Hmaster
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 346
- 86
Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Filauni! Nilikuwa na mpangaji mwenzangu katika nyumba moja Dar. Jamaa alikuwa ni rafiki yangu sana na alitokea kuniamini sana kwani alikuwa ananihadithia mambo mengi sana. Hata akipata utata wa jambo furani hakusita kuniomba ushauri kwa vile hata kielimu mimi nipo juu kiasi. Pamoja na kazi nzuri aliyonayo huyu jamaa sikumuona hata siku moja akiwa bize na wakinadada zaidi ya kutaniana nao tu hapa na pale. Akirudi kazini, alitumia muda mwingi kutazama tv, kupika, kuoga na hatimaye kulala. Mimi nilimsifia sana kwa hali hiyo si unajua mtu kujiheshimu. Kutokana na hali hiyo niliogopa hata kumweleza miadi yangu ya kujirusha kwa kuogopa jamaa ataniona namna gani.
Kuna siku tulitoka kwenda kutazama mechi ya mpira kiwanjani na wakati wa kurudi mi nilimueleza mwenzangu huyo kwamba atangulie home kwani mimi nilikuwa na miadi na mtu hivyo namsubiri baa furani. Jamaa akanieleza kwamba naye angenifuata kwani ana mazungumzo na mm. Tukaenda na tulipokuwa hapo alinipa A to Z ya hali yake tangu apate ujana. Jogoo wake anawika akiwa peke yake lakini akiwa na mtetea anakaa kimya hata siku nzima. Ndo maana akaachana na mitetea kwa kuogopa kudhalilika. Akaniomba ushauri, nikamwambia aende kwanza hosp. Akaenda akatibiwa kln tatizo bado. Huku na huku lakini wapi na umri wake sasa ni miaka 39. Mwisho hata kunieleza maendeleo yake akawa haniambii na akawa kama ananikwepa kwa aibu na mwisho akahamia sehemu nyingine na mawasiliano yakafa.
Jambo la kushangaza ni kwamba katika kipindi cha miaka takribani mitatu hivi tuliyopotezana tulikutana maeneo flani akiwa na mwanamke akiwa na mtoto mgongoni huku na yeye kamshika mwingine na kuniambia huyo ni mke wake na hao ni watoto wake. Nikashangaa sana na mwisho nikawapongeza, sikuweza kumuhoji kitu. Je inawezekana alipona au "kapewa alee"
Kuna siku tulitoka kwenda kutazama mechi ya mpira kiwanjani na wakati wa kurudi mi nilimueleza mwenzangu huyo kwamba atangulie home kwani mimi nilikuwa na miadi na mtu hivyo namsubiri baa furani. Jamaa akanieleza kwamba naye angenifuata kwani ana mazungumzo na mm. Tukaenda na tulipokuwa hapo alinipa A to Z ya hali yake tangu apate ujana. Jogoo wake anawika akiwa peke yake lakini akiwa na mtetea anakaa kimya hata siku nzima. Ndo maana akaachana na mitetea kwa kuogopa kudhalilika. Akaniomba ushauri, nikamwambia aende kwanza hosp. Akaenda akatibiwa kln tatizo bado. Huku na huku lakini wapi na umri wake sasa ni miaka 39. Mwisho hata kunieleza maendeleo yake akawa haniambii na akawa kama ananikwepa kwa aibu na mwisho akahamia sehemu nyingine na mawasiliano yakafa.
Jambo la kushangaza ni kwamba katika kipindi cha miaka takribani mitatu hivi tuliyopotezana tulikutana maeneo flani akiwa na mwanamke akiwa na mtoto mgongoni huku na yeye kamshika mwingine na kuniambia huyo ni mke wake na hao ni watoto wake. Nikashangaa sana na mwisho nikawapongeza, sikuweza kumuhoji kitu. Je inawezekana alipona au "kapewa alee"