JK, Msiba Wa Jirani Na Yanayotokea Dodoma- Tafsiri Yangu

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu zangu,

Katika dunia hii mwanadamu huwezi kumchagua jirani yako. Jirani yako ni jirani yako. Msiba wa jirani ni msiba wako pia, unakuhusu.

Maana, kuna wanaohoji JK kuacha mambo ya nyumbani na kwenda kushiriki maziko ya Bingu wa Mutharika. Silioni kosa katika hilo. Na hata kama JK angeamua kutokwenda mazikoni Blantyre, bado, asingekwepa lawama. Maana, kuna ambao wangemlaumu JK kwa kutozingatia mila na desturi zetu Waafrika; kushiriki kwenye kumzika jirani yako.


Tukumbuke, kuwa Wamalawi si tu ni jirani zetu, ni ndugu zetu pia. Kuna Wanyasa wengi wa Malawi katika nchi hii waliochanganyika na makabila yetu. Na tunaambiwa, kuwa siku ya mkesha wa Uhuru wa Malawi, Watanzania wengi kando ya Ziwa Nyasa nao walikesha wakishangilia. Uhuru wa Mnyasa ni Uhuru wetu. Msiba wa Mnyasa, ni msiba wetu.


Mengineyo...

Nchi yetu inapita sasa kwenye kipindi kigumu sana. Tusishushe chini kiwango cha mjadala. Kubaki kumjadili JK na safari kwenda kutuwakilisha mazikoni ni kushusha kwa makusudi kiwango cha mjadala. Kwa makusudi tutakuwa tumeacha kujadili hoja za msingi ikiwamo hii ya kashfa za ufisadi wa kutupwa uliodhihiri bungeni na unaotutaka tuweke shinikizo kwa wahusika kuachia ngazi na hata kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Maana, anayeliibia taifa ni mhalifu tena zaidi ya mwizi wa kuku. Huyu ni jambazi. Kumwacha aendelee kukalia ofisi ya umma ni sawa na kumsusia mlevi bia, au kumpa fisi kazi ya kulinda bucha.


Tuliko sasa ni kubaya. Tunakokwenda kutakuwa ni kubaya sana kama hatutachukua hatua sasa. Nimeona asubuhi ya leo kwenye runinga ( Channel Ten) utetezi wa ajabu kutoka kwa Waziri wa Uchukuzi Bw. Omar Nundu.

Nundu anadai hawezi kujiuzuru kwa kutoa hoja ambazo kimsingi zinamtaka aachie ngazi haraka iwezekanavyo ili abaki na heshima kwa jamii kama bado anayo.


Anatwambia Watanzania kuwa amekuwa 'akizungukwa' na Naibu wake Athuman Mfutakamba. Ndio, Waziri Nundu anapojitetea kwa Watanzania kwa kusema haelewani na Naibu wake na kuwa kampuni ya Kichina ilimpeleka Naibu wake China, Mauritania na Equatorial Guinea bila kibali chake inatosha kuonyesha kiwango cha juu cha ukosefu wa nidhamu, uwajibikaji na uadilifu katika baraza la mawaziri . Sioni ni kwa namna gani maelezo ya Nundu yanaweza kumlinda mbali ya kuonyesha ulazima wa kuwajibishwa kwake haraka iwezekanavyo.


Ndio huwezi kuonyesha kuwa ulijua kilichokuwa kikifanyika, ukabaki kimya mpaka unatwambia hii leo, halafu utake ridhaa ya umma ikuamini kuendelea kukupa dhamana ya kushika nafasi hiyo hiyo.


Na wahenga walisema; kwenye msako wa nyani ngedere hawezi kusalimika.
Ndio, tutafanya makosa kudhani kuwa ’madudu’ haya yaliyoibuliwa kwenye ripoti ya CAG yanahusu Wizara tano au sita tu. Hii ni fursa pekee kwa Watanzania kupitia wabunge wao kuendesha ’ msako mkubwa’ wa wote wenye kulitafuna taifa letu tunalolipenda.


Ni wakati pia wa kuhakikisha Katiba Mpya tunayokwenda kuitolea mapendekezo yetu itusaidie kuziba mianya ya wezi wa mali ya umma kuendelea kuliibia taifa bila ya hofu ya kufikishwa mahakamani na hata kutiwa magerezani.


Ndio, hatuwezi kuenenda kama tunavyoenenda sasa; maana, unapoona Wananchi wanalalamika, Wabunge wanalalamika, Mawaziri wanalalamika, na Rais analalamika, basi, hilo ni taifa la ajabu sana. Taifa la Walalamikaji.

Na maradhi ya ' kulalamika' ni ya kimfumo. Ni mfumo mbovu tu ndio unaoweza kuzaa Taifa la Walalamikaji. Turekebishe mfumo wetu kwa kupitia Katiba. Inawezekana.


Maggid Mjengwa,

Iringa.
0788 111 765
Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo
 
Nchi hii ni kama haina Rais kabisa.
Rais anashindwa kufanya maamuzi magumu.
Rais anakimbia kivuli chake
Rais amekuwa mwoga kuwaadabisha watu alio wateua.
Rais hajui kwa nini Tanzania ni maskini huku watendaji wake wakifanya ufisadi wa kufuru.
 
Mfalme wetu ana Juha...anaweza hata kwenda kuzima moto unaoanza kuteketeza nyumba ya jirani akaacha kuendelea kuzima ule ulio kolea nyumbani kwake..kweli ana Juha..
 
Binafsi nimesikitika saana kusikia kwamba ameenda kuzika nje ya nchi badala ya kushughulikia suala hili zito la Mawaziri mbaya san ni pale wabunge wanapowasilisha hoja ya PM kujiuzulu, yaani yeye haoni kuwa jambo hilo ni zito sana kiasi cha kumkoseha usingizi kabisa, badala yake anaenda kuzika!!!!!!! si angemtuma mwakilishi tu jamani kwani lazima kila tafrija ahudhurie yeye mwenyewe! kweli Mungu atusaidie nchi yetu isije angamia
 
Mambo mengi mazito ya kitaifa amewahi kuacha hapa nchini, yeye akaenda kutalii huko nje, mfano ni mgomo wa madakatari
 
Huyu Rais inabidi aingie kwenye Guinness book of records kwa kuwa rais wa ajabu duniani ambaye hajawahi na hatapata kutokea!
 
Ndugu zangu,

Katika dunia hii mwanadamu huwezi kumchagua jirani yako. Jirani yako ni jirani yako. Msiba wa jirani ni msiba wako pia, unakuhusu.

Maana, kuna wanaohoji JK kuacha mambo ya nyumbani na kwenda kushiriki maziko ya Bingu wa Mutharika. Silioni kosa katika hilo. Na hata kama JK angeamua kutokwenda mazikoni Blantyre, bado, asingekwepa lawama. Maana, kuna ambao wangemlaumu JK kwa kutozingatia mila na desturi zetu Waafrika; kushiriki kwenye kumzika jirani yako.


Tukumbuke, kuwa Wamalawi si tu ni jirani zetu, ni ndugu zetu pia. Kuna Wanyasa wengi wa Malawi katika nchi hii waliochanganyika na makabila yetu. Na tunaambiwa, kuwa siku ya mkesha wa Uhuru wa Malawi, Watanzania wengi kando ya Ziwa Nyasa nao walikesha wakishangilia. Uhuru wa Mnyasa ni Uhuru wetu. Msiba wa Mnyasa, ni msiba wetu.


Mengineyo...

Nchi yetu inapita sasa kwenye kipindi kigumu sana. Tusishushe chini kiwango cha mjadala. Kubaki kumjadili JK na safari kwenda kutuwakilisha mazikoni ni kushusha kwa makusudi kiwango cha mjadala. Kwa makusudi tutakuwa tumeacha kujadili hoja za msingi ikiwamo hii ya kashfa za ufisadi wa kutupwa uliodhihiri bungeni na unaotutaka tuweke shinikizo kwa wahusika kuachia ngazi na hata kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Maana, anayeliibia taifa ni mhalifu tena zaidi ya mwizi wa kuku. Huyu ni jambazi. Kumwacha aendelee kukalia ofisi ya umma ni sawa na kumsusia mlevi bia, au kumpa fisi kazi ya kulinda bucha.


