John chiligati vs wapinzani: Vita vya maneno!

Hiki ni kichekesho cha hali ya juu. Hivi kusema ukweli ambao unajulikana na kila Mtanzania anayefuatilia mambo ya siasa nchini kwamba CCM ni chama cha mafisafi ni kashfa!!!? :confused:

Mbona mafisadi waliojaa ndani ya chama hicho akina Mkapa, Lowassa, Msabaha, Mkono, Karamagi, Mramba, Rostam Azizi, Chenge na wengineo chungu nzima hawajachukuliwa hatua yeyote kuhusiana na ufisadi wao dhidi ya nchi yetu!? Safisheni chama ambacho mmeruhusu kichafuke kwa kukumbatia mafisadi vinginevyo ukweli ndiyo huo kwamba CCM si chama cha wakulima na wafanyakazi kama kilivyo miaka ya nyuma bali ni chama cha mafisadi.


BUBU, Bangusilo si fisadi kwani alishasema toka bungeni na kweli sasa inajulikana taratibu
 
Chiligati alichomaanisha ni kuwa;

1. Wana CCM wanaweza kukasirika na kuamua kulinda heshima yao kwa njia zisizo za amani.

Kwa mtazamo wangu, mawazo haya ambayo ni yake binafsi (sio ya wanaCCM) yanataka kuamsha ari ya wanaCCM ambao wala hawana haja ya kupigana na yeyote kuanza kufikiria kupigania chama. Kauli kama hizi ni kauli za hatari sana hasa kutoka kwa kiongozi wa kitaifa kama Chiligati (Waziri, NMEC, M-CC, Katibu Mwenezi CCM - Taifa, Mtu mzima, Baba mwenye familia na Mtanzania).

2. Amethibitisha CCM kutokuwa na nia yoyote ya kupambana na watuhumiwa wa ufisadi. Labda kwa utokutaka, kutokuwa na uwezo au sababu nyingine yeyote.

3. Zaidi ya hayo, anataka wote tushirikiane kulinda na kutetea maslahi ya mafisadi na kuacha kabisa kuwasumbua wanapokuwa wakitumbua rasilimali zetu. Tuwaache wale kwa amani na utulivu.

Mimi nina imani kuwa wana CCM wengi pia wamechoshwa na hali ya kisiasa nchini. Wamechoshwa na kashfa mbalimbali ambazo zinakikumba chama (CCM) na kwa vyovyote vile hawawezi kupambana kutetea ufisadi. Kama Chiligati haamini hivyo, aanze kuamrisha wanachama wake (Mil. 4 anaowasema) kupambana na yeyote anaetukana CCM kwa kulea mafisadi aone response itakuwaje. Ukweli ni kwamba, atagundua kuwa, asipochukua hatua za haraka, atapoteza wanachama hao karibu wote. Uthibitisho wa hili, ni malumbano ya viongozi wa chama hadharani. Chiligati anaweza kudhani kuwa malumbano yanayoendelea kati ya RA na HM ni yao binafsi. No way. Ni lalumbano yanayochomoza kutoka kwa wanachama na wasio wanachama wa CCM. CCM ya sasa itakuwa haina macho kama haioni hili kwa dimension hizi.

Kwa kuongezea tu, CCM haiwezi kuepuka lawama za ufisadi kama hazichukui hatua za haraka kupambana na ufisadi bila uoga na kwa kufuata sheria za nchi (zilizopo). Wahenga wanasema, "Samaki mmoja akioza, wote wameoza". Chiligati aondoe samaki waliooza kwenye kapu lake (CCM) kama anataka kapu lionekane halina samaki waliooza. Naamini kwa kufanya hivyo, ataona shutuma dhidi ya CCM zikififia na kuepusha hali ya upotevu wa amani aliyoizungumzia.

Sisi wote (ndani na nje ya CCM) tunasikitishwa na mwenendo wa chama na hatima ya nchi yetu. Take actions now.
 
Hiki ni kichekesho cha hali ya juu. Hivi kusema ukweli ambao unajulikana na kila Mtanzania anayefuatilia mambo ya siasa nchini kwamba CCM ni chama cha mafisafi ni kashfa!!!?

Mimi nadhani itaendelea kuwa kashfa as long as ufisadi huu utaendelea kuwa tuhuma tu kupitia magazeti na vyombo vingine vya habari. Something should be done to convict these people ili waonekane kuwa kweli ni mafisadi. Kama ni kwa kuwatuhumu mitaani tu, tutaendelea kucheza mchezo wa maneno hadi mwisho wa dahari
 
msishangae huyo ni Captain wa Jeshi sasa ameshazoea amri mambo ya siasa hayajui, sawa na katibu mkuu wake na Mwenyekiti wake wote ni wanajeshi kwa hiyo msishangae sana na kauli wanazozitoa
 
It seems uchochezi only comes from upinzani and media fratenity but not bureaucrats and ccm stalwarts. By his utterances Chiligati has failed the nation greatly
Mheshimiwa futa usemi wako kisha omba radhi wananchi. 2010 yaja
 
Ukweli usiopingika unajionyesha wazi sasa.
Huku kutawaliwa na Askari AMANI HAIWEZI KUWEPO, WAO NDIO WANAANZA VITISHO NA MATOKEO YAKE WATATUNYANYASA, kwa nini Hawa MA Captain, Luteni na Nanihii wasijiuzulu tuuuuu? Tangu lini askari akawa na uvumilivu wa Kisiasa ?
Mungu tunusuru na haya Ma amri amri yasiyo na kichwa wala miguu !
 
  1. Chiligati anaendeleza vitisho vilivyoanzishwa na Kikwete mwenyewe pale alipowatia mkwara viongozi wa zamani wa CCM.
  2. Kwa vile hao wazee wa CCM wamefunga midomo yao, mjumbe (Chiligati) sasa katumwa kuwanyamazisha Watanzania kwa kisingizio cha umwagikaji damu kwa sababu ya kelele za wapinzani (wananchi).
Ombi kwa Kikwete, kama hakubaliani na maneno ya Chiligati basi amuwajibishe ASAP, otherwise atuelezee ni yapi yaliyosemwa na wapinzani (wananchi) yatakayoharibu amani.
 
Hapo ni patamu.Wacha chama cha mafisadi wapandishe mzuka tupate pakuanzia.
Nadhani hata polisi wamechoka kutumiwa kama wehu.Watatusaidia kwenda ikulu
 
Wewe Chiligati do not threaten local mwananchi please! Some of your members may not be ready to support your assumed risk of mob justice against any party. What you could have said is personnally i see this and this and not that the 4 million members will be mobilised at ago!
It our responsibilities to ensure that leaders who have given priviledges of access national cake distribute it fairly and equally. As per now we all hear bad stories of mismanagement of funds among leaders and no actions taken! What can we say then as mwananchi and opposition leaders; THE PARTY IS FISADI GROUP
 
Recta;403518]Chiligati alichomaanisha ni kuwa;

1. Kwa mtazamo wangu, mawazo haya ambayo ni yake binafsi (sio ya wanaCCM)

- Sawa sawa ndugu, hapa tupo pamoja.

2.
Chiligati anaweza kudhani kuwa malumbano yanayoendelea kati ya RA na HM ni yao binafsi. No way. Ni lalumbano yanayochomoza kutoka kwa wanachama na wasio wanachama wa CCM. CCM ya sasa itakuwa haina macho kama haioni hili kwa dimension hizi.

- Malumbano yao ni part ya demokrasia makini ndio maana ni vizuri sana rais anavyofanya sasa yaani kunyamaza na kuachia yachukue mkondo wake.

3.
Wahenga wanasema, "Samaki mmoja akioza, wote wameoza".

- Hapana this one sio kweli, eti Chadema nzima inaunga mkono hoja ya Mheshimiwa Zitto ya taifa kununua mitambo mtumba ya Dowans? Misemo mingi ya wahenga haikubaliani na demokrasia makini na smarts politics za kisasa.

