Jk ni msikivu: CHADEMA pia wamemsikia-hakuna maandamano sasa!

Mchakato wa Katiba mpya bado ni mjadala endelevu hadi hapo itakapopatikana.Mwishoni mwaka 2011 Wabunge hasa wa CHADEMA hawakuridhika na maamuzi ya Bunge kuupitisha mswada huo.Walitoka nje wakati wote wa mjadala wa Katiba ulipokuwa ukijadiliwa. Waliazimia kufanya maandamano nchi nzima kuupinga mswada. Katika hotuba ya Mwaka Mpya 2012, Rais aligusia mchakato huo. Hata hivyo, alitoa angalizo kwa wale wanaotaka kuandamana akiwakumbusha kwamba dola ipo. CHADEMA walisikia. Wakakaa chini, wakatafakari. Wakaomba kuonana na kiongozi wa nchi.Akawaruhusu. Waliwasilisha maoni yao. Hata hivyo, hawakuridhika na uamuzi wa JK kuutia sahihi mswada huo baada ya mazungumzo na wawakilishi wa chama hicho. Waliazimia tena kuandamana.Hata hivyo, busara ilichukua mkondo wake. Wakaomba kuonana na Rais kwa mara ya pili. Wamefanya. Wameweza. Rais msikivu amewasikia.Tanzania ni yetu sote: CCM.CHADEMA, CUF, NCCR, nk. Ni mwanzo mzuri wa ukuzi wa Demokrasia ambayo katika nchi yetu naweza ifananisha kama ipo katika hatua ya mchicha ila kwa hekima tutaikuza na kuwa kubwa kama mbuyu.Kumbe ujumbe unaweza kufika kwa wahusika bila maandamano?

MWAKA 2005 JK ALIPOINGIA MADARAKANI ALISEMA HIVI " Ukiona Watu wanakusifia sana na kukushangilia kwa kila jambo, ujue wamekufanya ZUZU, wanakuibia hao"
Naona umeamua kumsifia sana JK....si Bure!!!
 
hata mwili wa nyoka unabeba vitu kibao ili aweze kutambaa lakini bado kichwa kinakuwa na ukali zaidi ya sehemu nyingine ya mwili sasa hata yeye anatakiwa awe kama kichwa cha nyoka

Davidie: unaungana na Sitta wakati fulani alimuomba awe mkali kidoogo! Katika yote hii ni hatua muhimu kwa kiongozi wa nchi anapoweza kufanyia kazi mawazo ya wapinzani kwa maslahi ya nchi. Tanzania kwanza vyama badaye.
 
Sio usikivu wala nini alipigwa mkwala ma mabalozi (wazungu) siku CCM wakicheza mdundiko bungeni chadema wakiwa wametoka. Usikivu ameanza lini???? na maswala mengine ni ukubwa wa misafara yake ilitoka indirectly akaamua kusema pia kapunguza. Zungu prayer si mchezo

Moja ya faida ya vyama vya upinzani ndio hiyo. Kuwa kama "watchdog". Piga kelele kama mbu hadi waliolala wanakosa usingizi!
 
JK mwenyewe anakunwa sana na CHADEMA na ingekuwa kuna kubadilishana angehamia CDM coz ameona jamaa walivyo na hoja za nguvu,haijawahi kutokea Rais kuwageuka wabunge wake, na alikiri kabisa kuwa alisaini kwa kuogopa kutengwa na wenzie hata walioporomosha mashairi bungeni,sheria iliporudi wamejikuta wakila matapishi yao,muulizeni Sendeka.

Kimsingi kama tutafika kwenye demokrasia ya masikilizano mazuri ni jambo jema sana,katika hili la katiba hauna mshindi na mshindwa,ni faida ya watanzania wote!Japokuwa waanzilishi wa vuguvugu walikuwa CDM.

Jk angekuwa pia msikivu kwenye RICHMOND,DOWANS,EPA,Vyuo vikuu,madaktari n.k nadhani tungefika pazuri.mi siafiki kuwa marekebisho haya yametokana na usikivu tu wa JK.big NO,ni kwamba hali ilikuwa mbaya kwani wahisani walitishia kuacha kutupia rupia kwenye kombe la matonya kama anawabana wapinzania na kupitisha sheria kandamizi!

