kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,307
- 12,602
Kuna watu walidhani kuwa Rais Kikwete ni dhaifu, hii ilikuwa wrong interpretation, mambo aliyoyafanya JK ni makubwa matupu na ya hatari kwa Rais yeyote kuyafanya. Kuyataja machache ni pamoja na kukubali katiba ya nchi ifanyiwe mabadiliko, utekelezaji wa zoezi la vitambulisho vya taifa, kuimarika kwa demokrasia nchini, kujenga barabara nchi nzima, kufukua mikataba ya madini, kubadilisha baraza la mawaziri na viongozi wengine mara kadhaa, ujenzi wa UDOM, n.k. mambo yote haya yalimshinda Nyerere, Mwinyi na Mkapa enzi zao, kilimo kwanza. Kigoma enzi hizo ulidhani haiko Tanzania.
Ila watu wanasema ni dhaifu kwa sababu wananchi wanapenda kwa sasa kiongozi mwenye sifa ya udikteta kidogo ili kunyoosha makosa yaliyofanywa na marais na viongozi wetu waliotangulia. Ndio maana watu wanampenda Dk. Magufuli na bomoabomoa yake ya waliojenga pasipo, Prof. Tibaijuka, Mh. Lyatonga Mrema (enzi zake), Mh. Sokoine (enzi zake), Mh. Amina Chifupa (enzi zake)
Mwaka 2005, JK alipata kura nyingi sana kutoka kwa wananchi wote bila kujali itikadi zao na kupata urais. Sababu kuu ya kupata kura nyingi wakati ule zilikuwa zilezile za wananchi kupenda kiongozi ambaye ni dikiteta atakayeweza kusawazisha maovu ya viongozi waliopita. JK alipata kura nyingi kwakua alikuwa anaonekana ni kijana, ni mwanajeshi, na ambaye alikuwa anachukia kuuzwa na kubinafsishwa kwa mashirika ya umma na nyumba za serikali. Ukweli huu ulichagizwa na kaulimbiu yake ya Ari Mpya, Nguvu mpya na Kazi Mpya aliyokuja nayo. Hivyo, wananchi walidhani Kikwete kwakutumia sifa hizo akipata urais angefanya kamatakamata ya mafisadi wote (wanafahamika), angerudisha mashirika na nyumba zilizouzwa na Mkapa, angerudisha open spaces zote nchini, angeimarisha michezo nchini kwakuwa ni kijana na mpenda michezo, na hata wanajeshi wenzake wangenufaika zaidi na ujio wake. Kilichotokea, baada ya JK kupata urais ile kamatakamata iliyotarajiwa na waliomchagua haikuonekana kabisa, utadhani hajawahi kuwa mwanajeshi wala mgambo hata siku moja. Na alikuwa anawakataza hata akina Magufuli na Makamba (mkuu wa mkoa) wasiwe madikteta kwa watu waliojenga kinyume na taratibu. Alitumia pesa za wananchi kwa kuwalipa watu wachache waliopatwa na mafuriko kwa kujenga sehemu za mabondeni(zisizoruhusiwa) na kugharamia wamachinga waliokimbia makusudi kutoka wilayani kuja mijini badala ya kutumia pesa hizi katika maendeleo ya ujumla ya wananchi kama kuongeza mishahara ya watumishi, madawati, vitanda hospitalini n.k. Wananchi walikufa moyo zaidi na JK na CCM yake hadi leo hii. Hali hii ya kukata tamaa ilionekana kwenye uchaguzi wa 2010 wakati kura zake ziliposhuka kwa kiwango cha kutisha.
Lakini wananchi wanataka kiongozi dikteta wakati katiba, kanuni na sheria zetu hazimruhusu Rais kuwa dikteta, rais bora ni yule anayetekeleza matakwa ya sheria hata kama sheria hiyo ni mbaya. Ndiyo maana JK ameridhia katiba iandikwe upya ili wananchi tuamue tunataka rais wa namna gani pia.
Nchi hii ni kubwa sana kuliko za wenzetu, ina hitaji wanajeshi wengi, walimu wengi, barabara ndefu na nyingi, nguzo nyingi, nyaya nyingi, transfoma nyingi za umeme, vituo vingi vya polisi, shule nyingi, zahanati na hospitali nyingi na watumishi wengi, n.k. Haya yote yanahitaji pesa nyingi za kugharamia huduma mbalimbali.
Tupeane ushauri kama taifa kuhusu maswali yafuatayo: Hivi wabongo tulipane bei gani kama mishahara (elimu, uzoefu)? Vyanzo vyetu vya pesa viwe vipi? Nani alipe kodi na nani asamehewe? Tutampataje kiongozi safi? Tumfanye nini kiongozi anayeiba mali yetu kwa njia yoyote ile? Tutajuaje kama hela ya kulipana ipo hau haipo hazina? Anayekwepa kodi tumfanyeje? na mwishowe ni nini vipaumbele vyetu mwaka huu, ujao, n,k?
