Jobs At Kibacha Safaris

mummyjimmy

Member
May 13, 2011
13
3
Habari wadau,

Jamani kuna kazi ziliadvertisiwa last week za udereva kibacha safari's na one of my relative aliapply but cha kushangaza wamemtumia email eti amechaguliwa kufanya nao kazi bila kufanyiwa usaili wa vitendo kutokana na CV yake imejitosheleza. Alafu eti anatakiwa kulipa 30,000/- kwaajili ya training ya jinsi ya ku - attend wageni through Tigo Pesa na wakishapata uo mshiko ndo watamwelekeza kwa simu offici zao zilipo.

my question is kuna mtu yeyote anaeijua hii kampuni au ni watu wanataka kula pesa za maskini jamani.
 
Mh jamani hili nalo linashangaza na kustua kidogo.
Sasa elfu 30, za nini na mtu anashida hana kazi?
Kaka mimi sijawahi kusikia hii company lakini jaribu ku search kwenye google na kisha fuatilia na ikiwezekana mpigie mkubwa wao wa hiyo company
Pole sana inauma
 
Hautaji kuwa genius kujua kuwa huo ni utapeli. Najua watu wanahangaika muda mrefu kutafuta kazi lakini hiyo isiwe sababu ya kutotumia akili katika kutambua genuine employers na matapeli wa mjini.

Achana nao hao. Kama wao ni waadilifu ilibidi waweke address yao wazi.
 
kwa haya mambo haya ya ajira tuwe makini zaid ya tunapofanya mapenzi kwa sasa.
 
Weka namba yake ya simu tukusaidie kuchecki na kujua ukweli
 
Naamini kuwa ni matapeli coz kwanzan deadline ilitakiwa kuwa 20th June but kwa email yao wanasema tulipe kabla ya 13th June na iyo training inaanza 18th June. How come usaili ufanyike kabla ya deadline.

jamani ndugu zangu tuwe makini sana na hizi kazi tusije tukapoteza vijihela vyetu vigodo tulivyonavyo kwa kuwanufaisha wengine.
Namba yao ni 0718 910458 mwenye kutuma hizo barua anaitwa J Pima.
 
Mh jamani hili nalo linashangaza na kustua kidogo.
Sasa elfu 30, za nini na mtu anashida hana kazi?
Kaka mimi sijawahi kusikia hii company lakini jaribu ku search kwenye google na kisha fuatilia na ikiwezekana mpigie mkubwa wao wa hiyo company
Pole sana inauma

Je ofisi ya hawa ipo wapi Arusha.
 
Mh jamani hili nalo linashangaza na kustua kidogo.
Sasa elfu 30, za nini na mtu anashida hana kazi?
Kaka mimi sijawahi kusikia hii company lakini jaribu ku search kwenye google na kisha fuatilia na ikiwezekana mpigie mkubwa wao wa hiyo company
Pole sana inauma

Kama Kibacha wa Arusha usitume pesa ni wezi wakubwa hao nawafahamu ni kikundi cha watu flani hivi wala usijiangaishe kabisa.
 
Usijaribu kutuma hiyo pesa...utalia!! Huu mchezo umeingia kwa kasi sana hapa bongo!! Hata wale wa Songea Uranium ni wezi wakubwa!! Dont send any coin to them
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom