JK Kanyaga twende, ukombozi wa watanzania u mikononi mwako!

Waberoya

Platinum Member
Aug 3, 2008
15,169
10,783
Gesi (15kg) from 45,000 to 70,000
Sadolin ya mkaa iliyokuwa inauzwa 1500 sasa ni 3000

kwa sisi wajenzi nondo zile za 12,000 sasa ni 17,000! kwa kifupi vifaa vya ujenzi vimepanda sana! kama hujajenga kihalali....

Mechi inaendelea natamani hali hii iendelee ifikie watu kushindia maji tu! shida zikiongezeka haya yatatokea:

1. Akili ya kuchagua viongozi bora itakuja tu!

2. watu watakuwa sensitive na hali ya nchi na sio kukurupuka tu

3. Mijadala ya kidini haitakuwepo, maana woote wamakonde, wamalira, wanyakyusa, wachaga, wangindo, wapogo wote wana suffer the same. waislamu na wahindu, wakristo na wapagani watapata shuruba ile ile! tutaona kama akili hazitakuja kichwani,

4. wale wasomi 'graduate' wanaotembelea magari ya mikopo na kupanga Sinza, huku wakiwa weredi wa vikao vya harusi na kushinda kuchoma mafuta yaliyopanda bei HUKU WAKIWA HAWANA MPANGO NA ISSUE ZA KITAIFA wataamka!!

we need same platform ili TUELEWANE!!, shida tu zitawakomboa watanzania, kelele tumepiga watu bado wanawachagua CCM!!!

Acha maisha magumu yaongezeke JK kanyaga twende!!!!
 
Kindoo cha mafuta kiwe 50,000 na kilo ya unga iwe 5,000, dagaa iwe 20,000, nauli ya kuendea kazini kwa siku iwe 5000. Kima cha chini baada ya makato kiendelee kuwa 70,000 hadi 150,000.

Wizi uendelee kushika kasi kama ulivyo sasa huku kwetu Temboni ambapo wezi wa kutumia silaha ndio wenye hatamu za utawala ambapo polisi huja kwenye tukio baada ya masaa 2 baada ya uhai kutoweka na watawala kuchikichia.

Shule za kata na za mchepuo wa kiswahili (msingi) zenye walimu wasiofikia 5 kwa wanafunzi wasiopungua 500 ziendelee hivyo hivyo. Kwani hili ni kundi maalumu la watawaliwa. Wa kwao si wanasoma st.. na ughaibuni?

JK kanyaga, hata mtoto wa nyani alipomuuliza ***** mwisho wa mpaka wa shamba lao la mahindi ili asile kisicho chao, jibu aliloambulia ni kuwa Kula tu mwanangu wenyewe watakuja kugawa/kuweka mpaka.
 
Waberoya... its like you were with me this evening, I am coming back from a night out.... we just paid 700 kwa maji ya kilimanjaro, talked about how caring JK is to mafisadi, how sad it is that his family suffers from our grievances.

we also talked about how romantic he is to rostams and the likes, how smiley he is to waziri wa nishati bwana ngeleja (imbecile); some went even further kwamba his acts are because he and his family have never purchased even a pen since he became a president kwahiyo hizo bei kwake ni kizungumkuti

as we were dropping someone in lamadi (magu)... i nice chap reminded us that presidaa is the most handsome in EAF

sadly, JK is turning his image/personality/presidency/ambitions into a circus
 
Na ratiba ya umeme iwe siku 3 badala ya 8 kwa siku!! Hapo ndio hata anayejifanya hana akili atazipata!!! :A S 39:
 
Jamani.. uchaguzi una matokeo yake. Binafsi sitaki kabisa kusikia mwana CCM au mtu yeyote aliyeunga mkono JK kurudi madarakani analalamikia iwe mafuta au dawa ya vipodozi. Watu lazima wajifunze kuishi na maamuzi waliyoyachukua.
 
Mkuu MKJJ, mbona tayari wana CCM wamenza kulalamika kuwa prezidaa anaonewa na kuhujumiwa, they even went fsr kwa kusema JK ni mtu safi kama haiba yake. Kwa kweli kusikia maneno haya kwa mtanzania mwenzangu nahisi kama tusi!!! Yaani mtu anahutubia kuwapa wananchi heri ya mwaka mpya, bado anasisitiza dhamira yake kuilipa DOWANS!!!

What a he...k!!
 
Yazidi kuwa magumu paka akina Topical and the co wajue! Na bado nauli inapanda....hureeeeeeee! maisha yanazidi kuwa magumu kwa nguvu zaidi, ari zaidi na kasi zaidi!
 
