Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,463
- 113,533
Wanabodi
Nilipata ka vakasheni kafupi, hivyo nikaamua kwenda kujipumzisha mikoa ya Moshi na Arusha
juzi na jana.
Baada ya mapumziko mafupi ya juzi yalitosha na jana nikaitumia kusafisha macho kwenye harakati za kisiasa mjini Moshi na Arusha.
Habari kubwa niliyokumbana nayo ni kuwa CCM ina hali mbaya sana Jimbo la Moshi Mjini ambako Mzee Philemon Ndesamburo wa Chadema, bado anakubalika sana. Pia CCM iko kwenye hati hati za kulipoteza jimbo la Hai, ambapo Freeman Mbowe anakubalika sana, na kwa upande wa Arusha, Jimbo la Karatu ndilo jimbo pekee linayoinyima usingizi CCM ili kuligomboa jimbo hilo ambalo ndilo roho ya Dr.Slaa.
Ili kujizatiti kwa mpambano huo, inasemekana CCM imemuomba Mwenyekiti wake na mgombea wa urais, kupiga kambi mikoa hiyo, kufanya kampeni ya nguvu ili kupata ushindi.
Japo JK alishafanya kampeni yake huko, sasa atarejea tena wiki ijayo kwa kampeni ya funga kazi, kabla ya kurejea jijini Dar kukamilisha kampeni hizi siku ya Jumamosi 30 Octoba katika viwanja vya Jangwani.
Kwa maoni yangu, JK atajiaibisha bure tuu kutaka kuking'oa kisiki cha mpingo kwa kutumia panga butu!. Kisiki cha mpingo hakikatika hata kwa shoka, bali huchimbwa kukizunguka mpaka kuufikia mzizi mkuu wa katikati ambao hukatwa kwa shoka kali, ndipo hung'ooka!.
Mgombea wa CCM kwa Moshi mjini, Salakana, anmaendelea kwa kampeni ya nyumba kwa nyumba nyakati za asubuhi na jioni kwenye mikutano ya hadhara. Jana alikuwa mitaa ya Bondeni na kila alipopita alishangiliwa na kuahidiwa kura zote ni kwake, japo sina uhakika kama ahadi hizi ni kiini macho kwa kumuonea aibu akiwa mtaani kwao, au ndio kitakachofanyika Octoba 31.
Kwa Upande wa Arusha, jana nimehudhuria kampeni za Mgombea wa Chadema, Godbless Lema pale Levolosi Desemba na kumalizia kampeni za Mgombea wa CCM, Dr. Batilda Burian Pale Kaloleni, kwa mikutano ya jana, ni CCM ilifunika, sijui kwa ile iliyotangulia maana sikuwepo!.
Kwa nini CCM haina wasiwasi na jimbo la Vunjo?. Nadhani ni kwasababu Chadema, NCCR na TLP wanaparurana katika vita vya panzi, hivyo CCM imepozi pembeni kama Kunguru kusubiri kulitaka kiulani!.
Nilipata ka vakasheni kafupi, hivyo nikaamua kwenda kujipumzisha mikoa ya Moshi na Arusha
juzi na jana.
Baada ya mapumziko mafupi ya juzi yalitosha na jana nikaitumia kusafisha macho kwenye harakati za kisiasa mjini Moshi na Arusha.
Habari kubwa niliyokumbana nayo ni kuwa CCM ina hali mbaya sana Jimbo la Moshi Mjini ambako Mzee Philemon Ndesamburo wa Chadema, bado anakubalika sana. Pia CCM iko kwenye hati hati za kulipoteza jimbo la Hai, ambapo Freeman Mbowe anakubalika sana, na kwa upande wa Arusha, Jimbo la Karatu ndilo jimbo pekee linayoinyima usingizi CCM ili kuligomboa jimbo hilo ambalo ndilo roho ya Dr.Slaa.
Ili kujizatiti kwa mpambano huo, inasemekana CCM imemuomba Mwenyekiti wake na mgombea wa urais, kupiga kambi mikoa hiyo, kufanya kampeni ya nguvu ili kupata ushindi.
Japo JK alishafanya kampeni yake huko, sasa atarejea tena wiki ijayo kwa kampeni ya funga kazi, kabla ya kurejea jijini Dar kukamilisha kampeni hizi siku ya Jumamosi 30 Octoba katika viwanja vya Jangwani.
Kwa maoni yangu, JK atajiaibisha bure tuu kutaka kuking'oa kisiki cha mpingo kwa kutumia panga butu!. Kisiki cha mpingo hakikatika hata kwa shoka, bali huchimbwa kukizunguka mpaka kuufikia mzizi mkuu wa katikati ambao hukatwa kwa shoka kali, ndipo hung'ooka!.
Mgombea wa CCM kwa Moshi mjini, Salakana, anmaendelea kwa kampeni ya nyumba kwa nyumba nyakati za asubuhi na jioni kwenye mikutano ya hadhara. Jana alikuwa mitaa ya Bondeni na kila alipopita alishangiliwa na kuahidiwa kura zote ni kwake, japo sina uhakika kama ahadi hizi ni kiini macho kwa kumuonea aibu akiwa mtaani kwao, au ndio kitakachofanyika Octoba 31.
Kwa Upande wa Arusha, jana nimehudhuria kampeni za Mgombea wa Chadema, Godbless Lema pale Levolosi Desemba na kumalizia kampeni za Mgombea wa CCM, Dr. Batilda Burian Pale Kaloleni, kwa mikutano ya jana, ni CCM ilifunika, sijui kwa ile iliyotangulia maana sikuwepo!.
Kwa nini CCM haina wasiwasi na jimbo la Vunjo?. Nadhani ni kwasababu Chadema, NCCR na TLP wanaparurana katika vita vya panzi, hivyo CCM imepozi pembeni kama Kunguru kusubiri kulitaka kiulani!.