JK kwenda Ufaransa leo

Kabla hamjalalamika kwa nini rais anasafiri nje, someni undani wa anayokwenda kuyafanya huko nje. Rais huwa anapata mialiko mingi, mingine anawakilishwa, na mingine anaamua kwenda mwenyewe. Sasa mlitaka awakilishwe tu kila mahali? Ikiwa hivyo kutakuwa hakuna sababu ya kumwalika rais kwenye shughuli yoyote, watu wangetuma tu ujumbe ikulu kwamba wanaomba mwakilishi. Kama analoenda kufanya ni kinyume au ni nje ya majukumu ya urais ndipo tulalamike. Naomba mtu yeyote mwenye ushahidi kwamba anachoenda kufanya JK huko Ufaransa ni kinyume au ni nje ya majukumu ya rais wa nchi alete ushahidi huo hapa tuujadili. Hebu tujaribuni kudhibiti hisia zetu katika masuala kama haya. Yaani kwa kuwa hapo nyuma kumekuwepo madai kwamba rais anasafiri sana nje (pengine yana ukweli, sijui), basi kila safari aifanyayo tuilalamikie na kuitilia mashaka? Ni lini basi rais atasafiri nje nasi tuone amefanya sawa kusafiri? Tumkosoe rais inapobidi, lakini tupunguze ushabiki usio na msingi kama huu wa kuona kwamba kila safari anayofanya eti anenda "kula nchi". Jamani, tuangalie pande zote.

Kwa ufupi naomba ushahidi au hoja za kuthibitisha kwamba kwa kwenda Ufaransa leo, JK amefanya jambo ambalo ni nje au ni kinyume na majukumu yake ya urais.
 
Tumkosoe rais inapobidi, lakini tupunguze ushabiki usio na msingi kama huu wa kuona kwamba kila safari anayofanya eti anenda "kula nchi". Jamani, tuangalie pande zote.

Kithuku,

wewe ukiwa na akiba ya sh alfu hamsini benki, una watoto wawili ambao wanasoma sekondari kwa karo ya alfu ishirini kwa mwaka, na mama yako mzazi ni mgonjwa na anahitaji tiba kwa sh alfu kumi na tano.

Wakati unafikiria cha kufanya, mjomba wako tajiri anakupa mwaliko wa kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya binti yake. ifahamike kuwa huyu mjomba wako aliwahi kukunyang'anya mali zako zote miaka ya nyuma ila siku za karibuni amekuwa anakupatia mkopo wa sh mia tano kila mwezi...Gharama ya kwenda kwa mjomba wako ni karibu sh elfu arobaini.

je, ingawa kwenda kuiitika mwaliko wa mjomba wako ni sehemu ya majukumu yako, wewe utakwenda kwa mjomba wako au utatumia akiba yako kupeleka watoto wako shule na kujaribu kumtibia mama yako?
 
Anakwenda kutupiga bei,hakuna lolote la maana subiri kama hutasikia kapewa kamsaada.
Serikali yake ingekuwa inafanya mambo kwa uwazi kusingekuwa na tatizo,lakini utaona rais kapiga picha yupo kwa mshikaji wake wanapiga stori kituambacho ni kinyume na maadili ya kazi
 
Mimi mpaka sasa bado siamini..nimesikia alikuwa usa kwa wiki tatu hivi majuzi tu, na sasa atakuwa ulaya kwa siku nane.Ukijumlisha ni mwezi mzima umekatika hayupo ofisini wakati nchi inawaka moto, bongo kila kitu mbofumbofu kwa sasa..akina butiku et al. wameyasema sana jana kwenye kongamano la mwalimu..nashangaa kusikia leo kaingia viwanja tena!!Huyu jamaa hayuko serious hata kidogo..Huu ni utani sasa na kejeli za wazi..Kwa hali ilivyo sasa hapo home inahitaji utulivu wa hali ya juu walau kuweka mambo sawa, watu waone ana usikivu na kujali kiasi fulani..Sio kutuambia kazi kwaachia pccb, wakiboronga yeye hayumo!!Kweli hizi dharau na ukwepaji wa majukumu wa wazi..binafsi inanisikitisha sana
 
Kithuku,

wewe ukiwa na akiba ya sh alfu hamsini benki, una watoto wawili ambao wanasoma sekondari kwa karo ya alfu ishirini kwa mwaka, na mama yako mzazi ni mgonjwa na anahitaji tiba kwa sh alfu kumi na tano.

Wakati unafikiria cha kufanya, mjomba wako tajiri anakupa mwaliko wa kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya binti yake. ifahamike kuwa huyu mjomba wako aliwahi kukunyang'anya mali zako zote miaka ya nyuma ila siku za karibuni amekuwa anakupatia mkopo wa sh mia tano kila mwezi...Gharama ya kwenda kwa mjomba wako ni karibu sh elfu arobaini.

je, ingawa kwenda kuiitika mwaliko wa mjomba wako ni sehemu ya majukumu yako, wewe utakwenda kwa mjomba wako au utatumia akiba yako kupeleka watoto wako shule na kujaribu kumtibia mama yako?

Mwafrika wa kike,

Salamu dada. Mfano wako unavutia sana. Nadhani unazungumza suala la vipaumbele hapa. Vema sana. Lakini katika muktadha wa safari hii anayofanya JK, sivyo. Wachangiaji wanadai ati kwa nini hakutuma mwakilishi? Sasa akituma huyo mwakilishi atasafiri bure? Kwa hiyo kama "mjomba" unayemzungumzia kanialika, na hela niliyo nayo ni kidogo, basi nisiende lakini nimtume mke wangu, mdogo wangu, wanangu n.k akaniwakilishe, kwani sasa huyu hatatumia gharama? Mantiki iko wapi hapa?

Na pili, kuna ushahidi kwamba anachoendea JK huko Ufaransa ni jambo dogo tu linaloweza kufananishwa na mfano uliotoa wa "sherehe ya kuzaliwa binti ya mjomba tajiri"? Je haendi kwa maslahi ya taifa? Je si wajibu wake kama rais kufanya safari hiyo? Ndizo hoja ninazohitaji kuona zikizungumziwa hapa.
 
Mzee mwanakijiji
naomba upeleke ule wimbo wa "tazama ramani utaona nchi nzuri" umetuwekea baada ya interview ya salim..umeniliwaza na kuniburudisha sana kwani niliflash back kwa muda na kusahau hizi kero zilizopo nyumbani, nadhani zile siku zilikuwa na uzuri zake!!
 
Mwafrika wa kike,

Salamu dada. Mfano wako unavutia sana. Nadhani unazungumza suala la vipaumbele hapa. Vema sana. Lakini katika muktadha wa safari hii anayofanya JK, sivyo. Wachangiaji wanadai ati kwa nini hakutuma mwakilishi? Sasa akituma huyo mwakilishi atasafiri bure? Kwa hiyo kama "mjomba" unayemzungumzia kanialika, na hela niliyo nayo ni kidogo, basi nisiende lakini nimtume mke wangu, mdogo wangu, wanangu n.k akaniwakilishe, kwani sasa huyu hatatumia gharama? Mantiki iko wapi hapa?

Na pili, kuna ushahidi kwamba anachoendea JK huko Ufaransa ni jambo dogo tu linaloweza kufananishwa na mfano uliotoa wa "sherehe ya kuzaliwa binti ya mjomba tajiri"? Je haendi kwa maslahi ya taifa? Je si wajibu wake kama rais kufanya safari hiyo? Ndizo hoja ninazohitaji kuona zikizungumziwa hapa.

..huitaji kupelekwa shule kujifunza kula samaki!

..uking'ata mnofu,ukihisi mifupa utaitema au kuiondoa!

..sasa weye yawezekana samaki huwajui!ipo siku utakula na hamna atakayekufundisha kumwondoa mifupa!
 