Na huo ugumu wa maisha uwaendee zaidi wale waliochagua ccm, hawataki mabadiliko ukiwauliza ccm imewafanyia nini? wanajibu ooh baba zetu ni ccm nasi ni ccm! Pumba tupu kichwani mwao.
 
.. ama kweli hii ni dhahma.. na inakatisha tamaa. Pamoja na kupanda gharama za kuishi kuna adha nyingine kibao zinahusishwa na awamu hii ya mlegevu - foleni mabarabarani, foleni kwenye mabomba ya maji, foleni kwenye mahospitali, foleni kwenye mabenki na ATM, kuongezeka vibaka (kutokana na maisha magumu), kuongezeka uchafu mitaani, kuongezeka kwa nzi na mbu mitaani, kuongezeka kwa harufu kali kwenye vyoo vya public (yaani hadi airport), etc.,etc. Eee Mungu ibariki TZ tuvuke 2015 salama.
 
Tatizo kuna wengine kijijini sijui kama wanajua kuwa ugumu wa maisha unasababishwa na serikali.

Ila kuna mijitu ya mijini inapewa kanga, tshirts,............. wanashabikia ngoja tuumie wote labda watapata akili. Ingawa wabongo wengi wanasahau haraka.
 
Gesi (15kg) from 45,000 to 70,000
Sadolin ya mkaa iliyokuwa inauzwa 1500 sasa ni 3000

kwa sisi wajenzi nondo zile za 12,000 sasa ni 17,000! kwa kifupi vifaa vya ujenzi vimepanda sana! kama hujajenga kihalali....

Mechi inaendelea natamani hali hii iendelee ifikie watu kushindia maji tu! shida zikiongezeka haya yatatokea:

1. Akili ya kuchagua viongozi bora itakuja tu!

2. watu watakuwa sensitive na hali ya nchi na sio kukurupuka tu

3. Mijadala ya kidini haitakuwepo, maana woote wamakonde, wamalira, wanyakyusa, wachaga, wangindo, wapogo wote wana suffer the same. waislamu na wahindu, wakristo na wapagani watapata shuruba ile ile! tutaona kama akili hazitakuja kichwani,

4. wale wasomi 'graduate' wanaotembelea magari ya mikopo na kupanga Sinza, huku wakiwa weredi wa vikao vya harusi na kushinda kuchoma mafuta yaliyopanda bei HUKU WAKIWA HWANA MPANGO NA ISSUE ZA KITAIFA wataamka!!

we need same platform ili TUELEWANE!!, shida tu zitawakomboa watanzania, kelele tumepiga watu bado wanawachagua CCM!!!

Acha maisha magumu yaongezeke JK kanyaga twende!!!!

sina cha kuongezea hapo
 
Jamani.. uchaguzi una matokeo yake. Binafsi sitaki kabisa kusikia mwana CCM au mtu yeyote aliyeunga mkono JK kurudi madarakani analalamikia iwe mafuta au dawa ya vipodozi. Watu lazima wajifunze kuishi na maamuzi waliyoyachukua.

JK chaguo la Mungu, Mungu huyu huyu tunayemsingizia kila baya.
 
JK chaguo la Mungu, Mungu huyu huyu tunayemsingizia kila baya.
Hivi yule aliyesema Chaguo la Mungu yupo wapi siku hizi? pengine hata kuomba radhi anaona haya..Unajua ndio tabu ya kuongea sana, matokeo yake ni aibu na kukosa credibility mbele ya watz.
 
Yes, life should keep on being so difficult that tanzanians may eventually relate it with jk's leadership and have a lesson before the coming election.
 
Hivi yule aliyesema Chaguo la Mungu yupo wapi siku hizi? pengine hata kuomba radhi anaona haya..Unajua ndio tabu ya kuongea sana, matokeo yake ni aibu na kukosa credibility mbele ya watz.

Dawa ni nini? uchaguzi? siasa? what do you think.
 
Dawa ni nini? uchaguzi? siasa? what do you think.
Dawa ni kuanza upya, kwa kuweka mfumo mpya wa kujitawala usiotegemea maono ya vikundi au individuals. Mfumo utakaohakikisha uwajibikaji, uhuru, ubunifu, uwazi et c ..pengine starting point iwe katiba.
 
Dawa ni kuanza upya, kwa kuweka mfumo mpya wa kujitawala usiotegemea maono ya vikundi au individuals. Mfumo utakaohakikisha uwajibikaji, uhuru, ubunifu, uwazi et c ..pengine starting point iwe katiba.

Unasuggest kipengele cha Katiba kitakachoaccomodate haya maoni yako kisomeke vipi, I mean toa mfano.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom