Jk kuwa mgeni rasmi wa sherehe za may mosi?

Kiby

JF-Expert Member
Nov 16, 2009
6,899
4,623
Kesho kutwa ndio sikukuu ya wafanyakazi ijulikanayo kama mei mosi. Kama ilivyo ada mkuu wa nchi huwa ndie anaealikwa kuwa mgeni wa heshima na ikitokea ana shughuli nyingine humtoma mmoja wapo wa wasaidizi wake kumwakilisha. Tofauti ya mwaka huu viongozi wa wafanyakazi poamoja na kutangaza mgomo utakaoanza tarehe tano, pia waliapa kutomwalika kiongozi yeyote wa serikali katika sherehe hizo ikiwa ni pamoja na rais wa nchi. Swali langu ni je msimamo wa wafanyakazi bado upo pale pale? Na kama upo pale pale mgeni wao wa heshima ni nani? Au walishabadilishwa msimamo kama ilivyokuwa enzi za kina Mpangala? Wasi wasi huu unasababishwa na kawaida yetu waTz kulamba chenga nyingi lakini goli halifungwi. JF kuna update gani kuhusu hili?
 
Suala letu liko palepale.
Kikwete akihudhuria sherehe, tutamuona amehudhuria kama mfanyakazi mwingine yeyote.
Mrisho mpoto ndiye anayetarajiwa kuwa mgeni rasmi.
 
Suala letu liko palepale.
Kikwete akihudhuria sherehe, tutamuona amehudhuria kama mfanyakazi mwingine yeyote.
Mrisho mpoto ndiye anayetarajiwa kuwa mgeni rasmi.

.
Ahsante sana kwa taarifa. Wakifanikisha hilo litaondoa shaka kwamba shabaha ya viongozi wa wafanyakazi haikuwa ya kusaka uwanja wa kuahidiwa madaraka na serikali, bali kutafuta masilahi ya wafanyakazi wote kwa manufaa yao na Taifa kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom