JK kukiri hali ya fedha serikalini ni mbaya

Sasa Kikwete amekiri kwamba Serikali ina ukata wa kutisha. Je, kuna hatua zipi ambazo Serikali inachukua ili kuongeza mapato yake na wakati huo huo kupunguza matumizi ya anasa kama vile mashangingi kwa maofisa wengi wa juu Serikalini ambao gharama kubwa za kuyaendesha haya ikiwemo mafuta na matengenezo yanatokana na pesa za walipa kodi? Vipi kuhusu kukata safari za nje kwa kwa kipindi cha miaka mitatu ili kupambana na ukata huu? Vipi kuhusu kufanyia marekebisho ya mikataba ya uchimbaji wa dhahabu ambayo aliahidi kufanya katika kampeni za 2005 ili nchi inufaike na na rasilimali zake? Je haiwezekani kuongeza mrahaba ukafikia hata 205 au zaidi na kuanza kuwatoza kodi ya mapato wachimbaji wote wa madini ili kutunisha mfuko wa hazina? Je kuna mkakati wowote kati ta Serikali na TRA kuongeza idadi ya walipa kodi nchini na kuwabana wale wakwepaji wakubwa wanaokwepa kulipa mabilioni ya kodi kila mwaka? Nasikia nchi yetu pamoja na kuwa population inasemekana ni 40 million lakini idadi ya walipa kodi inadaiwa haifiki hata laki 7!!!! Je kuna mkakati wa kuongeza idadi hii ili miaka mitano ijayo idadi ya walipa kodi iongezeke na kuwa mara 10 au hata zaidi ya hii sasa? Au ndio kishakubali kwamba Serikali ina utata basi yamekwisha wanaendelea kubweteka ili kumsubiri Mungu atuletee neema ya mapato kuongezeka na hivyo kuondoa utata uliokuwepo?

....na haya madeni waliyolipa ni madeni gani hayo!? Nadhani Watanzania wengi tungependa kuyafahamu ni madeni yepi anayoyazungumzia Kikwete na kama nchi iliingia madeni hayo kwa maslahi ya Watanzania au kwa ajili ya kununulia mashangingi?
 
...Wamethubutu, wameweza na sasa wanasonga mbele katika kuiangamiza nchi.
 
kwenye hotuba yake hakutumia neno hali ni mbaya ni kwa madhumini gani mwandishi ameongeza chumvi?
 
kumbe gazeti lenyewe ni la udaku mwananchi lina bifu na JK....mmmmh nina mashaka.
 
....Alikuwa wapi tangu August 2011 ambapo kulikuwa na dalili nyingi tu kwamba nchi imefilisika? Je, kukiri tu bila kuchukua hatua za kupambana na hali hiyo kwa kupunguza matumizi ya anasa na kutafuta mikakati mbali mbali ya kuongeza mapato kunasaidiaje nchi!? au anasubiri miezi sita mingine ndio aje na mikakati ya kupambana na ukata huo?
 
Labda hali mbaya imesababishwa na shetani.



shetani wa mtu ni mtu mwenyewe....huyo bwana hana maono tena ni jukumu la watanzani kuzuia hali hii...anaaibisha sana na kutia aibu......hapo alipo anaamini nchi haiwezi kuendelea bila uwekezaji!!!! hii ni aibu.....amkeni watanzania
 
Tuambie ww kuhusu raisi wako na mipa
ngo ya nchi yako au ww wa italy mwenzetu


mahali nilipo hatuna rais tuna waziri mkuu ambaye si kama huyo anayelia lia huko....na nchi inasonga vizuri.....viongozi wa tanzani kazi yao kusema uongo na kutangaza wengine kuwa wamekufa.......kwa hali hiyo nchi haiwezi kupiga hatua....wananhi badilikeni mzuieni kusafiri huyo mtu wenu.........
 
wale wale mnaofikiria kwa kutumia kile kiungo (meya wa jiji la dsm).unashindwa kuelewa kuwa mkapa aaliingia mikataba mingi ya uatata sasa kikwete ndio ana clear hayo ma gape,we unakurupuka na kuja hapa na uharo wako.shame on yuuuuu
Inahitajika uwe mlemavu wa akili ili uje na utetezi fyongo kama huu.
 
fumueni pae hazina muondoeni huyo waziri wa fedha fukuzia mbali kabisa pale walau akae kigoda,,WALAU huyo ana maono kuliko huyu aliyepo....kisha pale BOT muondoeni huyo gavana lakini tatizo lingine gavana huyo hana meno maan mambo mengi yanaamulia na the real gavana and the head of state Rostam Aziz......mkiweza kumthibiti huyu kila kitu kitakuwa sawa....kwa kuanzia anzeni na huyo jk....hata imf wanajua na walishamuonya juu ya uhaba wa pesa lakini hasikii....
 
hao mnaoita usalama wa taifa nao hovyo kabisa.....kazi yao kubwa ni kulinda maslahi ya wakubwa tu...usalama wa taida umegawanyika sana,,zamani yalikuwa makundi saba ila sasa limeongezeka moja yamekuwa nane na kila moja linafanya kazi chini ya mtu flani.....huku wakilipwa na serikali.....sasa hapo nchi itaendelea...wameacha majukumu yao ya msingi kabisa katika kuilinda nchi.......jukumu sasa ni la wananchi wenyewe kuamka na kusema sasa basi.......zaidi ya hapo endeleeni kugugumia kwa maumivu...
 
Wewe unataka Rais akupe pesa? wewe unampa nini?


hana chochote cha kunipa huyo mtu wako.....hana lolote la maana...hataki kuambiwa ukweli anachotaka ni kupambwa ka maneno mazuri kama unavyofanya wewe wakati anaungua.....sasa hivi agenda yenu kubwa ni vazi la taifa utadhani lina tija sana....akiambiwa ukweli anakasirika na kutuma vijana wake kuua....
 
Ya kwanza ipi?


iraq na afganistan then tanznaia...hizi mbili za mwanzo zimekuwa vitani miaka na mika...ninyi huko mnaimba amani na utulivu miaka 50 sasa..lakini hakuna lolote la maana.....mmekabidhi nchi kwa wezi na wanyang'anyi wakubwa.........
 
Wewe hujui hata kuwa Tanzania imepigana vita vingi tu? Umesahu Iddi Amin? umesahau Msumbiji? umesahau juzi Comoro? au zile zilikuwa lelemama?
tatizo la vita na comoro ni nini? tanznaia ilivamiwa na comoro? na msumbiji lini imepigana na tanzania??...lini kikwete alitangaza vita dhidi ya comoro kwa wananchi??.....acha ushabiki wa ajabu we mwanamke.....au kuna kitu hukielewi??......mambo ya ajabu kweli.......mwambie huyo raisi wako huyo hana lolote analofanya na sasa asitafute hurumu kwa kusema eti hakuna pesa..rais mzima unabana puna na kusema''' serikali ina hali mbaya sana kifedha''....hata aibu hana
 
Watanzania ambao hamfaidiki ni wavivu wa kutupa amma mmezubaa. Nawashangaa sana mnapopiga kelele kuna mali, kuna mali. Zako? kwanza zifanyie kazi ziwe zako halafu uone mtu anakunyang'anya ndio ulalamike. Sisi tuliona Nyerere tu ndio alidhulumu mali za watu kwa kuzitaifisha. Lakini kwa sasa, fanya biashara, kazi, chimba, chimbuwa uwezavyo, kikomo ni uwezo wako tu wakufikiri na kutenda.

Hiyo ndio kama kusifia "Bakhresa ana mali bwana, tajiri sana", "Mengi ana mali bwana, tajiri sana", Zako? walifanya kazi kwa bidii, na wewe unangoja nini?

Tena Tanzania hii wala huhitaji mtaji mkubwa wala huhangaiki. Njoo, uone kwangu, nimeweka kuku wa kienyeji, nimeanza na jogoo mmoja na kuku wa tatu (AlhamduliLlah) sasa hivi wako kama mia tatu, within 3 Years. Mbali niliowauza, mbali nilowala, mbali nakula mayai ya kienyeji kila siku. Unajuwa capital yake haijafika hata 50,000 leo nikiwauza kama walivyo wataniingizia sio chini ya 2 m. na ya nini niwauze wakati kila mwezi napata mshahara wa laki tano kwa hao kuku tu.

Mbali ya mbuzi, ng'ombe, bata. Ambao msingi wao ni mdogo sana mradi ujitume tu

Wacheni uvivu, fanyeni kazi.

na kitu kama inflation unatolea jasho kivipi kukabiliana nacho.. Au mkulima wa korosho afanye bidii ipi ili afaidike na ukulima wake...
 
'Wananchi watakula majani'
Nafikiri umefika wakati wa serikali kupunguza misamaha ya kodi isiyo ya lazima na kuacha fumbia macho biashara za viongozi.Kodi iwe ni kwa wote wenye vipato.

Kwanini raisi asipunguze watendaji wake e.g. manaibu waziri wanafanya nini kama makatibu wa wizara wapo? Wakuu wa wilaya au mikoa one of them should go etc. Kama tuko kwenye tight budget si ni lazima tupunguze spending ilituweze kumudu majukumu muhimu? I would think this is a no brainer! Kuna watu wamejazana kwenye hizo halmashauri za miji hawana kazi wana-report tu na wanatoka kabla hata ya masaa ya kazi kuisha (kwenda kwenye biashara zao). Mr President punguza safari, punguza wapambe, ondoa posho kwa wabunge, kodi kodi kodiiiiii- uswaiba unaimaliza hii nchi Mr President!. If your real serious mchangamshe mwanasheria wako awa-prosecute mafisadi then taifisha mali/pesa zao wale watakao kutwa guilty. Mr President unahitaji unawatendaji wachache lakini makini wanaojua kutumia resources wisely. Kinyume cha hapo wimbo ni ule ule
 
Back
Top Bottom