha kusimamia maslahi ya taifa kwa kura yake Bungeni hata kauli zake. Huwezi kuwa Mbunge wa Newala ukaacha kuunga mkono kupinga ufisadi katika uchimbaji dhahabu eti kwa vile Newala hakuchimbwi dhahabu. Mpinzani wa kweli hawezi kusema anaunga mkono Li bajeti kama hili hata kama anajua kupinga kwake hakuzuii kupita kwake.
Hii ni kama ule upuuzi wa baadhi ya wabunge wa CCM ambao akipewa nafasi analalamika sana kwamba jimbo lake limesahauliwa sana na bajeti hii ktk miradi mingi kisha anamalizia kwa kusema "Mhe Spika naunga mkono hoja kwa asilimia 105".
Ujinga gani huo? Kama ulkuwa ni msimamo wa Kambi ya upinzani kutokuunga mkono hoja,naye kama waziri kivuli akageuka, sasa iweje? fukuza. si ndio collective responsibility hiyo?
 
Huyu jamaa ni tapeli hana lolote, anafanya kila njia kuwasifia CCM ili aendelee kuwepo (wasifanye faul wanazocheza sehemu zingine).
 
Mlikuwa hamjui kuwa Cheyo ni pandikizi la CCM? Kumbukeni maneno mazito ya msajili wa vyama aliyepita aliwahi kutamka kuwa anawajua wote waliopandikizwa na CCM ndani ya upinzani
 
Cheyo alikuwa na pesa nyingi, kabla ya kuingia kwenye siasa. Anachokiona sasa ni kwamba pesa zimepungua sana kwa sababu ya kutumia muda mrefu kwenye siasa na kwenye siasa nako kitubua kipo hatarini hivyo anatafuta njia ya kulinda kitumbua chake
 
Ndugu wadau, kwa mtizamo wangu, naona kwamba huyu mheshimiwa anajipendekeza mno kwa CCM/serikali.... Chukulia mfano wa matukio haya:....jinsi alivyocheza ngoma wakati wa ziara ya Rais na kumsifu sana, kana kwamba serikali imetimiza yote kwa wananchi, wakati ukweli ni kwamba hata jimboni kwake Bariadi Mashariki, hali ya kipato cha mwananchi wa kawida inasikitisha sana.......pia kitendo cha kupingana na wenzake wa kambi ya Upinzani Bungeni ktk kikao kinachoendelea,ambapo alifukuzwa toka kambi ya upinzani na pia Sitta leo, kuthibitisha adhabu hiyo kimezidi kunipa wasiwasi....
Kama mchambuzi wa siasa,nachukulia mambo haya anayofanya kama ni kutojiamini, woga, kujipendekeza, na kutaka CCM wamuonee huruma ili wasimpe upinzani wa dhati jimboni kwake...(nakumbuka katika moja ya mikutano yake ya kampeni, aliwahi kudai kwamba CCM ni wezi sana,waliwahi kukosea ktk kuiba kura kwenye kituo alichopigia kura yeye na familia yake na wakamuachia kura moja tu!!!). Kwa hali hii,nathubutu kusema Cheyo kageuza ubunge wake kama ajira na si mtumishi wa kweli wa wananchi,jimboni na hata taifani pia....Watanzania tuzidi kuamka,tuweze kutofautisha sasa wanasiasa njaa na wa kweli...

Haya ndo yanayotokea sasa Njaa nyingiiiii
 
Ameshindwa kukijenga chama chake hivyo nadhani anaongozwa na ule msemo '' IF YOU CAN'T BEAT THEM JOIN THEM'' Huku ni kujipendekeza na kuganaga njaa kwelkweli. Aibu yake milele
 
Hapana,

Cheyo aliwahi kunyang'anywa nyumba yake nzuri sana kule Masaki kwa kushindwa kulipa deni la benki ikapigwa mnada. Baada ya tafrani ile, Cheyo alipata udhamini ambao ulitolewa kwa nguvu ya Kikwete na kurudishiwa nyumba yake. Ni kama ambavyo Mrema alivyopatiwa matibabu huko India kwa udhamini wa Kikwete. Sasa wote wanalipa fadhila.

Siasa za Tanzania (na Sehemu kubwa ya Afrika) ni za ubinafsi sana. Maalim Hamad alipoahidiwa madaraka kule Zanzibar na kulipwa mafao yake ya kuwa Waziri Kiongozi, akasema mwafaka sasa sawa. Before that, alikuwa anasukuma watu kuandamana hadi wanauwawa huku yeye akitembea dunia nzima kusema kuwa Zanzibar hian demokrasi na wala haitambui serikali ya Karume.

Kumbuka tena kuwa Tambwe aliwahi kusema akirudi CCM basi atakauwa anammega mama yake, Mrema liwahi kusema hatarudi CCM kwani atakuwa anamze matapishi yake. lakini leoa unawaona wanafanya nini. Ni Ubinafsi tu
 
Cheyo alikuwa mwanasiasa kweli ila kwa sasa amepoteza maono. Chama chake muda wote kimabaki kuwa cha mfukoni. Na napendekeza chama kikishakosa sifa za kuwa cha kitaifa kwa muongo mmoja basi kifutwe. Hii itasaidia kuondoa uwezekano wa mtu kugeuzwa mamluki wa kukodiwa kwa kazi ya kushambulia mtu au vyama vilivyo makini kwa kisingizio cha kusajiliwa.
 
Cheyo alikuwa mwanasiasa kweli ila kwa sasa amepoteza maono. Chama chake muda wote kimabaki kuwa cha mfukoni. Na napendekeza chama kikishakosa sifa za kuwa cha kitaifa kwa muongo mmoja basi kifutwe. Hii itasaidia kuondoa uwezekano wa mtu kugeuzwa mamluki wa kukodiwa kwa kazi ya kushambulia mtu au vyama vilivyo makini kwa kisingizio cha kusajiliwa.

mkuu, hapa inamaanisha UDP sasa ni kama NGO fulani ya mheshimiwa Cheyo....
 
Back
Top Bottom