Tuliko sasa ni kubaya. Tunakokwenda kutakuwa ni kubaya sana kama hatutachukua hatua sasa. Nimeona asubuhi ya leo kwenye runinga ( Channel Ten) utetezi wa ajabu kutoka kwa Waziri wa Uchukuzi Bw. Omar Nundu.

Nundu anadai hawezi kujiuzuru kwa kutoa hoja ambazo kimsingi zinamtaka aachie ngazi haraka iwezekanavyo ili abaki na heshima kwa jamii kama bado anayo.


Anatwambia Watanzania kuwa amekuwa 'akizungukwa' na Naibu wake Athuman Mfutakamba. Ndio, Waziri Nundu anapojitetea kwa Watanzania kwa kusema haelewani na Naibu wake na kuwa kampuni ya Kichina ilimpeleka Naibu wake China, Mauritania na Equatorial Guinea bila kibali chake inatosha kuonyesha kiwango cha juu cha ukosefu wa nidhamu, uwajibikaji na uadilifu katika baraza la mawaziri . Sioni ni kwa namna gani maelezo ya Nundu yanaweza kumlinda mbali ya kuonyesha ulazima wa kuwajibishwa kwake haraka iwezekanavyo.


Ndio huwezi kuonyesha kuwa ulijua kilichokuwa kikifanyika, ukabaki kimya mpaka unatwambia hii leo, halafu utake ridhaa ya umma ikuamini kuendelea kukupa dhamana ya kushika nafasi hiyo hiyo.


Na wahenga walisema; kwenye msako wa nyani ngedere hawezi kusalimika.
Ndio, tutafanya makosa kudhani kuwa ’madudu’ haya yaliyoibuliwa kwenye ripoti ya CAG yanahusu Wizara tano au sita tu. Hii ni fursa pekee kwa Watanzania kupitia wabunge wao kuendesha ’ msako mkubwa’ wa wote wenye kulitafuna taifa letu tunalolipenda.


Ni wakati pia wa kuhakikisha Katiba Mpya tunayokwenda kuitolea mapendekezo yetu itusaidie kuziba mianya ya wezi wa mali ya umma kuendelea kuliibia taifa bila ya hofu ya kufikishwa mahakamani na hata kutiwa magerezani.


Ndio, hatuwezi kuenenda kama tunavyoenenda sasa; maana, unapoona Wananchi wanalalamika, Wabunge wanalalamika, Mawaziri wanalalamika, na Rais analalamika, basi, hilo ni taifa la ajabu sana. Taifa la Walalamikaji.

Na maradhi ya ' kulalamika' ni ya kimfumo. Ni mfumo mbovu tu ndio unaoweza kuzaa Taifa la Walalamikaji. Turekebishe mfumo wetu kwa kupitia Katiba. Inawezekana.


Maggid Mjengwa,

Iringa.
0788 111 765
Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo

Mahusiano kati ya mataifa ni tofauti na mahusiano kati ya mtu na mtu. Huu mfano wako wa jirani kufiwa hau-apply katika medani za kidiplomasia. Inaruhusiwa kabisa kwa rais kumtuma mwakilishi wake kwenye msiba na nchi iliyofiwa ikampokea kwa uzito ule ule ambao angepewa rais.

Vile vile, inaruhusiwa kabisa kwa rais kumtuma waziri wa mambo ya nje kumpokea mkuu wa nchi airport kama yuko busy.
 
Maggid,

Wazungu wanasema charity begins at home, kwa hiyo wewe unaenda kwenye msiba nyumba ya jirani wakati nyumba yako hiko kwenye matatizo makubwa. Watu wa Pwani tuna priorities za ajabu sana! Tumeona marais mbali mbali waki-cancel safari pale nchi zao zinapokuwa na matatizo au wakitaka kupitsiha miswada mikubwa.
 
Kwa nini asimtume Rais wa Zanzibar kama Makamu wake hana nafasi au kama waziri wa mambo ya nchi za nje yuko kikaoni Dodoma? Wazanzibar wangefurahi kuona rais wao naye kapata heshima wanazolilia hii ni busara ya kawaida tu ingwa hatambuliki kupata heshima hiyo katika seriakli ya Muungano.
 
Back
Top Bottom