Haya ndo maswali yatakayompa kiongozi yeyote ujasiri wa kutenda bila kulazimika kutumia utashi wake binafsi.
Ila watu wanasema ni dhaifu kwa sababu wananchi wanapenda kwa sasa kiongozi mwenye sifa ya udikteta kidogo ili kunyoosha makosa yaliyofanywa na marais na viongozi wetu waliotangulia. Ndio maana watu wanampenda Dk. Magufuli na bomoabomoa yake ya waliojenga pasipo, Prof. Tibaijuka, Mh. Lyatonga Mrema (enzi zake), Mh. Sokoine (enzi zake), Mh. Amina Chifupa (enzi zake)
Mwaka 2005, JK alipata kura nyingi sana kutoka kwa wananchi wote bila kujali itikadi zao na kupata urais. Sababu kuu ya kupata kura nyingi wakati ule zilikuwa zilezile za wananchi kupenda kiongozi ambaye ni dikiteta atakayeweza kusawazisha maovu ya viongozi waliopita. JK alipata kura nyingi kwakua alikuwa anaonekana ni kijana, ni mwanajeshi, na ambaye alikuwa anachukia kuuzwa na kubinafsishwa kwa mashirika ya umma na nyumba za serikali. Ukweli huu ulichagizwa na kaulimbiu yake ya Ari Mpya, Nguvu mpya na Kazi Mpya aliyokuja nayo. Hivyo, wananchi walidhani Kikwete kwakutumia sifa hizo akipata urais angefanya kamatakamata ya mafisadi wote (wanafahamika), angerudisha mashirika na nyumba zilizouzwa na Mkapa, angerudisha open spaces zote nchini, angeimarisha michezo nchini kwakuwa ni kijana na mpenda michezo, na hata wanajeshi wenzake wangenufaika zaidi na ujio wake. Kilichotokea, baada ya JK kupata urais ile kamatakamata iliyotarajiwa na waliomchagua haikuonekana kabisa, utadhani hajawahi kuwa mwanajeshi wala mgambo hata siku moja. Na alikuwa anawakataza hata akina Magufuli na Makamba (mkuu wa mkoa) wasiwe madikteta kwa watu waliojenga kinyume na taratibu. Alitumia pesa za wananchi kwa kuwalipa watu wachache waliopatwa na mafuriko kwa kujenga sehemu za mabondeni(zisizoruhusiwa) na kugharamia wamachinga waliokimbia makusudi kutoka wilayani kuja mijini badala ya kutumia pesa hizi katika maendeleo ya ujumla ya wananchi kama kuongeza mishahara ya watumishi, madawati, vitanda hospitalini n.k. Wananchi walikufa moyo zaidi na JK na CCM yake hadi leo hii. Hali hii ya kukata tamaa ilionekana kwenye uchaguzi wa 2010 wakati kura zake ziliposhuka kwa kiwango cha kutisha.
Lakini wananchi wanataka kiongozi dikteta wakati katiba, kanuni na sheria zetu hazimruhusu Rais kuwa dikteta, rais bora ni yule anayetekeleza matakwa ya sheria hata kama sheria hiyo ni mbaya. Ndiyo maana JK ameridhia katiba iandikwe upya ili wananchi tuamue tunataka rais wa namna gani pia.
Nchi hii ni kubwa sana kuliko za wenzetu, ina hitaji wanajeshi wengi, walimu wengi, barabara ndefu na nyingi, nguzo nyingi, nyaya nyingi, transfoma nyingi za umeme, vituo vingi vya polisi, shule nyingi, zahanati na hospitali nyingi na watumishi wengi, n.k. Haya yote yanahitaji pesa nyingi za kugharamia huduma mbalimbali.
Tupeane ushauri kama taifa kuhusu maswali yafuatayo: Hivi wabongo tulipane bei gani kama mishahara (elimu, uzoefu)? Vyanzo vyetu vya pesa viwe vipi? Nani alipe kodi na nani asamehewe? Tutampataje kiongozi safi? Tumfanye nini kiongozi anayeiba mali yetu kwa njia yoyote ile? Tutajuaje kama hela ya kulipana ipo hau haipo hazina? Anayekwepa kodi tumfanyeje? na mwishowe ni nini vipaumbele vyetu mwaka huu, ujao, n,k?
Haya ndo maswali yatakayompa kiongozi yeyote ujasiri wa kutenda bila kulazimika kutumia utashi wake binafsi.