Tuna safari ndefu sana kuelekea ule usikivu halisi wa kidemokrasia,ila inawezekana ni suala la wananchi kufunguka kifikra!
Waliokwazika tusameheane,ndo uhuru wa mawazo wenyewe!

Tuko pamoja mkuu.
 
MWAKA 2005 JK ALIPOINGIA MADARAKANI ALISEMA HIVI " Ukiona Watu wanakusifia sana na kukushangilia kwa kila jambo, ujue wamekufanya ZUZU, wanakuibia hao"
Naona umeamua kumsifia sana JK....si Bure!!!

Nyumbu: Nimeipenda nukuu yako though. Ila kiukweli, kumbuka alikuwa amesaini mswada huo tayari kama Bunge ambalo sehemu kubwa linaundwa na CCM walipitisha. Lakini kikao cha pili walichokaa na CHADEMA kimewezesha yeye kubadili uamuzi. Ndiyo mana utaiona mantiki ya usikivu wake. Mkuu ni hilo tu: Hakuna kuzuzuliwa wala kuibiwa hapo!
 
Ukomavu huo pia umedhihirishwa na Mbowe pale mjengoni aliposisitiza:Maslahi ya nchi kwanza; vyama baadaye.


Chipolopolo umenikumbusha kauli ya MBOWE mjengoni. Alisema "kwa niaba ya kambi ya upinzani tunakubali yaishe" akaendelea kusema "Wabunge wa CCM wasiendelee na mtindo wa funika kombe mwanaharamu apite" Huu ni ukomavu wa kisiasa maana kauli kama hizi hazikuwepo....badala yake ilikuwa ni kutoka nje ya mjengo na kwenda kuitisha maandamano yenye kauli mbiu ya "Mpaka kieleweke"
 
Wafadhili gani? Nenda kwenye thread za magamba ukatoe hiyo micomment yako ya kimwanaasha

Solokondo! Mwache kidoogo Mwanaasha atafakari hatua ya kuchukua baada ya matokeo. Bado ananafasi ya kuthubutu. Makupa naye hayo ni maoni yake tu, mkuu.
 
Chipolopolo umenikumbusha kauli ya MBOWE mjengoni. Alisema "kwa niaba ya kambi ya upinzani tunakubali yaishe" akaendelea kusema "Wabunge wa CCM wasiendelee na mtindo wa funika kombe mwanaharamu apite" Huu ni ukomavu wa kisiasa maana kauli kama hizi hazikuwepo....badala yake ilikuwa ni kutoka nje ya mjengo na kwenda kuitisha maandamano yenye kauli mbiu ya "Mpaka kieleweke"

Kengemumaji: "You just hit the iron while it is still hot! Umepiga mulemule...kenge mumaji! Ni kweli huo ni ukomavu kabisa. Na mfano huo tunaweza kuijenga nchi yetu. Hakuna haja ya kugombania fito wakati wote tunalengo la kujenga nyumba yetu Tanzania.Katika itatumiwa na wote si CCM, CDM, CUF, NCCR, UDP, kwa kuorodhesha vichache.
 
Walishapita yale maeneo yao ya kujidai kwa yale maeneo ambayo si riziki kwao hawathubutu kukanyaga
 
Pinda hapa aliona mbali. CHADEMA nao sasa wametumia darubini wameona mbali ambako Pinda alikwisha ona.Angalau matunda ya ukomavu wa kisiasa tutaanza kuyaona.
Wacha kumsingizia Pinda, hajawahi kuona mbali kwenye jambo lolote la si hivyo asingelia bungeni juu ya kauli yake kuhusu wauaji wa albino wala asigerudi kujipendekeza kwa madaktari waliogoma au asingekomalia posho haramu za wabunge, we Vipi?
 
Wacha kumsingizia Pinda, hajawahi kuona mbali kwenye jambo lolote la si hivyo asingelia bungeni juu ya kauli yake kuhusu wauaji wa albino wala asigerudi kujipendekeza kwa madaktari waliogoma au asingekomalia posho haramu za wabunge, we Vipi?

