JK Rais Bora kuliko wote Tanzania

dada ff kafanya au kaendeleza?

Hivyo vyote nilivyoandika hapo juu, kavikuta vya kabla yake, nnachosema mimi ni kuwa, Kikwete kwa wakati wake huu mfupi wa miaka 6 tu, katika hivyo alivyovikuta hakuna hata kimoja ambacho kwa uchache hajakifanya zaidi ya mara mbili yake.

Nashangaa sana wooote wasioyaona haya, hivi huwa mnamchukia kwa jina lake? Kwa rangi yake? Kwa chama chake? Kwa dini yake? Kwa mafanikio yake? Maana nashindwa kuwaelewa kabisa, mkiambiwa leteni basi ambacho hajakifanya, hamna hata mmoja anae hata thubutu kuja na chochote. Tafakari.
 
Na wewe kwishney, kajipange uje na hoja..naona umeanza matusi....

acha ku-copy and paste mkuu,

Unataka hoja gani zaidi tumekuonyesha jinsi JK alivyowapiku marais wote kila idara ukaja na hoja zako dhaifu za udini ..kwishney njoo na hoja kupinga mafanikio ya JK (uje na economic statisitics comparative analysis) ..
 
acha ku-copy and paste mkuu,

Unataka hoja gani zaidi tumekuonyesha jinsi JK alivyowapiku marais wote kila idara ukaja na hoja zako dhaifu za udini ..kwishney njoo na hoja kupinga mafanikio ya JK (uje na economic statisitics comparative analysis) ..

Nategemea uje na vigezo mbadala vinavyoendana na "Uislamu" na matakwa ya "Allah", na siyo dhana za "economic statistics" na "comparative statistics" zinazotakana na "intellectual traditions" za "Mfumo Kristo". Kwa kifupi, nategemea ungekuja na vigezo na dhana za "Mfumo Islam" kupima mafanikio na mapungufu ya Alhaji Rais wako "JK."
 
Nategemea uje na vigezo mbadala vinavyoendana na "Uislamu" na matakwa ya "Allah", na siyo dhana za "economic statistics" na "comparative statistics" zinazotakana na "intellectual traditions" za "Mfumo Kristo".

Kwishney, njoo na hoja za kumlaumu JK zenye economic statistics ...and comparative analysis..

kuhusu mfumo kristo ni topic nyingine fungua uzi wake tutajadili ok
 
Kwishney, njoo na hoja za kumlaumu JK zenye economic statistics ...and comparative analysis..

kuhusu mfumo kristo ni topic nyingine fungua uzi wake tutajadili ok

Hapana, "Mfumo Kristo" ndiyo main issue here. Ama baada ya kusema hayo, ningependa uje na dhana na vigezo vyako vya kumtathmini Rais wako "JK" kulingana na "Mfumo Islamu". Usisahau kuja na takwimu na majedwali husika yanayokubalika aka "halal" kulingana na "Mfumo Uislamu"
 
Hapana, "Mfumo Kristo" ndiyo main issue here. Ama baada ya kusema hayo, ningependa uje na dhana na vigezo vyako vya kumtathmini Rais wako "JK" kulingana na "Mfumo Islamu".

Soma thread title: JK Rais bora kuliko wote Tanzania

Hayo mengine ni uchafuzi wa mada
 
Soma thread title: JK Rais bora kuliko wote Tanzania

Hayo mengine ni uchafuzi wa mada
Sawa, lakini kuna vigezo angalau viwili vya kutathmini "ubora wa rais JK": aidha kulingana na vigezo na dhana za "Mfumo Kristo" au zile za "Mfumo Uislamu". Au wewe unaonaje?
 
Haya endelea upendavyo...

Hapana mkuu, nimeomba tu utufafanulie namna gani "Rais wako JK" ni "Rais bora" kuendana na maadili, dhana, mafundisho na vigezo vya "Mfumo Uislamu" huku ukituwekea takwimu na ushahidi husika kuthibitisha na kuteteta hoja zako kulingana na mafundisho na matakwa ya "Allah".
 
Hapana mkuu, nimeomba tu utufafanulie namna gani "Rais wako JK" ni "Rais bora" kuendana na maadili, dhana, mafundisho na vigezo vya "Mfumo Uislamu" huku ukiutwekea takwimu na ushahidi kuthibitisha na kuteteta hoja zako kulingana na mafundisho na matakwa ya "Allah".

Kumbe umedandia treni kwa mbele..anza kusoma upya thread..utaona mafanikio ya JK kwa vigezo vya kiuchumi siyo hisia bila takwimu..

anza kusoma thread..
 
Kumbe umedandia treni kwa mbele..anza kusoma upya thread..utaona mafanikio ya JK kwa vigezo vya kiuchumi siyo hisia bila takwimu..

anza kusoma thread..

Hapana, fahamu kwamba thread nimeisoma vyema, na sielewi una maana gani haswa unapokuja na kauli kama "mafanikio ya JK kwa vigezo vya kiuchumi siyo hisia bila takwimu?"

