Mwalufunamba
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 211
- 129
Mwaka 2005 Jakaya Kikwete alijibu mara mbili kwa waandishi wa habari sehemu mbili tofauti, katika nyakati tofauti, kuwa sifikirii kushindwa. Majibu hayo aliyatoa baada ya kuulizwa swali kwamba itakuwaje iwapo licha ya maandalizi yote aliyofanya atakosa kuteuliwa{na CCCM kuwa mgombea wa Urais}
Akiandika makala yake ya tarehe 8 Agosti, 2010 yenye kichwa cha JK bado hafikirii kushindwa? Ansbert Ngurumo anasema,
Lengo ni kuhakikisha kwamba kwa njia safi au chafu, mtu wao anashinda. Muhimu kwao si wananchi kuchagua mtu wanayemtaka, bali kuhakikisha kwamba yule asiyefikiria kushindwa, anashinda.
Huu ni uchafu wa kisiasa. Unajenga urithi mchafu kwao na vizazi vyao. Wanacheka leo, lakini wanaweza kujikuta wanaliingiza taifa katika maafa yale yale tunayosikia katika nchi nyingine
Mwishoni alimalizia kwa kusema Wafanye watakavyo, lakini hili halikubaliki. Wanatengeneza bomu ambalo siku litakapolipuka, wao pia hawatabaki salama.
Makala hiyo haikuifurahisha Ikulu, ikaisakama MAELEZO, nao wakamita Ngurumo aliyekwenda pamoja na Mhariri wa Tanzania Daima, Absalomu Kibanda pale MAELEZO. Katika kikao hicho, Ngurumo anaandika kuwa Mkurugenzi Msaidizi wa MAELEZO (kwa wakati huo) Rapahel Hokororo alisema, Mashuja wote hawako hai Naye akajibiwa na msomaji wa www.ngurumo.blogspot.com kuwa Raphael Hokororo, hata mashujaa wakifa, hawafi na ushujaa wao; bali huuacha nyuma wananchi wakautumuia kujikomboa kimawazo, kisiasa, kiuchumi, na kijamii.
Akiandika makala yake ya tarehe 8 Agosti, 2010 yenye kichwa cha JK bado hafikirii kushindwa? Ansbert Ngurumo anasema,
Lengo ni kuhakikisha kwamba kwa njia safi au chafu, mtu wao anashinda. Muhimu kwao si wananchi kuchagua mtu wanayemtaka, bali kuhakikisha kwamba yule asiyefikiria kushindwa, anashinda.
Huu ni uchafu wa kisiasa. Unajenga urithi mchafu kwao na vizazi vyao. Wanacheka leo, lakini wanaweza kujikuta wanaliingiza taifa katika maafa yale yale tunayosikia katika nchi nyingine
Mwishoni alimalizia kwa kusema Wafanye watakavyo, lakini hili halikubaliki. Wanatengeneza bomu ambalo siku litakapolipuka, wao pia hawatabaki salama.
Makala hiyo haikuifurahisha Ikulu, ikaisakama MAELEZO, nao wakamita Ngurumo aliyekwenda pamoja na Mhariri wa Tanzania Daima, Absalomu Kibanda pale MAELEZO. Katika kikao hicho, Ngurumo anaandika kuwa Mkurugenzi Msaidizi wa MAELEZO (kwa wakati huo) Rapahel Hokororo alisema, Mashuja wote hawako hai Naye akajibiwa na msomaji wa www.ngurumo.blogspot.com kuwa Raphael Hokororo, hata mashujaa wakifa, hawafi na ushujaa wao; bali huuacha nyuma wananchi wakautumuia kujikomboa kimawazo, kisiasa, kiuchumi, na kijamii.