In general waziri yuko off line na hizi kinds of comments, hazileti umoja wa taifa wala kutoa ushuri wa kutatua tatizo sugu la ufisadi nchini.



Wiliam
 
msishangae huyo ni Captain wa Jeshi sasa ameshazoea amri mambo ya siasa hayajui, sawa na katibu mkuu wake na Mwenyekiti wake wote ni wanajeshi kwa hiyo msishangae sana na kauli wanazozitoa

Hakuna anaeshangaa maana watu huzidiana kuna wengine ni wanajeshi na wameshiriki vita katika mstari wa mbele au kwa kimombo wanaita Front Line ,nakumbuka nilipelekwa frontline katika jopo la mawasiliano ,wandugu amini usiamini kuna wakati mmoja wanajeshi wa Nduli wakikatisha njia nami nimejibanza juu ya mti tuli mivi kitambaani ,walipokatisha kwa dakika kumi na kuona wamefika mbali nikatoa mawasiliano na data kamili wapi kwa kuelekeza mizinga.Ndipo hapo tulipoanza kuingia Uganda maana ya kuangamiza kikosi hicho Cha uganda ambacho ndicho kilikuwa kikifanya doria katika sehemu za Tanzania ,mwenetu mmoja akiitwa federiki ,huyu alikuwa sio mwoga jambo ambalo lilimfanya apoteze maisha.kisa ,tulikuwa tumejichimbia kwenye misingi au mahandaki madogo madogo sasa ,tulifanya Chai ikabidi kupeleka chai handaki la pili ,tukamwambia asije akainua Kichwa ajaribu awezavyo kutambaa aloo ,hakukubali ikawa anakwenda kwa magoti kama mbuni hatujui risasi ilitokea wapi ikamvuruga kichwa.Ni hatari sana,mbali ya friendly fire maana tuliingia Uganda kwa mzunguko sasa tulipokutana ikawa kila mmoja amejaa woga wa kifo ndipo zikazuka risasi za hapa na pale lakini tulifanikiwa haraka haraka kupatiana data na kutulia.
Sasa Chiligati na wengine wasidhani watatishia watu na hivyo vyeo ,kuna makapteini fulani wakati tunarejea Uganda (Mi nilitokea Mtwara) sasa tulikuwa tumesheheni vitu vya ngawira kama TV maredio deki na mambo mengine ambayo mtu alimudu kuyabeba ,sasa kufika kituo fulani wakubwa wa pale wakataka kujionyesha kuwa kuwa wao ndio wenye dhamana na kututaka vile vitu vya ngawira tuviache pale na kurejea makwetu mikono mitupu ,aloo mbona ilikuwa mbinde maana tulimwambia wazi wazi kuwa bado tunanuka baruti na masikio hayajazibuka yameziba kwa sauti za machine gun na mizinga kama yeye na wengine watakaojaribu kuzuia vitu vyetu basi wajue itazuka vita mpya ,na usisikie kama angezidisha maneno kidogo tu angechezea shaba hapo hapo ,lakini alisituka na kuona bado macho yetu ni mekundu na nywele hazijachanwa tokea vianze vita masharubu yanashinda ya panya yanavyocheza ,na wakati tunazungumza hivyo bado vifaa na zana za kivita zipo mikononi ,mkubwa huyo hakuonekana tena sehemu hiyo hatujui alielekea wapi maana tulikuwa tumfanyizie ili ajue ,jeshi ni jeshi hata akiwa mdogo kwa cheo anapoamua kufanya ujeshi basi ni hatari na hakuna wa kumzuia ila kifo.
Chiligati cheo chako kisikufanye kutaka kuiharibu amani iliyokuwepo kwa hapa tulipo ni hatari kutishana.
 
Date::3/23/2009
Chama tawala chaambiwa kuacha kutisha wananchi kuhusu ufisadi

Na Mussa Juma, Same.
Mwananchi

KATIBU mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amemtaka katibu mwenezi wa CCM, John Chiligati, kuacha vitisho dhidi ya upinzani, akisema kuwa wataendelea kufichua ufisadi uliotanda kwenye chama hicho tawala.

Chiligati alivionya vyama vya upinzani kuwa visitumie ufisadi kama ngazi ya kujipatia umaarufu, huku akionya kuwa kuendelea kuishutumu CCM kunaweza kuhatarisha amani kwa sababu kama watu milioni nne watachukia (akimaanisha wana-CCM), hakutakuwa na amani.

Lakini Dk Slaa, mmoja wa wabunge ambao wamesimama imara katika kufichua na kupiga vita ufisadi, alisema hakuna ubishi kuwa CCM imeingia madarakani kwa kuchotewa fedha kutoka Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) na kama kinapinga, basi kiende mahakamani.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Dk Slaa wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika kata ya Hedaru na Makayanya wilayani Same na baadaye kukutana na waandishi wa habari.


Dk Slaa alisema Chadema ina ushahidi wa maandishi jinsi CCM ilivyokuwa inachotewa fedha za EPA kupitia kampuni ya Kagoda, hivyo kama inaona inapakwa matope, inaweza kwenda mahakamani kulalamika na sio kutoa vitisho kupitia vyombo vya habari.

"Tunamshangaa sana Chiligati na tunamuomba aache vitisho. Tunao ushahidi hadi muhtasari wa kikao kilichoongozwa na rais mstaafu kikielezea jinsi walivyokuwa wanajichotea fedha za EPA na pia ujumbe mfupi kutoka kwa katibu mkuu wa CCM kwenda Benki Kuu kuomba fedha hizo. Sasa wanaposema hawahusiki na EPA tunawashangaa," alisema Dk Slaa.

Dk Slaa alisema madai ya Chiligati kuwa wanachama milioni nne wa CCM wanaweza kukasirika kutokana na chama chao kuhusishwa na ufisadi ni ya kushangaza kwani ushahidi upo.

Alisema wanachama wa CCM hawawezi kukasirishwa na tuhuma hizo kwa kuwa ndio wahudhuriaji wakubwa wa mikutano ya Operesheni Sangara za Chadema na ndio wachangiaji wakubwa.

"Kwanza nchi hii ina watu zaidi ya milioni 40 hao, milioni nne wa CCM kwanza hawapo na hata waliopo pia hawapendi ufisadi wa watu wachache walio CCM," alisema Dk Slaa.


Wakati huohuo, Dk Slaa amemtaka Samuel Sitta kujivua nafasi zote za uongozi kwenye chama tawala, CCM ili aweze kutenda haki akiwa spika wa Bunge la Tanzania.

Dk Slaa alisema Spika Sitta ana nafasi nzuri ya kulisaidia taifa, lakini kutokana na kumezwa na CCM, amekuwa akitetea chama badala ya wananchi.

"Juzi nimesema posho za wabunge zipunguzwe, Sitta analalamika kuwa naingilia haki za bunge sasa leo nasema tunalipwa jumla ya Sh7 milioni kwa mwezi, acha posho za bungeni. Kweli hii ni halali kwa taifa masikini kama Tanzania," alihoji Dk Slaa.

Alisema malipo ya ya Sh135,000 kwa siku na ya Sh7 milioni kwa mwezi ni makubwa mno kwa wabunge kwa kuwa wafanyakazi wengi na Watanzania wanalipwa mishahara midogo na hivyo kuishi maisha duni.


"Mamilioni haya ya fedha kwenda mifukoni mwa watu ni aibu kwa nchi. Chadema tunasema hapana! Fedha hizi ziende katika masuala ya kusaidia jamii na kuongeza mishahara ya walimu, polisi, mahakimu na watendaji wengine," alisema Dk Slaa.
 