Kwa kweli, ninachoomba ni wewe kutueleza dhana, vigezo na takwimu vya kutathmini "mafanikio ya JK" yanayokubalika na "Mfumo Islam" vis-a-vis "Mfumo Kristo". Ikiwezekana, utuambie maneno ya Kiarabu au "Kiislamu" yanayolingana na dhana kama "economic statistics ...and comparative analysis"
 
Mbona umeshaanza kuzipinga kabla hata hujapewa? meaning wewe unaziamini zipi? WB, IMF au BoT? MoF ? tukupe hizo

Wananchi hasa wanafunzi ya UDSM ni munkari na hisia zilizotokana na wanasiasa wa cdm kuwajaza ujinga wanafunzi so hiyo haiwezi ku determinants ya kupendwa au success or unsuccess ya Rais ..nenda kigoma, handeni rukwa mikoa ya pembezoni alipowekeza JK ambako kuliachwa miaka nenda rudi uone wananchi wanavyofurahia..

Elimu wala usisema in terms of number of secondary and university enrollment (hakuna aliyemfikia comparisons)

Afya amewapita kwa mbali sana..

Zote hizo ni Bomu umeshawahi kusikia nchi yoyote hapa duniani ambayo ilifuata masharti ya IMF na WB kufanikiwa na sera hizo?
Umewasikia makada wa chama kama Warioba, SAS, Kitine na wengine jinsi wanavyosema kwamba Kikwete anaipeleka nchi pabaya? Sasa nani aaminiwe hapa hawa makada ambao wanayajua mengi ndani ya Serikali na chama chenu cha magamba au tukuamini wewe!? Hapa chini ni baadhi ya shule zetu na hospitali ambazo zinakatisha tamaa na kusikitisha sana na ndiyo maana watoto wa vingunge hawasomi katika shule hizi na wala wao na familia zao hawatibiwi katika hospitali zetu. Usafiri angalia TRC, ATC na hata usafiri wa meli ulivyochoka kutokana na sera mbovu za Kikwete.

Hiyo Elimu shule hazina Walimu au unakuta shule ina Mwalimu mmoja kuanzi la kwanza hadi la saba au sekondari kuanzi form 1 hadi 4 haina Walimu matokeo yake wanaomalia hata kuandika majina yao hawajui, hao wachache waliobahatika kumaliza vyuoni hakuna ajira halafu wanaambiwa mjiajiri!!!! Utajiajiri vipi unatoka katika familia ya kimaskini huna hata kianzio cha biashara. Acha hizo banaaa. Hakuna Mtanzania ambaye ana chuki binafsi na msanii Kikwete lakini ikija kwenye utendaji wake lazima ukweli tuuseme kwamba kazi ya kuongoza nchi imemshinda vibaya sana, angekuwa na mapenzi ya kweli na nchi yetu basi angejiuzulu na kuwapisha wenye uwezo wa kuongoza nchi wafanye hivyo.

tanzania_materna_460261artw.jpg





ya+bwatta.jpg
156565_178002748892675_100000488544093_599644_5694958_n.jpg

WAGONJWA_ZAHANATI_KISAKI[1]_[1].JPG

 
Hapana, fahamu kwamba thread nimeisoma vyema, na sielewi una maana gani haswa unapokuja na kauli kama "mafanikio ya JK kwa vigezo vya kiuchumi siyo hisia bila takwimu?"

Kwa kweli, ninachoomba ni wewe kutueleza dhana, vigezo na takwimu vya kutathmini "mafanikio ya JK" yanayokubalika na "Mfumo Islam" vis-a-vis "Mfumo Kristo". Ikiwezekana, utuambie maneno ya Kiarabu au "Kiislamu" yanayolingana na dhana kama "economic statistics ...and comparative analysis"

Mie nasema vyoote hivyo Kikwete kafanya zaidi, kama wewe una data zinazonesha hajafanya zaidi tuwekee hapa.

Kuwa hiki hapa kilifanywa kabla ya Kikwete Kikwete hajafanya kama hata robo yake, siyo vimefanywa tu, na viwepo vinafanya kazi iliyokusudiwa.
 
Haya ni maneno ya Mstaafu SAS na si maneno ya BAK na huyu sidhani kama ana chuki binafsi na Kikwete hata baada ya Kikwete na kundi lake la mtandao kumchafua katika kampeni za 2005:


ANAONYA BILA MARIDHIANO NCHI ITAELEKEA KUBAYA, KITINE ADAI SERIKALI 'INATUPELEKA PABAYA'
Boniface Meena
Mwananchi

MJADALA wa Muswada wa Katiba Mpya umechukua sura mpya baada ya viongozi waandamizi wa Serikali wakiwamo wastaafu, kutaka upatikane mwafaka wa kitaifa kuhusu suala hilo vinginevyo taifa litaelekea kubaya.Onyo la viongozi hao akiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Dk Salim Ahmed Salim na Mkurugenzi Mkuu mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa , Dk Hassy Kitine, linakuja ikiwa ni siku chache baada ya Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe kutaka mwafaka huo wa kitaifa.

