Hebu fikiria kwamba, umegundua kwamba, mumeo ameishiwa kabisa nguvu za kiume. Bado umri wenu ni ule wa kati, mnahitaji bado kushiriki jambo hilo au pengine mnahitaji hata watoto bado. Je, kama ni wewe ungefanyaje?
Kama ulimpenda kwa dhati lazima utavumilia ili mtafute ufumbuzi wa tatizo hilo kwani kama alizaliwa na nguvu za kiume basi lazima solution yake ipo. Ila kama ndio hamkupendana kwa dhati ndio hapo kasheshe kila siku tunaambiwa mke/mume mwema hutoka kwa bwana tuombe na kusubiri na atakuletea wa kufanana nae na ukimpata wa kutoka kwa bwana hata uwe na tatizo la aina gani atakuvumilia tu.
Mimi naamini ndoa ni zaidi ya tendo japo sipingi kwamba sio muhimu. Kwa kuwa ni mume wangu nitamsupport na kumsaidia asijisikie vibaya. Nitamuhakikishia kuwa mapenzi yangu kwake ni unconditional hivyo asiwe na wasiwasi. Nitamshauri na kumsindikiza kuwaona wataalamu (madaktari) kama atahitaji. Kwa kifupi mapenzi yangu kwake yataongezeka zaidi na zaidi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.