Enhee hapo nilisema Mtawala CCM anatumia wachache katika vyombo vya dola ,usalama ,polisi ,na jeshi katika kuhakikisha wanalipwa unono ,hawa ni viongozi wachache katika vyombo hivyo ambavyo hutumiwa wakiwa kama manokoa wanaotoa amri kwa FFU,polisi kwenda kupambana na kambi za upinzani ,kuvunja mikutano yao,kuwanyima vibali vya mikutano na maandamano ,na hata hujuma za kuwapiga wapinzani wakidai wao ni wanachama wa CCM au wakereketwa tunao janjaweeds hawa hushakizwa kupiga kwa kutumia vitu vyenye ncha kali na hakuna anaekamatwa wala kuhojiwa.
Sasa hawa hulipwa kula kwa kupikiwa ugali na maharage na kupewa vitu vikali vya kuwatoa katika ubinadamu na halafu huamrishwa kwenda kazini kazi ambayo ni kushambulia raia wanaojiandikisha,wanaoandamana kudai haki zao za msingi.watu hawa hawajui wale wanaowaamrisha kuwa wanalipwa mishahara ya mamilioni kwa kwa mwezi wakati wao wakiishia kulala kwenye mahema na kuendesha baiskeli wakati wenzao wakiendesha magari ya kifahari.
Mishahara ya polisi na jeshi si lolote si chochote ukilinganisha na hawa wabunge na mawaziri, milioni saba kwa mwezi ,tuna wabunge wangapi ,kuna vikao vingapi ndio hata wasomi wanakimbilia huko.
Kwa kweli huu ni ufisadi mwengine tunataka upinzani upinge kwa nguvu zote mishahara inayotolewa hapo kwani ndio inazorotesha uwajibikaji wa wa Bunge na wengine kubakia kupiga makofi na kuunga mkono ,bila ya kuelewa wanachokiunga mkono kama kina faida au maafa kwa jamii.
Na zaidi hawa polisi wanaokuwa mstari wa mbele kuinkingia kifua CCM kila sehemu,ukweli ndio huo mmeelezwa kuwa yule mnamkingia kifua anamaslahi makubwa kibinafsi kuliko mnavyofikira kuwa mnalinda amani kumbe mnalinda wezi.
Wabunge wa upinzani inafaa wajiuzulu mara moja kupinga mshahara huo ili kuilazimisha kuwekwa kiwango kipya.ila ikiwa mnapanda kwenye viriri na kurapu mtakuwa hamna jipya ,kama tunavyowambia wanaopinga mafisadi ndani ya CCM wajitoe kwenye Chama Cha CCM na nyinyi mnaopinga mishahara mikubwa mjitoe katika kupokea mishahara hiyo,ndio tutajua kuwa kweli mmeamua kuwagombani wananchi na kupata faida kwa jamii.
 

"Juzi nimesema posho za wabunge zipunguzwe, Sitta analalamika kuwa naingilia haki za bunge sasa leo nasema tunalipwa jumla ya Sh7 milioni kwa mwezi, acha posho za bungeni. Kweli hii ni halali kwa taifa masikini kama Tanzania," alihoji Dk Slaa.

Alisema malipo ya ya Sh135,000 kwa siku na ya Sh7 milioni kwa mwezi ni makubwa mno kwa wabunge kwa kuwa wafanyakazi wengi na Watanzania wanalipwa mishahara midogo na hivyo kuishi maisha duni.



Dr. Slaa tunakusikia tena kwa sauti kubwa sana. Mshahara wa TShs. 7 millioni kwa maoni yangu sio nyingi za kutisha kwa kazi ya ubunge, lakini hizo posho za TShs. 135,000 sielewi kabisa kwa nini ziwepo ikiwa kazi ya wabunge ni vikao vya kujadili na kutunga sheria.

Hii ni sawa na kuwalipa waalimu posho kwa ajili ya kusimamia majaribio (test) za wanafunzi.
 
Dr. Slaa tunakusikia tena kwa sauti kubwa sana. Mshahara wa TShs. 7 millioni kwa maoni yangu sio nyingi za kutisha kwa kazi ya ubunge, lakini hizo posho za TShs. 135,000 sielewi kabisa kwa nini ziwepo ikiwa kazi ya wabunge ni vikao vya kujadili na kutunga sheria.

Hii ni sawa na kuwalipa waalimu posho kwa ajili ya kusimamia majaribio (test) za wanafunzi.
Milioni saba sio nyingi ,ndugu hebu fikiria tena Unazungumzia Tanzania sio Ulaya.
Milioni Saba katika Nchi ya mwisho kwa Umasikini unasema sio nyingi kwa mtu anaekaa na kupiga makofi tu kushangilia wengine,wakati mshahara wa daktari anaetibu magonjwa ya hatari na kuhatarisha afya yake haukatizi huko ,polisi anaepigwa na jua pale getini na kutafunwa na mbu usiku kucha akiwa mlinzi wa Mkuu wa mkoa hata haunusi huko ,mwalimu aneota masuguru kwenye vidole kwa kushika chaki kila siku kwa kumfundisha raisi mtarajiwa haoni ndani ya mshahara huo na ambae hulipwa bakora na DC,wanajeshi wanaochukua dhamana ya nchi na kuishi mbugani muda mwingi wa maisha yao hawakaribii kabisa huko kwenye milioni saba na akimaliza unapishana nae njiani anaendesha basikeli na kakuvalia yeboyebo,halafu unasema milioni saba ni vijisenti tu ,aloo wewe inaonyesha hujafika hapa nyumbani miaka mingi ukaona ni jinsi gani watu wanateseka na maisha ,wakati mbunge na viongozi wanatembelea magari ya kifahari ,akina mama wajawazito wanaswekwa kwenye chumba kimoja hata wakiwa mia watabanana humo humo,na kuzalishana humohumo ,hivi tuna wabunge wangapi ,zaidi ya mia mbili ni milioni ngapi hizo ,hivi ikiwa wabunge wataamua nusu ya mishahara yao ipelekwe kwenye kujenga vituo vya akina mama kutakuwa na kosa,mbona upo na mawazo ya kudharau sana, milioni saba si fedha kidogo kwa Tanzania ni fedha nyingi sana kuipokea kila mwisho wa mwezi nafikiri ni kama dola 2000 kwa mwezi ,hiyo ndugu si fedha ndogo kwa Tanzazia kuipokea kila mwezi mbali ya posho ,kwa miaka mitano 2000 x 12 x 5 mbunge posho tu inamuendeshea maisha yake.
 
Dr. Slaa Heshima Mbele,

Ila kupiga kelele na kujibishana kati yenu hakusaidii sana,ila tunachotaka ni mikakati ya maendeleo na nini kifanyike kuwaondoa mafisadi.Mmpeza sauti sana ila usanii bado uko [pale pale],na hatujaona cha maana ambacho wamefanya.

Mie hata sijui kesi za watu wa EPa zinaendeleaje?

We need a new Move while we are waiting 2010
 
Sijui Dr. Slaa anapokea mshahara na posho yake yote au anarudisha cheki serikalini?
 
Sijui Dr. Slaa anapokea mshahara na posho yake yote au anarudisha cheki serikalini?

Siku hizi hawarudishi kwa culprit, wana donate kwenye charity.

Kwa hiyo swali liwe Dr. Slaa ana donate kwenye causes hicho kilichozidi? Au anafanya maigizo tu?

All in all, ana point muhimu sana na hata kama ana donate au ha donate ni muhimu kuwa na standard itakayo apply kwa wabunge wote, kitu ambacho Dr. Slaa anakipigania.
 
Sijui Dr. Slaa anapokea mshahara na posho yake yote au anarudisha cheki serikalini?
Dr kaniacha hoi.....eti leo miaka mi4 ndio anasema posho zao nyingi is he kidding me?

yeye angetuambia yeye hayo mapesa yote anaona ni ubadhirifu anazipeleka sehemu za maendeleo lakini anazichukua tu huku analalamika ati nyingi......wabunge bwana..
 
Back
Top Bottom