Mwafrika wa kike,

Salamu dada. Mfano wako unavutia sana. Nadhani unazungumza suala la vipaumbele hapa. Vema sana. Lakini katika muktadha wa safari hii anayofanya JK, sivyo. Wachangiaji wanadai ati kwa nini hakutuma mwakilishi? Sasa akituma huyo mwakilishi atasafiri bure? Kwa hiyo kama "mjomba" unayemzungumzia kanialika, na hela niliyo nayo ni kidogo, basi nisiende lakini nimtume mke wangu, mdogo wangu, wanangu n.k akaniwakilishe, kwani sasa huyu hatatumia gharama? Mantiki iko wapi hapa?

Mimi sikushauri umtume mke wako au mdogo wako kwa sababu sioni umuhimu wa kwenda hiyo safari in the first place. Kwa waliosema kuwa atume mwakilishi nadhani wanatumia mantiki kuwa Rais wa nchi anasafiri na detail kubwa sana na inayogharimu pesa nyingi.... Huwezi kulinganisha gharama za msafara wa rais na kama let's say akimwambia balozi ambaye tayari yuko katika hiyo nchi husika akamwakilisha!

Na pili, kuna ushahidi kwamba anachoendea JK huko Ufaransa ni jambo dogo tu linaloweza kufananishwa na mfano uliotoa wa "sherehe ya kuzaliwa binti ya mjomba tajiri"? Je haendi kwa maslahi ya taifa? Je si wajibu wake kama rais kufanya safari hiyo? Ndizo hoja ninazohitaji kuona zikizungumziwa hapa.

Umesoma lakini yaliyosemwa kwenye news kuhusu baadhi ya mambo ambayo kikwete atafanya? kuhudhuria mkutano wa sijui FAO!, kukutana na pope, nk?

Come on Kithuku, hii mikutano labda ni lazima kwa ushirikiano wa kimataifa lakini faida yake kwa nchi ni kidogo sana. Maendeleo na wawekezaji yataletwa na miundo mbinu mizuri na mikataba iliyo wazi na yenye manufaa kwa raia sio safari za nje zisizokwisha!

Hii ndiyo sababu nafanisha safari hizi na kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya binti ya mjomba wako.
 
...kumbe ile safari ya Medical check up ufaransa kweli!

...Tanzania yetu imejaa amani na utulivu, 'anaamini' nchi anaiacha kwenye 'safe hands' za Dr.MS na EL. Kuna nchi maraisi wao wakisafiri tu huko nyuma watu wanachukua nchi, (mfano Thai).

...Hivi, mawaziri wanasafiri 'kimya kimya', au ndio Mh Rais 'kawazibia', isipokuwa wale 'muhimu' anaoongozana nao kwenye hizi safari?. Kuhusu Mh Membe, bado nataka kuamini anatangulia kabla ya Rais kwenye hizo safari zake 'kusafisha njia'.

...All in all, namtakia kila la heri, maana 'mgaa gaa na upwa hali wali mkavu'! Enzi za JK Nyerere tuliwapokea 'vigogo' kama; Queen Elizabeth, Indira Gandhi, Pope John Paul nk, zama hizi 'madhali hawaji', bora rais awafuate huko huko!
 
when he was young he couldnt do good, now he cant do bad..... why are we mad ! ndio maana ya taito ya Muungwana, haiji kimchezomchezo, kama mliadhani kumuita Muungwana was just a name, there you go now !
 
when he was young he couldnt do good, now he cant do bad..... why are we mad ! ndio maana ya taito ya Muungwana, haiji kimchezomchezo, kama mliadhani kumuita Muungwana was just a name, there you go now !

kwi kwi kwi.........by the time unamaliza huu utetezi wako usio na mwazo wala mwisho, wallahi tena utakuwa na carpal tunnel syndrome. Ndugu yangu kibarua chako kigumu, pole weee!!!.
 
Kithuku,

wewe ukiwa na akiba ya sh alfu hamsini benki, una watoto wawili ambao wanasoma sekondari kwa karo ya alfu ishirini kwa mwaka, na mama yako mzazi ni mgonjwa na anahitaji tiba kwa sh alfu kumi na tano.

Wakati unafikiria cha kufanya, mjomba wako tajiri anakupa mwaliko wa kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya binti yake. ifahamike kuwa huyu mjomba wako aliwahi kukunyang'anya mali zako zote miaka ya nyuma ila siku za karibuni amekuwa anakupatia mkopo wa sh mia tano kila mwezi...Gharama ya kwenda kwa mjomba wako ni karibu sh elfu arobaini.

je, ingawa kwenda kuiitika mwaliko wa mjomba wako ni sehemu ya majukumu yako, wewe utakwenda kwa mjomba wako au utatumia akiba yako kupeleka watoto wako shule na kujaribu kumtibia mama yako?
Mwk,
Safi sana, mfano rahisi sana kueleweka yaani.......nadhani kada mpinzani huwa anaelewa mifano kama hiyo!!
 
mikutano hii hupangwa muda mrefu ili kusaidia upangaji wa ratiba
ya kiongozi. sasa kama itaonekana mialiko hiyo itagongana na shughuli nyingine muhimu za kitaifa au zitamfanya kiongozi kuwa njiani kwa kipindi kirefu basi ni kiongozi anaweza kutoa udhuru ili waandaaji wapate nafasi kukaribisha kiongozi mwingine au kumuomba mualikwa ateuwe mwakilishi. kama ni state visit basi unaweza tafutwa muda muafaka wa kufanya hiyo safari. hata siku moja mialiko hii si lazima kuhudhuria na hakuna adhabu ya kutokuudhuria zaidi ya wale wanaokualika kusita kukualika mara nyingine.
 
kwa hali ilivyo inaelekea mheshimiwa alijua kuna safari ya ufaransa na italy hata kabla ya kwenda marekani. kama vile anavyojua kuna safari ya uganda (commonwealth) na ureno (eu/au summit). labda iwe kwamba safari ya ufaransa aliyoifanya baada ya kutoka usa ilikuwa ya dharura sana nadhani angeweza subiri aiunganishe na safari yake ya sasa. kutokana na uwepo wa taarifa za safari muda mrefu kabla ya safari husika ni haki wananchi kushangaa na kuuliza maswali pale wanapohisi ratiba ingeweza kupangwa vizuri zaidi ili kulipunguzia taifa gharama na pia kujali afya ya kiongozi wao. kwani safari za mara kwa mara zinadhuru afya ati.
 
Yaani hii serikali imejaa watu wenye kiburi na jeuri ya hali ya juu sipata kuona,kuanzia mkuu wa kaya.
 
duuh jamani mwenzenu mie sina mbavu kabsaa inabidi nikanunue mpya..maana imebidi nisome mawazo yoote ya topic hii ya mkuu wetu wa nchi na allmost zote zimenivunja mbavu..
nasikitika zaidi kuwa zimenichekesha lakini nchi yetu yazidi teketea tartiiibuu...mtalii wetu ndo hivyoo anazidi kata mawingu tuu na by de tym akimaliza miaka yake kumi..nadhani atakua anajiuliza na wasaidizi wake ni nchi gani maarufu duniani hakwenda..na akizimaliza zoote ataanza hudhuria match za fainali za mpira wa miguu n.k cz ni vitu ambavyo ya show alikua anaviota toka utotoni so now he has got the means kutimizia ndoto zake..
aliyeongelea suala la medical checkup..je ni kwenda kuchekiwa au ni kwenda ku......... kuna tofauti ya kuchekiwa na kujulikana kuwa waumwa kitu flani so ukienda hospitali wafuata tiba tuu na sio kuchekiwa tenaaa
jamani wa tz tumeambiwa tutulie..na kufunga mikanda ndege yapaa..so tuwe na imani na mapilot wetu hata kama twaona yawaka moto au yazama baharini sie tutulie,na kuamini ndege yapaa!!!!ha ha ha ha haaa
Mungu ibariki Tanzania japo wengi wetu tuna uchungu
 
Kama makada wa SISIEMU wamwagavyo sera huko mikoani kwamba Safari za nje za Kikwete ni za kutafuta wafadhiri kwa hiyo zinamanufaa.
Sijui hilo nalo limo kwenye Ilani ya uchaguzi ya SISIEMU?

Watanzania wengi wanaamini kwamba Misaada ni haki yao ya kuzaliwa na bila misaada hawawezi endelea. Watanzania wenye akili kama hiyo wako radhi kuuza nchi yao kwa mkoloni kama tu atawaahidi misaada toka kwao.

Kwa maana hiyo kama hatuna mtu wa aina ya kikwete ambaye ni hodari wa kusafiri na kuomba huko ughaibuni nchi haitaendelea kamwe.

Tunaachia Mabilioni ya $$ kwa mwaka kwa wawekezaji halafu rais Mzima aenda pigia magoti wanaume wenzie kuomba vijidolla vichache. Unajua hata wazungu wenyewe huwa hawaamini kama hila zao ndogo zimeweza kuwachanganya kabisa viongozi wa Afrika.

Kiongozi wa Afrika akiambiwa nchi yake ni rafiki mkubwa na nchi ya ughaibuni anakenua meno kama Panya kabanwa na mlango.

Lakini pengine jambo jingine kubwa ni kukimbia Makombora yaibukayo kila siku na zaidi makombora ya Dr Slaa.

Watu anaosafiri nao akiwaita wafanya biashara ni marafiki zake na wapambe zake wasio na hisia wala mwelekeo wa kufanya biashara.
Kuna washika tunguri.
Kuna makuwadi wa kusaka mademu.
Kuna mademu wake regular.
Kuna mashga ake wa karibu ambao kazi zao bado sizijui ambao mionendo yao inaleta maswali mengi sana!

Wanaitwa wafanya biashara ili kutupiga maboya na kuzuga kwamba ana nia ya dhati ya kukuza uchumi.
Huyu Mkwere kakua kimo na ukubwa wa kichwa tu akilini mwake bado ana mambo kama kijana mcheza Disco wa miaka 19. Watanzania tumeliwa.
Suluhisho la matatizo ya Tanzania lipo Tanzania na wanalo watanzania wenyewe. Matatizo yetu ya TAnzania yatatatuliwa na sisi wenyewe na si mghaibu yeyote.
Rais hawezi kutatua matatizo kwa kuongeza safari za nje au kwa kuhudhuria kila mkutano aalikwao.
Hii ni dalili moja kwamba hana Priority list ya mambo muhimu ya kufanya ndani ya nchi ndiyo maana kila uchao yuko majianni ku fulfill prioriy za viongozi wa magharibi.

Kwenye moja ya mahojiano yake na waandishi wa habari Tanzania alishawahi sema;

Wakuu wa nchi za magharibi, kama Tony wa uingereza walikuwa wananamwalika je angeacha kwenda??

(Makofi toka kwa waandishi kuafiki fact)

Ukiarikwa ni lazima uende?
Ukikaribishwa kula ni lazima ule?
Tena pengine huko apendako kwenda kila siku wanamlisha Konokono wale wa njano,nyoka na nyama ya Tumbiri yeye hajui anakula!!!

Tukiwa na Rais anayeitikia kila mwaliko,kama ilivyo sasa,tuna balaa kubwa la kitaifa .
 
aisee hiyo listi yako imenifurahisha..washika tunguri,mademu regular na ma kuwadi wa mademu...so raisi wetu anashow how akienda nchi za watu anaenda tu represent wa tz nchi za nje..ndo anatutaftia wafadhili hivyoo?no wonder why anatakiwa aende pia kwa ajili ya afya........
 
Back
Top Bottom