Kikwete aanze kipi? Chama, Serikali, Bunge ama Madaktari?
Vijana wa mtaani wanasema ameshikwa bapaya. Bunge wanataka ongezeko la pesa - naona hilo anajaribu kutia mkazo hakusaini, lakini hawezi kusema hadharani. Madaktari wamegoma lakini alichelewa kuona mgomo huu utafika hapa ulipo kwahiyo hawezi kuingilia sasa. Waziri Mkuu anashutumiwa anambadilisha vipi maana kambadilisha Lowasa majuzi tu - na swala amuweke nani? ili afanye nini? Eti afanye reshuffle kwa nini? Lakini unamfukuzaje Waziri na Naibu wake tu? Wabunge wa CCM wanamtishia juu ya katiba na labda kutoridhishwa na maamuzi yake ya posho.
Jamani haya mambo sio mepesi, na tusitizame kama jambo moja moja maana ikitokea tu haya mambo yakaunganika - basi tumekwisha.
Nadhani kikwete anahitaji ushauri hapa! Aanzie wapi? Unaanzaje na mgomo wakati ndani kwako ni vuruvaru?
Vijana wa mtaani wanasema ameshikwa bapaya. Bunge wanataka ongezeko la pesa - naona hilo anajaribu kutia mkazo hakusaini, lakini hawezi kusema hadharani. Madaktari wamegoma lakini alichelewa kuona mgomo huu utafika hapa ulipo kwahiyo hawezi kuingilia sasa. Waziri Mkuu anashutumiwa anambadilisha vipi maana kambadilisha Lowasa majuzi tu - na swala amuweke nani? ili afanye nini? Eti afanye reshuffle kwa nini? Lakini unamfukuzaje Waziri na Naibu wake tu? Wabunge wa CCM wanamtishia juu ya katiba na labda kutoridhishwa na maamuzi yake ya posho.
Jamani haya mambo sio mepesi, na tusitizame kama jambo moja moja maana ikitokea tu haya mambo yakaunganika - basi tumekwisha.
Nadhani kikwete anahitaji ushauri hapa! Aanzie wapi? Unaanzaje na mgomo wakati ndani kwako ni vuruvaru?