Hapo mkuu naona unataka kuipindisha nia njema ya Pinda.Mgomo wa madaktari tuseme tu awali alishauriwa vibaya!
 
jk hawezi kwenda chama cha kikabila cha wachaga,wakatoliki
JK mwenyewe anakunwa sana na CHADEMA na ingekuwa kuna kubadilishana angehamia CDM coz ameona jamaa walivyo na hoja za nguvu,haijawahi kutokea Rais kuwageuka wabunge wake, na alikiri kabisa kuwa alisaini kwa kuogopa kutengwa na wenzie hata walioporomosha mashairi bungeni,sheria iliporudi wamejikuta wakila matapishi yao,muulizeni Sendeka.

Kimsingi kama tutafika kwenye demokrasia ya masikilizano mazuri ni jambo jema sana,katika hili la katiba hauna mshindi na mshindwa,ni faida ya watanzania wote!Japokuwa waanzilishi wa vuguvugu walikuwa CDM.

Jk angekuwa pia msikivu kwenye RICHMOND,DOWANS,EPA,Vyuo vikuu,madaktari n.k nadhani tungefika pazuri.mi siafiki kuwa marekebisho haya yametokana na usikivu tu wa JK.big NO,ni kwamba hali ilikuwa mbaya kwani wahisani walitishia kuacha kutupia rupia kwenye kombe la matonya kama anawabana wapinzania na kupitisha sheria kandamizi!

Tuna safari ndefu sana kuelekea ule usikivu halisi wa kidemokrasia,ila inawezekana ni suala la wananchi kufunguka kifikra!
Waliokwazika tusameheane,ndo uhuru wa mawazo wenyewe!
 
Kitu kinachoifanya CDM iendelee kupaa kwa popularity ni kuwa very strategic. Sasa JK yupo jikoni katika kutengeneza list ya wale watakaounda timu ya kutafuta kura ya maoni. Within the next 5 weeks atayaweka wazi majina ya hao wateule.

Kama JK atacheza vizuri karata zake basi CDM wataendelea kuwa watulivu ila kama ataonyesha kuwa ni muendelezo wa same old watu bado wana haki ya kupinga.

CDM imesema kuwa bado ina haki ya kuingia kutoa elimu juu ya katiba na hapo ndipo utakapouona umakini wa chama hiki. Katiba ni nafasi nzuri sana ya kuleta mabadiliko ya kweli Tanzania kama tu hakutakuwa na pre-conceived preferences kwa CCM. Ila kama CCM itachezea mchakato huu basi 2015 itakuwa ni worse election year na kunawezekana kabisa uchaguzi usifanyike kama ilivyopangwa ili kurekebisha uozo wa katiba mpya.

Tanzania ni mali yetu sote, CCM, CDM et al ni nembo za kutofautisha mitazamo tu, kama haki itapatikana hakutakuwa na tofauti kwani mtu anaweza toka CCM na kugombea kupitia CDM and vice versa. Country first should be our slogan, parties are subsets of a country.
 
Kitu kinachoifanya CDM iendelee kupaa kwa popularity ni kuwa very strategic. Sasa JK yupo jikoni katika kutengeneza list ya wale watakaounda timu ya kutafuta kura ya maoni. Within the next 5 weeks atayaweka wazi majina ya hao wateule.

Kama JK atacheza vizuri karata zake basi CDM wataendelea kuwa watulivu ila kama ataonyesha kuwa ni muendelezo wa same old watu bado wana haki ya kupinga.

CDM imesema kuwa bado ina haki ya kuingia kutoa elimu juu ya katiba na hapo ndipo utakapouona umakini wa chama hiki. Katiba ni nafasi nzuri sana ya kuleta mabadiliko ya kweli Tanzania kama tu hakutakuwa na pre-conceived preferences kwa CCM. Ila kama CCM itachezea mchakato huu basi 2015 itakuwa ni worse election year na kunawezekana kabisa uchaguzi usifanyike kama ilivyopangwa ili kurekebisha uozo wa katiba mpya.

Tanzania ni mali yetu sote, CCM, CDM et al ni nembo za kutofautisha mitazamo tu, kama haki itapatikana hakutakuwa na tofauti kwani mtu anaweza toka CCM na kugombea kupitia CDM and vice versa. Country first should be our slogan, parties are subsets of a country.

Mkuu umesomeka kizalendo zaidi. Shukrani:Tanzania ni yetu sote. Nchi kwanza CCM,CDM, CUF,NCCR,UDP, nk baada ya kuiweka sawa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom