JOHN MNYIKA: Msimamo wangu wa sasa juu ya Kauli yangu bungeni!

Sidhani kama mtu anayeropoka hurudia mara mbili kwa msisitizo. Mnyika alikuwa anajua anachokifanya na Lukuvi na Ndugai wanalijua hilo na ndiyo maana wakaamua kumkatiza asiendelee kuwamwagia sumu. Kama Ndugai hakumpa nafasi ya kutoa maana ya kumwita Rais dhaifu ulitaka atolee wapi? ni dhairi atafanya hivyo nje ya bunge.

Nafikiri Ndugai ndiyo alikurupuka na sasa ataonekana yeye ndio dhaifu kuliko hata huyo rais anayemtetea. Tukianza kuwekeana mipaka ya nini kiongelewe tutakuwa na wabunge mazuzu wengi zaidi ya wale wa CCM ambao tayari ni loss kwa taifa.

Pamoja sana mkuu. Kama kuna mtu anadhani haya maneno huwa yanaropokwa, naomba akamkumbushe Spika kuhusu ule ushahidi wa Godbless Lema kuhusu kauli yake kuwa PM ni MUONGO. Mbona hawataki kuusikia mpk leo?

Kama Mnyika anao ushahidi kuwa Rais ni legelege na alitakiwa apewe nafasi ya kuelezea na sio kumwambia afute kauli, utafuta vipi UKWELI!
 
Kuja kutoa ufafanuzi nje ya mbunge haisaidii Mnyika angekiokoa chama chake kwa kutoa maneno ambayo yamepelekea adhabu

jiandaeni kugawa sanda, wananchi tumemuelewa jm, tunamuunga mkono na ni kweli jk ni dhifu kiafya mpaka kiakili. Ushahidi upo wazi.
 
Wewe PIMBI unafahamu namna ya kukopi tweet za watu au mnakopi tweet za ma coward wa magamba wanaolalamika kwa zito na kudha ni za zitto hebu cheki hii....

Zitto Zuberi Kabwe ‏@zittokabwe
Wanaomlaumu Mnyika hawakupata fursa kusikiliza alikuwa anasema nini? Rais anaruhusu vipi mpango wa maendeleo aliousaini ukiukwe?

Tatizo sio kukiukwa kwa mpango wa maendeleo ni neno Rais dhaifu yalimtoa nje na maneno mawili au moja nimesahau
 
Kuja kutoa ufafanuzi nje ya mbunge haisaidii Mnyika angekiokoa chama chake kwa kutoa maneno ambayo yamepelekea adhabu
Hakuwa na sababu yoyote ya kufuta kauri yake ambayo ndio ukweli halisi. Nampongeza sana Mnyika, kwani ameisimamia kauri anayoiamini. Bravo kamanda.
 
Lakini Mnyika si mnajua namna nyie CHADEMA mnavyochangia kwenye udhaifu wa Rais wetu? au mnajitoa akili, nyie ndio chanzo cha matatizo yote haya.
Kwani Mkuu CHADEMA wamekwapua fedha za EPA, wamekula rushwa ya radar, wameuza migodi ya dhahabu, wamaedidimiza uchumi wa nchi yetu kifisadi au kivipi??????

 
Kanuni za bunge ziko wazi kama wabunge wanataka mabadiliko ni bora wakaanza na kanuni badala ya kumlaumu spika ambaye amesoma kifungu cha adhabu ambacho kiko wazi.

Inawezekana itikadi za CCM na chadema zikatupeleka kwenye malumbano lakini ukweli uko wazi Mnyika alikuwa na nafasi moja tu ya haraka ya kuondoa maneno yake ili kifungu cha 64 (b) cha kanuni za bunge kisimwangukie.


utarekebishaje hizo kanuni na idadi ile ya magamba isiyoelewa nini maana ya utaifa imejaza nafasi bungeni. Hoja ya marekebisho ya kanuni itapitia wapi bila kupingwa kwa ushabiki wa magamba?
 
Nitatoa tamko la kina baadae kuhusu kilichotokea lakini kwa ufupi ubovu wa bajeti hii ni matokeo ya udhaifu wa Rais Kikwete, yeye ndiye aliyesaini Mpango wa Taifa wa miaka mitano kama Kiongozi Mkuu wa Nchi tena kwa wino mwekundu kama Amiri Jeshi Mkuu. Na yeye ndiye Mwenyekiti wa baraza la mawaziri, bajeti hii iliyoacha kuzingatia mpango wa Taifa imepita kwenye baraza alilloliongoza, pia kushindwa kutekelezwa kwa bajeti iliyopita ni matokeo pia ya udhaifu wa taasisi ya Urais.

*

Pia kwa mujibu wa Katiba Rais ndiye ambaye anapeleka bajeti bungeni, Waziri mwenye dhamana anapeleka tu kwa niaba. Rais amepewa mamlaka makubwa juu ya bajeti ibara ya 99 imeweka mipaka kuhusu mambo ambayo bunge lina mamlaka nayo huku ibara ya 90 inasema bunge likikataa bajeti rais ana mamlaka ya kuvunja bunge. Hivyo Rais Kikwete anapaswa kuagiza Waziri wa Fedha bajeti iondolewe irudi kwenye baraza la mawaziri ikafanyiwe marekebisho!



John Mnyika
19 Juni 2012
 
Ameshaanza kujitetea, hii ndio faida ya kuropoka. Sasa woga wa nini wakati umesha chafua hali ya hewa?

Usiwe kama vuvuzela unaimba kwa nguvu za anayekupuliza! Information is power! Wengi hatukujua kilijiri nini pale, kwa hiyo ufafanuzi ulihitajika! Nakupongeza mheshimiwa kwa kutoa ufafanuzi wa hoja yako. Mnyika ni Mpambanaji, na sijawahi kusikia Bondia mpambanaji akiogopa ngumi!
 
Kilichotokea leo bungeni kimefunua udhaifu mkubwa kwenye governance system ya Tanzania. Tuna mfumo wa kifalme ambao umetupa wanasiasa wanaodeka-deka kama watoto wa wadogo. Wabunge wako 'too sensitive' kwa mambo ambayo ni wazi tena mambo madogo kabisa. Na cha kushangaza kuna kanuni za kulea huu mfumo wa kudeka-deka!

Naibu Spika kasoma/Lukuvi wamesoma vifungu vinavyomfunga Mnyika kumuita rais kuwa ni dhaifu. Lakini bila hata ya kuacha amalizie kueleza alimaanisha nini hasa tayari hukumu imetolewa. Hivi mtu akisema wewe ni dhaifu hilo ni tusi? Kwa nini wasitoe hoja inayoonesha kuwa rais ni mtu makini?

Lakini kama ni kanuni ningetaka kujua Lukuvi na Naibu Spika walikuwa wapi siku ile Lowassa aliposema bungeni kuwa serikali imeshindwa kufanya maamuzi magumu? Nini maana ya hayo madai na yana tofauti gani na kauli ya Mnyika?

Mwisho, wabunge wa CHADEMA wamewazunguka wenzao wa CCM. Mara ya bajeti kusomwa tulisikia baadhi ya wabunge wakiipinga vibaya sana na kusema wako tayari kwa lolote! Leo hii wametikiswa na CHADEMA na haraka haraka wameonesha their true colours kwa kuiunga mkono bajeti! Huu ndio unafiki na Mnyika yuko sahihi kusema bunge la kipuuzi.
 
Back
Top Bottom