Jana, viongozi wakichangia maoni yao katika mdahalo uliondaliwa na Taasisi ya Mfuko wa Mwalimu Nyerere (MNF), kuhusu nafasi na umuhimu wa katiba katika maisha ya Watanzania, kwa sehemu kubwa walipaza sauti kutaka mwafaka huo ili kunusuru taifa.

Kauli ya Dk Salim
Dk Salim ambaye ni mwenyekiti wa MNH, alisema ni muhimu kuwe na makubaliano na maafikiano katika suala la Katiba Mpya kwa CCM na Chadema.

Alisema, “Chama tawala na chama kikuu cha upinzani vijue tunaangalia mustakhabali wa taifa letu, lazima uelewano uwepo”.
Dk Salim alisema kwamba malumbano si mazuri japokuwa ni sehemu ya siasa, lakini akaonya kwamba yasiruhusiwe yakasababisha nchi ikafika pabaya.
“Ninachoomba chama tawala na Chadema wafikirie mwafaka na kuangalia mustakhabali wa taifa, kama hakuna maafikiano si jambo zuri kwa taifa,”alisema Dk Salim ambaye ana uzoefu na utatuzi wa migogoro ya kimataifa.

 
Mie nasema vyoote hivyo Kikwete kafanya zaidi, kama wewe una data zinazonesha hajafanya zaidi tuwekee hapa.

Kuwa hiki hapa kilifanywa kabla ya Kikwete Kikwete hajafanya kama hata robo yake, siyo vimefanywa tu, na viwepo vinafanya kazi iliyokusudiwa.

Nasema hivi, mtuwekee takwimu na sababu zenu za kudai kwamba Kikwete "kafanya zaidi" kulingana na dhana na vigezo vya "Mfumo Islamu" ukilinganisha na vile vya "Mfumo Kristo". Kwa kifupi, tunaomba "darsa" kwa nini Kikwete ni bora zaidi ya Nyerere na pengine hata Mkapa kulingana na mtazamo mliyo nao wa "Mfumo Islamu"
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ni Rais aliyepitia Misukosuko mingi
Ni Rais alikumbana na upinzani mkali
Ni rahisi aliyetoa uhuru wa kwa kila mtu asemalo
Ni Rais alietuletea misaada mingi kutoka kwa wahisani
Ni rahisi ambaye anaongoza katika kipindi kigumu
Ni Rais anayepambana na ufisadi Mf richmond,EPA,nk
Ni Rais anayepambana na wanaofuja mali ya umma
Ni Rais Msikivu na mpokea maoni ya wapinzani

Namtakia kila la heri na kazi yake
Ongeza na sifa hizi:
  • Ni Rais wa kwanza tokea tupate Uhuru kutumia muda wake kuzurura ulimwenguni kwa safari zaidi ya 360 ndani ya miaka sita tu ya utawala wake ambazo ni sawa na jumla ya safari walizofanya wenzake woote!
  • Ni Rais wa kwanza 'kuingizwa mjini' kwa kudanganywa na kusaini nyaraka kadhaa nyeti ambazo baadae aligundua kuchomekewa na kuzifuta!
  • Ni Rais wa kwanza kuchaguliwa kwa kishindo kikubwa katika uchaguzi uliohusisha upinzani lakini ambaye kwa kipindi kimoja tu cha miaka mitano alichokwa karibu na kila mtu hadi ilimbidi kuchakachua ili kubaki madarakani!
  • Ni Rais wa kwanza kufunga safari kwenda kuomba vyandaruwa na kurejea akijitapa kwamba safari yake imezaa matunda - (Ya kupewa vyandaruwa?)
  • Ni Rais wa kwanza kutumia mabavu kuwanyamazisha wanaompinga kwa kutumia Jeshi linaloongozwa na shemeji yake kuwauwa wananchi wengi kwa risasi zaidi ya Rais yeyote aliyemtangulia.
  • Ni Rais wa kwanza kushindwa kuchukua hatua dhidi ya vibaka uchumi na mafisadi na ambao yeye mwenyewe pia ni mtuhumiwa.
  • Ni Rais wa kwanza kuiongoza nci kisanii sanii na kwamba analolisema si analolidhamiria.
  • Ni Rais mwasisi wa udini, ukabila na umakundi makundi katika chama chake na nchi.
Na wengine ongezeni niliyoyasahau, maana ametenda meengi.
 
Jibu swali: mgao wa umeme umekwisha? Leo ni Novemba 26 tunaelekea Desemba. Mwaka mzima Tanzagiza inarindima unaniambia
ameongeza mitambo. Tanzagiza ya Kikwete hiyo. Na shilingi inazidi kuporomoka. Hapo hujaweka inflation ambayo inakimbilia 20% wakati anachukua nchi Mkapa alikuwa ameishusha hadi 6%. Tanzania ya Kikwete hawachekani na Zimbabwe ya Mugabe, lakini kama mavuvuleza wa Patriotic Front wanavyoendelea kumsifia kizee ndivyo hivyo hivyo mavuvuzela ya Bongo yanaendelea kumsifia kilaza.

kwa mf ukiulizwa nini source ya kuporoka kwa tsh against dola utajibu nini?
 
Back
Top Bottom