JK: Wafanyabiashara chanzo cha ufisadi

mwanaizaya

Senior Member
Apr 26, 2008
133
1
JK: Wafanyabiashara chanzo cha ufisadi
Na Mwandishi Wetu


RAIS Jakaya Kikwete, amepasua ukweli mbele ya wenye viwanda, akisema kuwa, rushwa kubwa nchini zina mkono wa baadhi ya wafanyabiashara.


Kutokana na hali hiyo, Rais alilitaka Shirikisho la Wenye Viwanda nchini (CTI), kushirikiana na serikali kupambana na rushwa nchini.


Akizungumza juzi usiku wakati wa utoaji wa Tuzo bora ya Rais kwa Wazalishaji Bora, Rais Kikwete alisema, hakuna biashara inayoweza kudumu katika mazingira ya rushwa na ukiukaji wa sheria.


Rais Kikwete ambaye alizungumza mbele ya wenye viwanda akiwemo Mwenyekiti wa CTI, Reginald Mengi, alisema, wakati mwingine katika kutafuta upendeleo wa ushindani ni wafanyabiashara ndio wanaochochea rushwa.


Alisema, kama wafanyabiashara wataamua kuacha kupenda upendeleo na upindishaji sheria, basi rushwa kubwa zitakoma.


"Lakini, pia na wenyewe mjitazame katika shughuli zenu. Na nyie mnalalamikiwa kwa rushwa katika ajira na kupata shughuli ya kufanya kama vile kupata uwakala, wahusika kuomba na kupokea rushwa," alisema Rais Kikwete.


Rais alisema: "Kama mwombaji ni msichana, basi huombwa penzi ndipo apate kazi au shughuli."


Alisema, imezoeleka kusemwa kwamba, rushwa ni adui wa haki; na akasisitiza kuwa sheria za nchi ziheshimiwe katika mienendo ya biashara na wafanyabiashara.


Alisema kuwa, serikali inatambua na kuridhishwa na mchango mkubwa wa sekta binafsi na umuhimu wa sekta ya viwanda katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya taifa.


Alisema, serikali inajivunia uamuzi wake wa kuifanya sekta binafsi kuwa injini ya ukuaji uchumi, kwani imeonyesha mafanikio ambayo ni kufanya ukuaji wa haraka wa Pato la Taifa kwa wastani wa asilimia sita kwa mwaka katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.


Rais aliongeza kuwa, mchango wa sekta ya viwanda katika pato hilo umeongezeka kutoka asilimia 17.2 mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 18.4 mwaka 2007, lakini akasema bado haridhishwi na mchango wa sekta hiyo katika pato la taifa.


"Vile vile, pamoja na kwamba mchango wa Pato la Taifa umeongezeka katika mauzo ya nje kutoka asilimia 5.3 mwaka 2005 hadi kufikia asilimia 8.3 mwaka 2007, mchango huo ni mdogo mno ukilinganisha na uwezo wa sekta hii," alisema Rais Kikwete.


Rais alisema kuwa ni vema pia watu wakachangamkia soko katika Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), na kuongeza: "Leo mkulima wa machungwa kule Muheza, anaweza kupakia machungwa yake katika Fuso na kupeleka Mombasa tu, tofauti na kwamba apeleke Marekani itakuwa ni matatizo, mambo ya kupakia. Sisi tumefungua mipaka, fanyeni biashara."


Rais alikabidhi tuzo mbalimbali kwa viwanda katika sekta tofauti huku Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), ikiibuka mshindi wa jumla
 
mara watu wasiogope kuitwa mafisadi mara chanzo cha ufisadi tuchukue lipi tuache lipi? Au ameisha sahau?
 
Rostam ajikanganya

2008-07-14 09:36:06
Na Simon Mhina


Mbunge wa Igunga (CCM), Bw. Rostam Aziz, ameibuka jijini Dar es Salaam na kutoa shutuma za kujikanganya baada ya kuwageukia na kuwatuhumu baadhi ya wanasiasa na wafanyabiashara kuwa wanamuonea wivu.

Aidha, Mbunge huyo, alisema hana ugomvi na Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT) ila viongozi wa kanisa hilo wanatumiwa na kushinikizwa na watu hao kumkana

Bw. Rostam alikuwa akijibu taarifa ya KKKT iliyokana kumsafisha na tuhuma za ufisadi na kutaka mtu mwenye ushahidi kuwa yeye ni fisadi autoe hadharani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Bw. Rostam, alisema taarifa ya KKKT haikutokana na matakwa ya viongozi wa kanisa hilo, bali shinikizo la watu wanaomuonea wivu kibiashara na kisiasa.

``Ili kutenda haki na kujua ukweli wa mambo, natoa changamoto kwa yeyote mwenye ushahidi wa madai ya ufisadi dhidi yangu awasilishe ushahidi huo katika vyombo vya sheria vinginevyo wafunge midomo,`` alisema.

Aidha, alisema kundi hilo limeungana na kundi lingine la wanasiasa ambao wanadhani kwamba yeye aliwakwamisha kupata nafasi fulani serikalini.

Akifafanua, Bw. Rostam alisema utajiri wake na fedha alizonazo ni \'safi\' na wala sio \'chafu\' kama ilivyoripotiwa.

Alisema fedha na biashara zake, ni matokeo ya biashara ya familia yake aliyoirithi toka vizazi kadhaa vya ukoo wao vilivyopita.

Alisema biashara anazomiliki zilianza mwaka 1852 huko Tabora na amezirithi toka kwa mababu zake.

Bw. Rostam alisema hakwenda katika kanisa hilo kujisafisha na wala hakuvamia, bali alikaribishwa.

``Nilikwenda katika sherehe hizo kwa mwaliko na wala sikujialika (kama KKKT walivyosema) siku ya sherehe, mzee wa Kanisa alikuja kunichukua nyumbani kwangu, nilipokelewa Ofisi za Kanisa nikajaza kitabu cha wageni. Nilifanya mazungumzo kadhaa na uongozi na baadaye nikapelekwa kwenye uwanja wa tukio,``alisema.

Aliwataka viongozi wa Kanisa la Kinondoni kupuuza kile alichokiita chuki, wivu na ubaguzi.

Alisema ni kweli siku za nyuma hakuwa na tabia ya kukutana na waandishi wa habari kwa vile mambo yake hataki yatangazwe na akasisitiza kuwa, mara baada ya mkutano huo wa jana, ataendelea na msimamo wake wa kutofanya mikutano kama hiyo.

Nimeona haja ya kuitisha mkutano huu kufuatia mwendelezo wa kampeni maalum ya kujaribu kunichafulia jina, hadhi na heshima yangu mbele ya jamii.

Alidai Mchungaji Christopher Mtikila pia alitumiwa na kikundi hicho kulishinikiza Kanisa kutoa taarifa ya kumkana.

Hata hivyo, alisema ameamua kujibu baadhi za hoja za Mtikila kwa vile aliligusa kanisa, vinginevyo angenyamaza kwa vile Mtikila hana hadhi ya kujibiwa na yeye (Rostam).

``Nataka niweke jambo moja wazi kwamba kama Mtikila angenituhumu mimi tu, nisingeitisha mkutano huu kwa vile hastahili heshima ya kujibiwa na mimi kilichofanya nichukue nafasi hii ni kwa vile amelitia msukosuko Kanisa ili lione kuwa limefanya dhambi kunikaribisha,`` alisema.

Bw. Rostam aliwaomba waumini wa KKKT Kinondoni wamwalike tena kwa vile hana kinyongo nao na atakwenda.

Alisema amekuwa akishirikiana na Makanisa mengine kama Moravian, Pentekoste na Katoliki.
Hata hivyo, akijibu tuhuma hizo Mchungaji Mtikila alisema ameshangazwa na madai hayo.

``Amesema alinipa milioni tatu? Kwa hiyo alinipa fedha hizo ili ninyamaze kusema kuwa yeye sio fisadi. Amenipa pointi nzuri sana, kwamba kumbe mimi siwezi kuhongwa wala kununuliwa, ninaweza kupewa milioni tatu, halafu nikabaki na msimamo wangu,`` alijigamba
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom